McLaren
JF-Expert Member
- Feb 19, 2025
- 889
- 2,863
Umoja wa Walimu Wasio na Ajira Tanzania umesema unaendelea kufuatilia maombi ya ajira yaliyowasilishwa serikalini. Kupitia taarifa yake, uongozi wake umeeleza kuwa suala la ajira za walimu ni kipaumbele na tayari umeandika barua kwa Ofisi ya Rais Utumishi pamoja na Ofisi ya Rais Ikulu kueleza hoja za walimu wasio na ajira.
Taarifa yao ilisema "Kwa kutambua umuhimu wa matakwa ya walimu wasio na ajira uongozi wa NETO umeanza ufuatiliaji wa karibu ambapo wizara tatu ambazo zinashusika kwa ukaribu na masuala ya ajira na vijana imekuwa ndio kipaumbele cha kwanza kwa ajili ya kukumbusha kuhusu makala iliyowasilishwa hapo mwanzo"
Pia umefikisha maelezo kwa Waziri wa Elimu ukisisitiza umuhimu wa hatua za haraka katika sekta ya elimu. NETO imetoa wito wa umoja kwa walimu wasio na ajira na kuhimiza Serikali kuendelea kushirikiana nao ili kufanikisha ajira kwa vijana.
"Pia kwa umuhimu zaidi uongozi umeiandikia barua Ofisi ya Rais Maendeleo ya vijana ambapo ipo chini ya waziri Mhe Arthur Nanauka kwa ajili ya kuitambulisha NETO kama muunganiko wa vijana walimu wasio na ajira na kutoa matakwa ya walimu wasio na ajira kwa ajili ya ufuatiliaji zaidi ikiwa ndiyo wizara mpya ambayo inahusika na maendeleo ya vijana"
Taarifa yao ilisema "Kwa kutambua umuhimu wa matakwa ya walimu wasio na ajira uongozi wa NETO umeanza ufuatiliaji wa karibu ambapo wizara tatu ambazo zinashusika kwa ukaribu na masuala ya ajira na vijana imekuwa ndio kipaumbele cha kwanza kwa ajili ya kukumbusha kuhusu makala iliyowasilishwa hapo mwanzo"
Pia umefikisha maelezo kwa Waziri wa Elimu ukisisitiza umuhimu wa hatua za haraka katika sekta ya elimu. NETO imetoa wito wa umoja kwa walimu wasio na ajira na kuhimiza Serikali kuendelea kushirikiana nao ili kufanikisha ajira kwa vijana.
"Pia kwa umuhimu zaidi uongozi umeiandikia barua Ofisi ya Rais Maendeleo ya vijana ambapo ipo chini ya waziri Mhe Arthur Nanauka kwa ajili ya kuitambulisha NETO kama muunganiko wa vijana walimu wasio na ajira na kutoa matakwa ya walimu wasio na ajira kwa ajili ya ufuatiliaji zaidi ikiwa ndiyo wizara mpya ambayo inahusika na maendeleo ya vijana"