Wakuu nimechanganyikiwa - daktari yupi yuko sahihi?

georgina george

Senior Member
Dec 19, 2012
114
30
Salaam Zenu Wakuu!

Mimi ni mama wa watoto watatu, wote wa kike. Watoto wote hao nilijifungua kwa njia ya operation. Wakati wa mimba ya kwanza niliambiwa na Daktari kuwa siwezi kujifungua kwa njia ya kawaida hivyo nilifanyiwa Emergency Caesarian ili kunusuru maisha yangu pamoja na mtoto. Mimba mbili zilizofuata nilifanyiwa a Planned Caesarian. Pamoja na watoto wote watatu kuzaliwa kabla ya muda (premature), thank Lord, watoto wote wamekua vizuri wakiwa na afya njema.
First born yuko Kidato cha 2 mwaka huu, wa pili Class 5 na watatu yuko Chekechea.

Mwaka jana (2013) mimi & my husband tuliamua kutupa karata zetu za mwisho, japo mwenzangu mwanzoni alikataa akishauri kuwa watoto watatu wanatosha regardless of being the same gender. Nilitumia busara sana kumshauri mwenzangu kuhusu kutengeneza mtoto mwingine wa nne na wa mwisho. Lengo langu likiwa at least kubahatisha a baby boy, Lord knows!

Mnamo Aug, 2013 sikuona siku zangu, obviously nilijua kitu kimenasa!
Nisiwachoshe sana; in short lipo tatizo linalonipa wasi wasi ambalo ndilo lengo kuu la kuleta hapa jamvini thread hii.

Nimekuwa niki hudhuria clinic mara kwa mara na pia Daktari alifanya calculations zake na kunijulisha kuwa tarehe yangu ya kufanyiwa OP itakuwa 15.04.2014.
Nilipotimiza wiki ya 34 ya ujauzito wangu, niliamua kufunga safari na kwenda kwa mama yangu mzazi ili nipewe uangalizi wa karibu. Nilipofika kwa mama mzazi, baada ya siku mbili au tatu hivi nikwenda clinic (hospitali nyingine) pia Daktari wa pale naye alifanya calculations zake akitumia kadi ya clinic niliyokwenda nayo toka hospitali ya mwanzo. Huyu Daktari wa pili aliniambia kuwa nitafanyiwa OP tarehe 11.05.2014! Nilimwambia kuwa ni tarehe 15.04.2014, Daktari huyu alikataa na kuniambia kuwa yeye yuko sahihi na kwamba yule wa kwanza alikosea hesabu.

Tatizo langu: Binafsi hii variation ya siku takriban 27 kati ya hesabu za hawa madaktari wawili inanichanganya sana wakuu! Naogopa risk zitakazojitokeza endapo huyu Daktari wa pili atakuwa amekosea hesabu zake.

NINAOMBA USHAURI WENU WANA JF PAMOJA NA MADAKTARI WALIOPO HAPA JF.
 
g-g,

Fanya vyovyote wawasiliane, mweleweshe dr. 2 asijisikie humwamini na mmeo aongee na dr.1 huko nyumbani asione kapuuzwa

Ndio maana wakati mwingine hukaa 'jopo la ma dr.' kunapokuwa na complications,case mpya au mkanganyiko
 
g-g,

Fanya vyovyote wawasiliane, mweleweshe dr. 2 asijisikie humwamini na mmeo aongee na dr.1 huko nyumbani asione kapuuzwa

Ndio maana wakati mwingine hukaa 'jopo la ma dr.' kunapokuwa na complications,case mpya au mkanganyiko

Fuata huu ushauri utakusaidia kukuweka huru
 
Cjui uko mkoa gani lkn ungekua dar ungeenda kwa wataalamu na ungepata majibu kwa kuona na sio kuambiwa.mm tulipokua dar na mke wangu tulimtumia mtaalam mmoja anaitwa doctor mgaya ni muhimbili lakini ana hospitali yake kinondoni baada ya mataa ya njia panda ya kwenda coco beach tu kuna hyo hospital.ana vifaa vya uhakika kwani wife aliona mwenyewe kila kuchoendelea kwa kupitia mashine sio kazi ya kuguess. But kama upo mbali look for the third doctor uone inaweza kuwa the leading solution
 
Umahiri wa madaktari hutofautiana nakushauri urudi kwa daktari aliyekupangia mwanzo kujifungua watoto wa kwanza.
 
Umahiri wa madaktari hutofautiana nakushauri urudi kwa daktari aliyekupangia mwanzo kujifungua watoto wa kwanza.

Mkuu Shori habari?
Watoto wote watatu wamezaliwa sehemu tatu tofauti tofauti hivyo madaktari walionifanyia OP nao ni tofauti.
Pia yule Daktari wa kwanza alishatangulia mbele ya haki! (Alale panapostahili Dr. Makala!)
 
Last edited by a moderator:
Cjui uko mkoa gani lkn ungekua dar ungeenda kwa wataalamu na ungepata majibu kwa kuona na sio kuambiwa.mm tulipokua dar na mke wangu tulimtumia mtaalam mmoja anaitwa doctor mgaya ni muhimbili lakini ana hospitali yake kinondoni baada ya mataa ya njia panda ya kwenda coco beach tu kuna hyo hospital.ana vifaa vya uhakika kwani wife aliona mwenyewe kila kuchoendelea kwa kupitia mashine sio kazi ya kuguess. But kama upo mbali look for the third doctor uone inaweza kuwa the leading solution

Niko mbali na DSM, Asante kwa ushauri.
 
g-g,

Fanya vyovyote wawasiliane, mweleweshe dr. 2 asijisikie humwamini na mmeo aongee na dr.1 huko nyumbani asione kapuuzwa

Ndio maana wakati mwingine hukaa 'jopo la ma dr.' kunapokuwa na complications,case mpya au mkanganyiko

Thanks!
 
Hakika Huna tatizo lolote linaloitaji mchango. Fuata ushauri wa daktari anayetegemea kukuzalisha siku hiyo utakayopanga Kama ulivyozoea

Mkuu mimi siwezi kupanga siku, anayepanga ni Daktari!
Pia ninakumbuka mimba ya pili, makadirio ya Daktari hayakuwa mazuri sana maana nilikaa muda mrefu hospitali kwa maana mtoto alikuwa njiti sana hivyo alilazimika kuwekwa ktk Incubator.
 
Usijali sana kama hauna complications zozote. Kama uko wiki ya 34 inamaana ukiongeza hizo siku 27 means utajifungua katika wiki ya 38 au 37 na siku kadhaa, kama hesabu ingekua inaleta wiki 40 au zinazidi 40 ndio ingeleta wasiwasi
 
Lakini information anazotoa daktari si inategemea na mgonjwa umesema nini? Expectation date haitegemei na 'siku' za mwisho zilipoonekana? Si ndio hapa inapokuja zile plus or minus za makosa kwenye kuhesabu? Sasa hii ya kupishana kwa karibu mwezi mzima mbona kama ina utata? Kwa mpishano huu nafikiri kuna umuhimu wa kumuona daktari mwingine, ila isingekuwa 'planned' CS, ungesubiri mpaka mwisho ndio uende wakakufanyie hiyo operation...
 
Lakini information anazotoa
daktari si inategemea na mgonjwa umesema nini? Expectation date
haitegemei na 'siku' za mwisho zilipoonekana? Si ndio hapa inapokuja
zile plus or minus za makosa kwenye kuhesabu? Sasa hii ya kupishana kwa
karibu mwezi mzima mbona kama ina utata? Kwa mpishano huu nafikiri kuna
umuhimu wa kumuona daktari mwingine, ila isingekuwa 'planned' CS,
ungesubiri mpaka mwisho ndio uende wakakufanyie hiyo
operation...

Mara ya mwisho, niliingia ktk period 8 july, 2013, mwezi uliofuata sikuona siku zangu.
 
Mara ya mwisho, niliingia ktk period 8 july, 2013, mwezi uliofuata sikuona siku zangu.

Kama tarehe 8 ndio ilikuwa siku ya kwanza, kwa kalenda ya google inasema due date ni 14th April 2014. Ila muone daktari kwa ushauru zaidi, sie madaktari kanjanja tusije tukakuingiza chaka. Na ndio maana nikasema, isingekuwa issue ya planned tarehe, ungesubiri mpaka uone dalili za mauza uza ndio ujisogeze...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom