Mkuu ni kweli kabisa Viwanda bila kilimo haiwezekani ila awamu hii wameshupalia viwanda bila
Kujali vitazalisha nini.
Wakulima wanasahaulika kuanzia pembejeo, masoko ya mazao hadi utatuzi wa migogoro yao ya ardhi.
Mfano yale maharage kule kigoma na kagera mwaka huu wakulima wamekosa pa kuuza au la wameuza kwa bei za hasara kabisa . Choroko kule shinyanga ( recently nilikuwa sangamwalugesha nimejionea kwa macho) choroko za kutosha watu wamevuna ila kwa kuwa mnunuzi ni mmoja na msimu huu amesusa kununua kwa hiyo wakulima wamebaki wamekumbatia choroko zao.
Kilimo kinatelekezwa na wakulima wanapelekewa frustrations hadi mashambani kila kukicha badala ya kuwapelekea mahitaji yao muhimu kwa wakati . Ndio maana nikasema kilimo kinapotezwa ili viwanda visikike zaidi.
Akili ndogo za waimbaji wa sera ya viwanda ndio inaua kilimo Tanzania.