Mung Chris
JF-Expert Member
- Sep 12, 2017
- 3,439
- 3,951
Serikali ingilieni kati, Mbolea imekuwa na masharti magumu kununua, sasa hivi hakuna kupima kwa kilo, kila mkulima analazimika kununua mfuko wa Kilo 50 ambao bei yake ni sh 50,000-55,000 wengine hawana mashamba makubwa ya kutumia mfuko wa 50kg ukizingatia mifuko ya 25kg haipatikani kwa urahisi, viwatilifu vya kuulia wadudu (dawa) zimekuja kwa bei ya ghali sana wengine kama Manyara wamepiga dawa zaidi ya mara 3 wadudu hawafi tuna wasiwasi na hizi dawa, , dawa zilizotoka mwaka jana tumezitafuta hazipo madukani kwanini? kwa mwaka jana shamba langu nilipiga dawa mara moja tu wadudu wakafa kwa sasa nimenunua dawa moja wapo nimepiga wadudu hawafi nimerudi dukani nikaambiwa nipige dawa mara 3 nikawauliza kama wanajua kazi ilivyo ngumu kubeba mtungi wa dawa mgongoni isitoshe unamlipa mtu wa kupiga dawa unamipa mara ngapi kwa kila tripu.
Basi naomba serikali waliangalie swala hili popote pale ambapo dawa zina feli hii haipo kwenye historia ya miaka ya hivi karibuni kuwa ukipiga dawa wadudu hawafi, gharama kwa wakulima wadogo ni kubwa sana hata mbegu zenyewe bei ni ile ile pamoja na serikali kutangaza kuwa wametoa tozo kwenye mbegu za kilimo.
Itakuwa vyema kama dawa hizi za kuulia wadudu wa mashambani ziwe kwa bei rahisi, mbolea ishuke bei na mbegu ishuke bei ili WENGINE TUSIMAME NA KILIMO. maana kama viuatilifu (dawa) zitakuwa ghali, mbolea masharti magumu kupata na mbegu bei ghali tu hii kilimo tunayosema itatufikisha wapi mwisho wa siku tutaacha kulima na tutafute maisha mengine.
Baada ya kuyasikia haya nimeomba off mapumziko ya wiki 2 ili nikabiliane na hawa wadudu maana mashamba yamevamiwa.
Basi naomba serikali waliangalie swala hili popote pale ambapo dawa zina feli hii haipo kwenye historia ya miaka ya hivi karibuni kuwa ukipiga dawa wadudu hawafi, gharama kwa wakulima wadogo ni kubwa sana hata mbegu zenyewe bei ni ile ile pamoja na serikali kutangaza kuwa wametoa tozo kwenye mbegu za kilimo.
Itakuwa vyema kama dawa hizi za kuulia wadudu wa mashambani ziwe kwa bei rahisi, mbolea ishuke bei na mbegu ishuke bei ili WENGINE TUSIMAME NA KILIMO. maana kama viuatilifu (dawa) zitakuwa ghali, mbolea masharti magumu kupata na mbegu bei ghali tu hii kilimo tunayosema itatufikisha wapi mwisho wa siku tutaacha kulima na tutafute maisha mengine.
Baada ya kuyasikia haya nimeomba off mapumziko ya wiki 2 ili nikabiliane na hawa wadudu maana mashamba yamevamiwa.