Jamani wana JF nisaidieni ushauri.
Sisi tulizaliwa 7, wavulana 3, na wanawake 4.
Bahati mbaya wazazi wetu wote walishatangulia mbele ya haki.
wavulana wote wameoa na wasichana wameolewa.
Kwa upande wetu sisi 7 tunapendana. Kwa wasichana huwa tunatembeleana, tunasaidiana, kwa kifupi tuko karibu sana. Tatizo kwa hawa wifi zetu. Yaani kitu cha ajabu hawapendani wao kwa wao utafikiri wake wenza jinsi wanavyochukiana. Pia wanatuchukia sana sisi wifi zao. Ajabu hata watoto wao hawaruhusiwi kwenda kwa baba mkubwa au mdogo, kwa shangazi ndio kabisa sikumbuki kuwa walikuja lini kwangu.
Tofauti na mimi nilikoolewa, huwezi tofautisha kati ya sisi tuliolewa na wifi zetu, tunapendana tunashirikiana na hata watoto wetu wanapendana sana, wakiwa likizo wanatembeleana, yaani wamekuwa zaidi ya ndugu, wamekuwa marafiki kwani kila mara kwa mara wanapokuwa likizo wanakuwa pamoja wakati wanaishi mikoa tofauti.
Natamani wake za kaka zangu hata wapendane tu wao kwa wao, acha wasitupende sisi mawifi lakini wao wapendane na washirikiane ili wawainue waume zao. Kwani kutokana na tabia ya kuchukiana naona hata Mungu anafunga mibarakwa kwa kaka zangu kwani mambo yao hayaendi vizuri kabisa.
Sisi tulizaliwa 7, wavulana 3, na wanawake 4.
Bahati mbaya wazazi wetu wote walishatangulia mbele ya haki.
wavulana wote wameoa na wasichana wameolewa.
Kwa upande wetu sisi 7 tunapendana. Kwa wasichana huwa tunatembeleana, tunasaidiana, kwa kifupi tuko karibu sana. Tatizo kwa hawa wifi zetu. Yaani kitu cha ajabu hawapendani wao kwa wao utafikiri wake wenza jinsi wanavyochukiana. Pia wanatuchukia sana sisi wifi zao. Ajabu hata watoto wao hawaruhusiwi kwenda kwa baba mkubwa au mdogo, kwa shangazi ndio kabisa sikumbuki kuwa walikuja lini kwangu.
Tofauti na mimi nilikoolewa, huwezi tofautisha kati ya sisi tuliolewa na wifi zetu, tunapendana tunashirikiana na hata watoto wetu wanapendana sana, wakiwa likizo wanatembeleana, yaani wamekuwa zaidi ya ndugu, wamekuwa marafiki kwani kila mara kwa mara wanapokuwa likizo wanakuwa pamoja wakati wanaishi mikoa tofauti.
Natamani wake za kaka zangu hata wapendane tu wao kwa wao, acha wasitupende sisi mawifi lakini wao wapendane na washirikiane ili wawainue waume zao. Kwani kutokana na tabia ya kuchukiana naona hata Mungu anafunga mibarakwa kwa kaka zangu kwani mambo yao hayaendi vizuri kabisa.