ni muda wa mashoga nao kushiriki na kudai haki yao iwe ya kikatiba. Kazi ndo imeanza.
Wapo majaji ambao wamesomea contitunal law. Hao mara nyingi wanatumiwa na nchi za nje ili waanda mabadiliko ya katiba. Na wanajulikana sababu hawana upande watakao chukuwa na wanajali uzalendo Awachukuwe hao.
Kutaka wananchi au taasisi kupendekeza ni delay tactics tu.
Tutakuja kufanya kosa kubwa kwa kudhani Kamati hii itaindwa na watu wa Dar es Salaam tu! na wasomi tu ama watu tunaowaona kwenye runinga. Hii Tume itakuwa inakusanya maoni toka kwa Watanzania wote hivyo ni muhomu ikawa na mchanganyiko maalum. Mimi napendekeza mkulima mmoja toka kijiji cha Kemondo anaitwa Mzee Kateme. Napendekeza mfugaji mmoja toka kijiji cha Mbuyuni huko Chunya anaitwa Masanja Mazuri. Mwisho nampendekeza mlima bangi mmoja toka kijiji cha Kemakorere anaitwa Mwita Gekerero Marwa.
Walioko magerezani wanaotumikia vifungo vya maisha au vifo,jeetu patel,babu wa loliondo nao wawemo
Hapo kwenye Red nafikiri unawaza ufadhili wa magari...kwa CCM
TISS mumeshaanza!
Prof.Chris Miana, Bashirryy nawaunga mkono
Naona kama huu utakuwa Muhadhara badala ya Tume ya Maoni!Jenerali Ulimwengu..
Mussa Kundecha (shiekh)
Prof. Ibrahim Lipumba
Kardinali Pengo
Wanabodi kama tujuavyo Raisi Jakaya Kikwete amealika taasisi mbalimbali na wadau wampelekea mapendekezo ya majina ya watu ambao atafikiria miongoni mwao awateuwe wawe wajumbe wa Tume ya kukusanya maoni na kuandika rasimu ya katiba mpya! Nadhani haitakuwa vibaya kama tukijadili na kupendekeza nani anatufaa katika tume hii sauti zetu zina maana sana hata kama hatutapeleka rasmi lakini wengi wanatapita na kusoma humu hviyo naamini watatusikia tu.
Tume inahitaji watu MAKINI, WASIKIVU na WANAOJALI MASLAHI ya TAIFA. Kwa kuanza napendekeza wafuatao ambao sio wabunge na nadhani kati yao wangefikiriwa watatusaidia katika kuyajari maslahi mapana ya taifa letu :
Wengine wengi tubaki au wabaki katika kundi la watoa maoni, wahamasishaji wa watu kwenda kutoa maoni mbele ya tume, waelimishaji(elimu ya uraia hasa juu ya katiba) na wachambuzi kwa Mfano kama wakina Dr.Lwaitama, Prof Issa Shivji, Generali Ulimwengu, Mwanakijiji, Makwaia wa Kuhenga, Prof Kabudi, Heleni Kijo-Besimba, Dr. Kitila Mkumbo, Privatus Karugendo,Deus Kibamba n.k ningependa waachwe ili waje kutusaidia katika uchambuzi na ukosoaji wa rasimu itakapo kuwa tayari ili kuleta mawazo mapana zaidi.
- Wanahabari: Ayubu Ryoba, Hamisi Dambaya, Rosemary Mwakitwange na Joseph Mihangwa
- Wanataaluma: Prof. Chris Peter Maina, Mugongo Fimbo, Dr. Masumbuko Lamwai, Dr. Frola Kessy, Dr. Vicensia Shule, Dr.Honest Prosper Ngowi na Bashiru Ally
- Asasi za Kiraia: Jefred Myenzi, Usu Mallya, Ananelia NKya…
- Kutoka JF: Pasco wa JF ... Vyama vya Siasa: Prof.Mwasiga Baregu, Dr. Sekondo Mvungi na Prince Bagenda…
- Wanamichezo: Filbert Bayi…
- Wanasanii: Chemudu Ngwao, Irine Sanga na John Kitime…
- Viongozi wa Dini: Sheikh Mkuu wa Dar es Salaama-alhad Mussa Salum, Pd.Stevene Kaombwe
- Walemavu(physical challenged):...
- Wafanyabiashara:...
- Wanafunzi:...
- Wafanyakazi:..
- ...
Katiba ni jukumu letu sote tujenga misingi ya sasa na ya baadaye!tuna nafasi ya pekee sana ambayo HISTORIA haitacha kutusahau na kutuhukumu.
Je wewe mdau ungependa nani awemo katika kamati ya katiba?