Wild Flower
JF-Expert Member
- Jul 20, 2023
- 844
- 1,608
Wajumbe wa Kata ya Tabata Jimbo la Segerea, jijini Dar es Salaam wametakiwa kutoka ndani ya ukumbi mara baada ya kupiga kura.
Hata hivyo, tangazo la kuwataka watoke ndani kwenda nje limeibua malalamiko leo Jumatatu, Agosti 4, 2025 katika ukumbi wa Green Light kutoka kwa wajumbe.
Hatua hiyo imefuatia baada ya matangazo kutoka kwa mmoja wa wasimamizi wa mchakato huo (hakutaka kutaja jina) alipowatangazia wajumbe wanapaswa kutoka nje mara baada ya kupiga kura.
"Ndugu wajumbe tunaanza rasmi zoezi letu la upigaji kura, na kwa sasa hatutoruhusu mtu yeyote kuingia ndani. "Wajumbe baada ya kupiga kura utaratibu mtatoka nje, nje ya geti kabisa na ndani tutaendelea na utaratibu mwingine," amesikika akitangaza.
Hata hivyo, kauli hiyo ilizua malalamiko kutoka kwa wajumbe ambao walikiwemo katika ukumbi huo wakipinga utaratibu Mtoa matangazo huyo alisikika akisisitiza:"Utaratibu utakaotumika ni kama nilivyotangaza na kama mna wasiwasi mawakala wako hapa."
Hatua hiyo imefuatia baada ya matangazo kutoka kwa mmoja wa wasimamizi wa mchakato huo (hakutaka kutaja jina) alipowatangazia wajumbe wanapaswa kutoka nje mara baada ya kupiga kura.
"Ndugu wajumbe tunaanza rasmi zoezi letu la upigaji kura, na kwa sasa hatutoruhusu mtu yeyote kuingia ndani. "Wajumbe baada ya kupiga kura utaratibu mtatoka nje, nje ya geti kabisa na ndani tutaendelea na utaratibu mwingine," amesikika akitangaza.
Hata hivyo, kauli hiyo ilizua malalamiko kutoka kwa wajumbe ambao walikiwemo katika ukumbi huo wakipinga utaratibu Mtoa matangazo huyo alisikika akisisitiza:"Utaratibu utakaotumika ni kama nilivyotangaza na kama mna wasiwasi mawakala wako hapa."