Wajue Kingpin ( Vinara) wa CCM Kikanda

Wajue Kingpin ( Vinara) wa CCM Kikanda

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
104,319
Reaction score
183,528
Victoria - Mh Biteko

Nyanda za Juu - Dr Tulia

Kusini - Mh Salma

Kaskazini - Mh Makonda

Mashariki- Mh Ridhiwan

Kati - Mh Bashe

Magharibi - Mh Kafulila

Ahsanteni sana

Nawatakia Dominica njema 🙏
 
Joni acha zako, Kafulila hajulikani CCM kabisa, wala hajawahi kuwa CCM, so acha kumweka katika list..!!

Kafulila hajawahi kuwa CCM, au Joni unaanza kupata mental disorders..!!
Una hakika Kafulila hajawahi kutia Nia ya Ubunge kupitia CCM? 😂😂
 
Hakuna Kingpins wa Siasa za kikanda Tanzania, TZ especially CCM ,Kingpins uwa ni kamati kuu ya Chama, kama hawakutaki ata ufanyeje , huwezi toboa..Marehemu Sitta , Ndugai, Mpina na Makamba wanajua Hilo...Kanda ya Ziwa wangekua na KINGPIN kuna foul nyingi zinazofanyika zisingevumiliwa..kila mtu anapambana kivyake.. Tofauti na Kenya ambapo siasa ziko Regional sana na ukabila unatumika, TZ ni tofauti, wanasiasa wengi wanaufyata Mbele ya kamati kuu ya Chama.
 
Mara ya mwisho kwenda shule ya msingi na kuhitimu darasa la tatu chee nilijua kwamba Tabora lilipo Jimbo la uchaguzi kwa Bashe na Kigoma ni Kanda ya magharibi.
Siasa haiko hivyo ndio sababu Makonda kwake ni Misungwi na Kigamboni lakini…… 😂😂
 
Una hakika Kafulila hajawahi kutia Nia ya Ubunge kupitia CCM? 😂😂
Yaani Kafulila kutia nia ya Ubunge CCM ndio kumuweka katika list ya Kingpin? Au hujui maana ya Kingpin? Joni vipi lkn? Hivi hujui watia nia Ubunge CCM wako hadi machwa tu kama Mwijaku, Baba Levo, Shilole, Darasa la 7 failure, wenye feki PhD kama Musukuma na wengine wengi hata hawajulikani, sasa kutia nia ndio awe kinara wa CCM kweli? Hivi Joni kwanini unashusha hadhi ya Chama chetu CCM hivi?

Kafulila awe kinara wa CCM kweli? Please wahi Mirembe una tatizo kubwa Joni, sasa naanza kuamini wenye majina ya Joni wana tatizo katika Medula zao..!! Edit hapo kwenye post yako utoe aibu hiyo
 
Yaani Kafulila kutia nia ya Ubunge CCM ndio kumuweka katika list ya Kingpin? Au hujui maana ya Kingpin? Joni vipi lkn? Hivi hujui watia nia Ubunge CCM wako hadi machwa tu kama Mwijaku, Baba Levo, Shilole, Darasa la 7 failure, wenye feki PhD kama Musukuma na wengine wengi hata hawajulikani, sasa kutia nia ndio awe kinara wa CCM kweli? Hivi Joni kwanini unashusha hadhi ya Chama chetu CCM hivi?

Kafulila awe kinara wa CCM kweli? Please wahi Mirembe una tatizo kubwa Joni, sasa naanza kuamini wenye majina ya Joni wana tatizo katika Medula zao..!! Edit hapo kwenye post yako utoe aibu hiyo
Endelea na Ligi 😄🙏
 
Kwenye haya maisha ukiamini kuwa binadamu wana nguvu na ni bora kuliko wengine then wewe kwa kuanzia ni tatizo kwenye jamii.

Hao wote umewataja wanaendeshwa na kiburi kinachotokana na uzembe wa wanainchi kuto wawajibisha kwa mujibu wa sheria za inchi na vyama vyao.

Unapoandika kitu kwenye hadhira kama hivi ni vema ukasema na wewe interest zako zimelalia wapi. Kwasababu kuandika hivi bila kuweka bayana maudhui ya andiko lako au declaration ya interests zipo upande upi unatulazimisha kuamini kuwa wewe ni muhuni na unasherekea kuwaona wahuni wakishika hatamu na kukamata mamlaka kama vile wamekamatia biashara za urithi za familia na koo za baba zao.

Ni muda sasa tuwe wazalendo hata kwa kauli zetu tu. Hiki ulichofanya hapa ni automatically glorification na idolization ya binadamu wenzako ambao hawana cha maana cha kuofa katika jamii zaidi ya uharibifu. Je unataka tuungane na wewe kuwasheherekea na kuwapa mapambo?

Kama sivyo then nambie kwanini uandike andiko la kinafiki hivi ukijua wazi hawa watu si watu wazalendo na umewa benchmark kama vinara wa kisiasa na washika mfumo?

Am sorry kama nimekukwaza ila sipendi hii tabia ya kuwapandisha na kuwapa sifa watu wa hovyo.
 
Victoria - Mh Biteko

Nyanda za Juu - Dr Tulia

Kusini - Mh Salma

Kaskazini - Mh Makonda

Mashariki- Mh Ridhiwan

Kati - Mh Bashe

Magharibi - Mh Kafulila

Ahsanteni sana

Nawatakia Dominica njema 🙏
Mbona wepesi hivyo?
 
Back
Top Bottom