Wahitimu Rwanda wabuni njia mpya ya kutatua tatizo la ajira

MMOJA

JF-Expert Member
Aug 30, 2012
445
259
Leo napenda ku share hii na wana jamvi wenzangu kuhusu tatizo la kukosa ajira,
Wahitimu wenzetu wa nchi ya Rwanda baada ya kuona ukubwa wa tatizo la ajira,
Wao wenyewe hivi sasa wakimaliza chuo tu, badala ya kuanza kupambana na kutafuta ajira kisha kukutana na bango kubwa HAKUNA KAZI, Sasa baada ya kuhitimu shahada ya kwanza wanaenda vyuo vya ufundi stadi kujifunza fani mbalimbali kama upishi,kuchomelea,useremala, mitindo(design),umakenika,Kilimo,Ufugaji, ujenzi na mengineyo, Lengo ni kwamba ukiwa na ujuzi wa moja kwa moja angalau utaweza kujiajiri pasipo kutegemea mtaji kwa kiasi kikubwa na ujuzi wako kuwa mtaji wako na hivyo kuweza kusonga mbele pasipo kusubiria ajira za maofisini

KWETU SISI WAHITIMU WA KITANZANIA. Ni vema na sisi tukaiga mfano huo wa majirani zetu, kwani sasa hali katika soko la ajira sio nzuri na miaka inavyozidi kwenda ndio hali inazidi kua taabani na hakuna matumaini hata kidogo kutokana na wahitimu ni wengi katika soko kuliko nafasi mpya za ajira zinazozalishwa kila mwaka.

Kuliko kuendelea kulalamika siku hadi siku ni vema tukachukua hatua ya kutatua tatizo hili kwa namna nyingine.

TAFAKARI,CHUKUA HATUA

Ahsante
 
inamana wakishaenda kwenye vyuo vya ufundi stadi ndo tayari wameashatatua tatzo la ajra ?
 
  • Thanks
Reactions: WAR
Imekaa vizuri
Leo napenda ku share hii na wana jamvi wenzangu kuhusu tatizo la kukosa ajira,
Wahitimu wenzetu wa nchi ya Rwanda baada ya kuona ukubwa wa tatizo la ajira,
Wao wenyewe hivi sasa wakimaliza chuo tu, badala ya kuanza kupambana na kutafuta ajira kisha kukutana na bango kubwa HAKUNA KAZI, Sasa baada ya kuhitimu shahada ya kwanza wanaenda vyuo vya ufundi stadi kujifunza fani mbalimbali kama upishi,kuchomelea,useremala, mitindo(design),umakenika,Kilimo,Ufugaji, ujenzi na mengineyo, Lengo ni kwamba ukiwa na ujuzi wa moja kwa moja angalau utaweza kujiajiri pasipo kutegemea mtaji kwa kiasi kikubwa na ujuzi wako kuwa mtaji wako na hivyo kuweza kusonga mbele pasipo kusubiria ajira za maofisini

KWETU SISI WAHITIMU WA KITANZANIA. Ni vema na sisi tukaiga mfano huo wa majirani zetu, kwani sasa hali katika soko la ajira sio nzuri na miaka inavyozidi kwenda ndio hali inazidi kua taabani na hakuna matumaini hata kidogo kutokana na wahitimu ni wengi katika soko kuliko nafasi mpya za ajira zinazozalishwa kila mwaka.

Kuliko kuendelea kulalamika siku hadi siku ni vema tukachukua hatua ya kutatua tatizo hili kwa namna nyingine.

TAFAKARI,CHUKUA HATUA

Ahsante
sasa kuna faida gani kwenda chuo wakati unaona wenzako walomaliza miaka mpaka mitano nyuma hawana ajira? Ni upumbavu kwenda chuo kikuu kisha ukakosa ajira ukaamua wenda kusomea ufundi, kwanini hukwenda direct kusomea ufundi badala ya kupoteza miaka mitatu au mitano chuo kikuu kisha unaenda kuwa fundi mbao, au umesoma chuo kikuu na una digrii ya public relation kisha unakwenda shamba kulima matikiti, kwanini hukwenda sua kusomea kilimo kabisa badala ya hiyo PR? Wasomi wengi wanasoma kama fasion tu, eti mimi nachukua Masters kisha unamkuta anauza mama ntilie kisa heti ajira hakuna, si nafuu angesomea mapishi?
 
Kuna mtoto wa dada yangu niliwashauri wampeleke VETA eti wao wakampeleka mipango Dodoma, ngoja amalize aje apambane na tatizo la ajira. Mimi nilishaawambia, akisoma VETA hawezi kufa njaa. Wao wanajali sifa kuwa sijui kasome kozi ya kuvaa suti na tai. Anyaway, kila mtu na bahati yake bhana.
huyo dogo ana akili saana , tatizo wazazi wengi wana akili mgando na kukariri maisha, binafsi nimependa story ya coulibaly wa Senegal amefight mpaka amefika Italy acheze mpira hili apate pesa nyingi wazazi wake wanamlazimisha abaki Senegal asome then aajiriwe cha kuujiuliza akiajiriwa atalipwa shs ngapi ?, mimi naonaga maamuzi mengi kuhusu maisha ya wasomi wenye makaratasi au vyeti ni hovyo na yamejaa oga tu
 
sasa kuna faida gani kwenda chuo wakati unaona wenzako walomaliza miaka mpaka mitano nyuma hawana ajira? Ni upumbavu kwenda chuo kikuu kisha ukakosa ajira ukaamua wenda kusomea ufundi, kwanini hukwenda direct kusomea ufundi badala ya kupoteza miaka mitatu au mitano chuo kikuu kisha unaenda kuwa fundi mbao, au umesoma chuo kikuu na una digrii ya public relation kisha unakwenda shamba kulima matikiti, kwanini hukwenda sua kusomea kilimo kabisa badala ya hiyo PR? Wasomi wengi wanasoma kama fasion tu, eti mimi nachukua Masters kisha unamkuta anauza mama ntilie kisa heti ajira hakuna, si nafuu angesomea mapishi?
fantastic mkuu
 
NIMEKUWA NIKIWAZA KUFANYA HIVYO KWA KITAMBO KIREFU SANA LAKINI NANI WA KUNILIPIA ADA,OK HATA NIKIPATA WA KUNILIPIA ADA KUSOMA SOMA KILA WAKATI BILA YA KUWA NA PESA MFUKONI WALA MAENDELEO KATIKA MAISHA UKIZINGATIA UMRI UNAENDA DAHHHH!!!!!!! NI MSALA KWAKWELI.


KUNA BROO MMOJA YEYE AMEMALIZA SHAHADA YA KWANZA PALE IFM,ALIVYOONA MIYEYUSHO ALIENDA KUSOMA MAPISHI SASA HIVI AMEJIAJIRI MSAIDIZI MKE WAKE WANAMGAHAWA WANAPIGA SANA PESA AISEEE.
 
Hiyo ndio mbinu mliobakiza kumaliza tatizo la ajira TZ nchi hii??? basi sawa! Nadhani mnadhihirisha mlivyochoka....
 
Story za vijiweni hizi.

Haina haja ya kuzunguka safari ndefu hadi upate degree halafu urudi kusomea ufundi seremala wakati ungesomea ulipomaliza darasa la saba tu.
 
Tatizo lilopo ni kwamba wahitimu wa hapa tanzania wanaidharau elimu ya veta.
Ukiwaambia waende kusoma vyeta wanaona unawashusha...

Mafunzo ya veta kwa sasa ndio habar ya mjini
 
Ukizungumzia suala La Kujiajiri ni Kama umechokoza Nyuki kwenye Mzinga Jiandae kwa Matusi yao Poor Tz Graduates!
 
Yanini usubiri mpaka umalize chuo then ili kwenda kwenye ufundi stadi, unaweza fanya hilo hata baada ya form 4!!!
Exactly kabisa mkuu. Hapo hakuna solution ya tatizo la Ajira. Kama hiyo ni solution basi ilibidi wai-apply kuanzia mwanzo kabisa.
Labda nikuulize swali mtoa mada, Je wakishamaliza chuo tu wanaunga Chuo cha ufundi stadi? Au wataanza kutafuta ajira akikosa ndio aende ufundi stadi? Na kama mpaka akose, je Inachukua muda gani mpaka huyo muhusika aamue kwenda chuo cha ufundi stadi (Mfano; Labda ataomba kazi 4 sipoitwa kwenye interview, au akiitwa akakosa ndio ataaamua?) Yaan kwa kifupi nataka kujua kitu gani kitam-trigger ili afanye maamuzi ya kwenda ufundi stadi?
Nisaidie kwa hilo ili tufikirishane kidogo.
 
Kuna mtoto wa dada yangu niliwashauri wampeleke VETA eti wao wakampeleka mipango Dodoma, ngoja amalize aje apambane na tatizo la ajira. Mimi nilishaawambia, akisoma VETA hawezi kufa njaa. Wao wanajali sifa kuwa sijui kasome kozi ya kuvaa suti na tai. Anyaway, kila mtu na bahati yake bhana.
Hapa ndipo watu wanazingua, Ungekaa na mdogo wako huyo, umueleze faida chanya za ushauri wako, pia umueleze hasara za ushauri ambao yeye anataka kuuchukua, then compile naye hapo, ili afanye choice, wewe unawashauri wazazi kwan wazazi ndio wanao soma? Ni vizuri unapomueleza mtu suala la choice ukawa vizuri kwenye hilo eneo, uwe na mifano halisi yenye faida na hasara, sasa wabongo wakiweka vitu wanaweka faida tupu tuu, hakuna ushauri wa namna hiyo.
 
Wote mnataka tuwe mafundi?? Watu wote wakiishia veta nchi itapata wapi wahasibu?? Maafisa rasilimali watu??waalimu n.k.....hizi ni harakati za waliokosa mwanya wa kupata degree kujifariji.tulio na degree tunawaumiza sana akili ambao hawana japo kazi hatuna...videmu vyenu tunavila tu baada ya kuvionyesha picha za majoho
 
Back
Top Bottom