'Khalid na Philemon walipendana' - Saida Karoli alimaanisha nini hapa?

Farolito

JF-Expert Member
Sep 10, 2018
11,634
26,376
Wakuu habari zenu,
Katika wimbo wa Saida Karoli unaoitwa Maria Salome' kuna mashairi yanasema
'Khalidi na Filimoni walipendana, mapenzi yao yakadumu,
Wenye wivu wajinyonge sana, wenye wivu wajinyonge'

Sasa Khalidi na Filimoni walipendana mapenzi ya namna gani hayo yakadumu?
Hao wote si ni wanaume au kuna mmoja ni mwanamke hapo maana nimejaribu kutafuta mashairi sikupata.

Labda wenzetu mtusaide kwakuwa mnaelewa maneno mwanzo mwisho inawezekana stori mmeielewa au pengine katika tamaduni zenu kuna majina ya kike yanafanana na hayo?

Karibuni mtujuze


 
Wakuu habari zenu,
Katika wimbo wa Saida Karoli unaoitwa Maria Salome' kuna mashairi yanasema
'Khalidi na Filimoni walipendana,mapenzi yao yakadumu,
Wenye wivu wajinyonge sana,wenye wivu wajinyonge'

Sasa Khalidi na Filimoni walipendana mapenzi ya namna gani hayo yakadumu?
Hao wote si ni wanaume au kuna mmoja ni mwanamke hapo maana nimejaribu kutafuta mashairi sikupata.

Labda wenzetu mtusaide kwakua mnaelewa maneno mwanzo mwisho inawezekana stori mmeielewa au pengine katika tamaduni zenu kuna majina ya kike yanafanana na hayo?

Karibuni mtujuze


Wahaya wanahusika vipi hapo wakati lugha iliyotumika kwenye msingi wa swali lako ni kiswahili?
 
Wakuu habari zenu,
Katika wimbo wa Saida Karoli unaoitwa Maria Salome' kuna mashairi yanasema
'Khalidi na Filimoni walipendana,mapenzi yao yakadumu,
Wenye wivu wajinyonge sana,wenye wivu wajinyonge'

Sasa Khalidi na Filimoni walipendana mapenzi ya namna gani hayo yakadumu?
Hao wote si ni wanaume au kuna mmoja ni mwanamke hapo maana nimejaribu kutafuta mashairi sikupata.

Labda wenzetu mtusaide kwakua mnaelewa maneno mwanzo mwisho inawezekana stori mmeielewa au pengine katika tamaduni zenu kuna majina ya kike yanafanana na hayo?

Karibuni mtujuze





Philomena.
 
Urafiki wa kuchanjana damu unaobadilika kuwa undugu ndiyo anaoongelea. Mhaya akifanya urafiki unageuka undugu.
Kwahio kwa wahaya huu utaratibu ni kawaida mwanamke na mwanaume kuchanjana damu au mwanaume na mwanaume?
 
Kwahio kwa wahaya huu utaratibu ni kawaida mwnamke na mwanaume kuchanjana damu au mwanaume na mwanaume?
Mimi ninavyoelewa ni jinsia moja. Siwezi semea kila mtu maana mimi babu yangu alichanja damu na watu wa jinsia zake ambao sasa ndugu zao ni ndugu zetu ambao tunawaheshimu zaidi kuliko wetu sababu mkifarakana wanasema kuna laana. I cant prove it. Sijawahi sikia wanawake wanachanja damu na sijui kwanini. Labda kuna watu humu JF wanajua zaidi.
 
Asante mkuu kwa maoni yako, nimekupata vizuri
Mimi ninavyoelewa ni jinsia moja. Siwezi semea kila mtu maana mimi babu yangu alichanja damu na watu wa jinsia zake ambao sasa ndugu zao ni ndugu zetu ambao tunawaheshimu zaidi kuliko wetu sababu mkifarakana wanasema kuna laana. I cant prove it. Sijawahi sikia wanawake wanachanja damu na sijui kwanini. Labda kuna watu humu JF wanajua zaidi.
 
Back
Top Bottom