Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,064
- 22,757
Kwa wagombea Ubunge kupitia CCM;
Na kwa wapiga kura wote;
Siku ya kupiga kura tujitokeze kwa wingi tulikomboe taifa letu kutoka mikononi mwa mafisadi kwa kumpigia kura Dr. W. P. Slaa. Nafasi kama hii hupatikana mara moja katika miaka mitano.
- Kama kweli unakerwa na usanii wa serikali ya CCM chini ya Raisi Kikwete.
- Kama kweli unachukia vitendo vya rushwa ndani ya serikali ya CCM.
- Kama kweli unakerwa na uhuni wa viongozi wa CCM na serikali yake.
- Kama umechoka na utawala mbovu usiojali haki wala kufuata sheria.
- Kama unakerwa na EPA, Kagoda, Dowans, Richmond, Radar, Kiwira n.k.
Na kwa wapiga kura wote;
- Kama unalipenda Taifa lako na ungependa kuliona linaendelea
- Kama ungependa kuona mabadiliko ya msingi pamoja na katiba.
- Kama unataka kuona heshima ya Tanzania kama taifa inarudi.
- Kama ungependa kuongozwa na serikali inayowajali wananchi wake.
- Kama ungependa kuona sheria ikichukua mkondo wake dhidi ya dhulma.
Siku ya kupiga kura tujitokeze kwa wingi tulikomboe taifa letu kutoka mikononi mwa mafisadi kwa kumpigia kura Dr. W. P. Slaa. Nafasi kama hii hupatikana mara moja katika miaka mitano.