Wagner wapo wa kutosha hapo Central African Republic ila sijajua kama wapo DRC. Hata hivyo sipingi maana wao kwa Afrika hupenda nchi zenye madini na vita
Wagner wapo wa kutosha hapo Central African Republic ila sijajua kama wapo DRC. Hata hivyo sipingi maana wao kwa Afrika hupenda nchi zenye madini na vita
M23 inabidi wapige mpaka Kinshasa na kumuondoa Tshesekedi, Tshesekedi badala ya kuleta amani kwa wananchi wake wote ameamua kuwa muuaji wa wanyamulenge, acha M23 wapigane maana huwezi kukaa nyumbani ukisubiri genocides' waje wakumalize
Wagner wanachoangalia ni pesa au rasilimali. Alafu kumbuka hao ni private military contractor (PMC) kama kina Blackwater ya Erik Prince. Serikali yeyote duniani inaweza fika makubaliano nao kama cause inaendana na sera za Russia, au serikali ya Kremlin yenyewe inaweza watuma popote ambapo haitaki nzi wengi kuisumbua kwanini Russia imeleta wanajeshi wake.
Ni kawaida sana ya mamluki kupigana na adui leo, baada ya miezi sita akaungana na adui kupigana na adui mwingine. Au kupigana na adui ZTY nchi fulani ila wakati huohuo memebers wa PMC hiyohiyo nchi nyingine wanaungana na ZTY kupigania kitu fulani.
Ila CAR wana jeshi la kipuuzi sijawahi ona. Kukutana mwanajeshi kavaa ndala akiwa na gun ni kawaida sana, hata sare wanaungaunga. Kumlinda Rais hawawezi, mwenyewe ana wasiwasi nao ndio akawaleta Wagner.
Wagner hawako uniform, huku wanaweza kuwa the best fighters with good gears na kule wakawa vilaza. Hawa wanaosema Wagner huvaa vizuri (wanawaona Ukraine) wamesahau fact kwamba zile silaha wanapewa na MoD ya Urusi.
Uwezekano wa wao kuwa DRC siukatai. In fact nilishawaza kuna siku tutawaona hapo, DRC ina kila kitu wanachokitafuta kuliko nchi yoyote Afrika