Kambi ya Fisi
JF-Expert Member
- Feb 3, 2018
- 13,486
- 21,955
Ni nadra sana mkaka aliyetulia kumkuta anatapanya hela kwa kutoka out na mdada asiye mkewe.
Ila kuna hawa wakaka wahuni wanaojua kucheza na akili za wadada wakurupukaji.
Huwatoa out na kuvinjari kutoka klabu moja kwenda nyingine usiku kucha wadada wakurupukaji hujiona wamepata mtu wa maana mtu wa ndoto zao mwenye kujua mapenzi, hakika kinadada wakurupukaji husisimuliwa sana na mitoko ya hao wakaka wahuni na kujiona wamepata mtu wa maana.
Kwa wakaka waliotulia,wao hurudi maskani mapema mara baada ya kutoka kazini, hawanaga mizunguko kwenye vilabu, Wala mbwembwe nyingi kiasi kwamba huonekana ni 'washamba' mbele za wadada wakurupukaji.
Ni kweli wanawake wanapenda kuolewa na mwanaume wa tabia njema, Ila hujikuta wakiangukia mikononi mwa wakaka wahuni wanaowatoa out kila mara kwa ajili ya kujifurahisha. Mkaka mhuni humfanya mwanamke acheke, husisimua moyo wake, humwambia hasa kile anachotaka kusikia.
Kwa asili wadada hupenda mtu mwenye tabia thabiti kwa mbali - lakini pia hupenda kukaa karibu na wakaka wahuni kwa sababu "they want to hear naughty jokes - they love being teased and seduced.."
Sasa basi wakaka wahuni wana busara zao, wakisha mchota akili mdada mkurupukaji humchukua na kumpeleka nyumbani na kujilia watakavyo, baada ya muda huhamia kwa mdada mwingine na kumtenda vivyo hivyo. Baada ya yule mdada wa kwanza kubaini kwamba haliwagi peke yake hapo sasa hutafuta Wataalam wa magonjwa ya akili huku akitumia dawa za mfadhaiko ili kudhibiti ndoto mbaya zinazomwandama baada ya kugundua kuwa alikuwa anachezewa tu na mkaka mhuni.
Wadada msiwadharau na kuwaona washamba wakaka wasiopenda kuwatoa out.
Mbarikiwe .
Ila kuna hawa wakaka wahuni wanaojua kucheza na akili za wadada wakurupukaji.
Huwatoa out na kuvinjari kutoka klabu moja kwenda nyingine usiku kucha wadada wakurupukaji hujiona wamepata mtu wa maana mtu wa ndoto zao mwenye kujua mapenzi, hakika kinadada wakurupukaji husisimuliwa sana na mitoko ya hao wakaka wahuni na kujiona wamepata mtu wa maana.
Kwa wakaka waliotulia,wao hurudi maskani mapema mara baada ya kutoka kazini, hawanaga mizunguko kwenye vilabu, Wala mbwembwe nyingi kiasi kwamba huonekana ni 'washamba' mbele za wadada wakurupukaji.
Ni kweli wanawake wanapenda kuolewa na mwanaume wa tabia njema, Ila hujikuta wakiangukia mikononi mwa wakaka wahuni wanaowatoa out kila mara kwa ajili ya kujifurahisha. Mkaka mhuni humfanya mwanamke acheke, husisimua moyo wake, humwambia hasa kile anachotaka kusikia.
Kwa asili wadada hupenda mtu mwenye tabia thabiti kwa mbali - lakini pia hupenda kukaa karibu na wakaka wahuni kwa sababu "they want to hear naughty jokes - they love being teased and seduced.."
Sasa basi wakaka wahuni wana busara zao, wakisha mchota akili mdada mkurupukaji humchukua na kumpeleka nyumbani na kujilia watakavyo, baada ya muda huhamia kwa mdada mwingine na kumtenda vivyo hivyo. Baada ya yule mdada wa kwanza kubaini kwamba haliwagi peke yake hapo sasa hutafuta Wataalam wa magonjwa ya akili huku akitumia dawa za mfadhaiko ili kudhibiti ndoto mbaya zinazomwandama baada ya kugundua kuwa alikuwa anachezewa tu na mkaka mhuni.
Wadada msiwadharau na kuwaona washamba wakaka wasiopenda kuwatoa out.
Mbarikiwe .