supercharger GT
JF-Expert Member
- Sep 25, 2016
- 1,017
- 1,965
Hii imekaaje wakuu? Kuna wanawake wa aina flani kwa kweli nashangaa.
Hapa kazini kuna jamaa fulani yupo kitengo tofauti na mimi, ila tunasalimiana! Jamaa mtanashati na mpambanaji kisawa sawa. Kupitia story za jamaa yake wa kitengo hicho,
Nasikiaga alipitia maisha magumu sana kuanzia kusoma, maisha ya kutafuta kazi e.t.c, Sasa wakati anatafuta kazi maisha ndo yakiwa magumu haswaa ndo alikutana na mrembo fulani wakaivana.
Huyu mrembo alikuwa mvumilivu ajabu, na huyu mrembo kwao sio kwamba wana maisha mazuri La Hasha ni kawaida tu ila hawana njaa na hakufanikiwa kufika chuo so yupo tu nyumbani.
Miaka imeenda kama minne hivi jamaa hajapata kazi na mwanamke yupo tu, sometimes anaenda gheto kwa mshikaji na buku buku hizi au buku mbili na mchele kaiba home kwao wanapika maisha yanaendelea.
Cha ajabu jamaa kaja kapata kazi, maisha yakanyooka na nyota ikamuendea vizuri kipindi kile mikopo nje nje kachukua mkopo kajenga kanyumba kadogo fresh na kigari cha kutembelea, hapo ndo maajabu yakatokea, si mwanamke akamuacha bila sababu ya maana! Jamaa ashaweka yule ndo mke wake wa baadaye kwa waliyopitia ila mwanamke kakataa kata kata!
Sababu anazosema ni eti anaona havutiwi tena na yeye, na anaona kama hamjali kama zamani
wanawake wa namna hii sijaelewa huwa wanakuwa wanakuhurumia ukiwa na matatizo au ni vipi? Au ni wale wanaletwa na Mungu ili usijiue kwa matatizo ya dunia???
Kuna anayeweza fafanua hii Scenario humu???
Hapa kazini kuna jamaa fulani yupo kitengo tofauti na mimi, ila tunasalimiana! Jamaa mtanashati na mpambanaji kisawa sawa. Kupitia story za jamaa yake wa kitengo hicho,
Nasikiaga alipitia maisha magumu sana kuanzia kusoma, maisha ya kutafuta kazi e.t.c, Sasa wakati anatafuta kazi maisha ndo yakiwa magumu haswaa ndo alikutana na mrembo fulani wakaivana.
Huyu mrembo alikuwa mvumilivu ajabu, na huyu mrembo kwao sio kwamba wana maisha mazuri La Hasha ni kawaida tu ila hawana njaa na hakufanikiwa kufika chuo so yupo tu nyumbani.
Miaka imeenda kama minne hivi jamaa hajapata kazi na mwanamke yupo tu, sometimes anaenda gheto kwa mshikaji na buku buku hizi au buku mbili na mchele kaiba home kwao wanapika maisha yanaendelea.
Cha ajabu jamaa kaja kapata kazi, maisha yakanyooka na nyota ikamuendea vizuri kipindi kile mikopo nje nje kachukua mkopo kajenga kanyumba kadogo fresh na kigari cha kutembelea, hapo ndo maajabu yakatokea, si mwanamke akamuacha bila sababu ya maana! Jamaa ashaweka yule ndo mke wake wa baadaye kwa waliyopitia ila mwanamke kakataa kata kata!
Sababu anazosema ni eti anaona havutiwi tena na yeye, na anaona kama hamjali kama zamani


Kuna anayeweza fafanua hii Scenario humu???