Kwa maoni yangu kwa situesheni aliyofikia huyu jamaa yetu inabidi kwanza atulie ili interval kati ya uhusiano mmoja na mwingine iweze kumpa nafasi ya kutafakari na kuwa na strategy mpya maana nina hofu kuwa kwa haraka zake anaweza kua anahamisha mapungufu ya uhusiano mmoja na kuyahamishia kwenye uhusiano mpya, Pili ni vizuri akatafakari zaidi kujijua kwality yake na strength zake ili ajue mume bora huwa anakuwaje na yeye ajitengeneze kuwa mume bora yumkini wadada wakikaanae wanamshtukia kuwa yeye siyo mume bora ndo maana wanamkimbia. Kitu kingine ni vyema akajifunza kuwa mtu wa kawaida ( common man) mara nyingi watu wanapenda kuwahadaa wadada kwa kujifanya bab kubwa na mikogo miingi wakati wadada nao skuiz wanajua michano wakiskia tu stori zako za ujanja ujanja wanakukimbia maana wanajua huwezi kuhold maisha kwa uwongo uwongo, mwisho amtangulize mungu katika sala zake aombe kupata mke mwema maana hata akiwa mjanja vipi atabakia kupate mtu mke na siyo mke, matokeo yake ni shida tu.