Wachumba kukimbia tatizo nini?

Wachumba kukimbia tatizo nini?

wakyagara wakinyora

JF-Expert Member
Joined
Jan 1, 2013
Posts
735
Reaction score
286
wana jf salaam,
nimeshindwa kuanalyse situation ya rafiki yangu mmoja hivi ambaye tunafanya kazi,kaniomba ushauri wa kimsaada lakini kwa ushauri niliompa naona kama haujitoshelezi na bado hajapata majibu muafaka wa tatizo lake.swahiba wangu huyu ana nia ya dhati kabisa ya kuoa lakini wachumba wamekuwa wakimkimbia.ndani ya mwaka na nusu sasa amekimbiwa na wachumba watatu na huyu aliyenaye kwa sasa haeleweki.wa kwanza alimfumania lakini hakujua kwanini aliamua kwenda kwa mwanamme mwingine.wakaachana.wa pili aliishi nae kwa muda wa miezi minne lakini baada ya kumeleza kuwa anahitaji akamtambulishe kwa wazazi alikubali,jamaa kaja kazini aliporudi home hakumkuta huyo mdada.alipompigia simu mdada akajibu eti alikuwa na mchumba tayari.watatu ilikuwa siku ya mwakampya wanajiaandaa kutoka lakini ghafla mdada akampigia simu na kumwambia hawataweza kutoka na mapenzi yao yaishie hapo hapo na hana sababu yoyote ya kumpa ila yaishe tu.jamaa kakubali kwa shingo upande.maisha yakaendelea.mwaka huu mwezi wa pili akapata mdada mwingine ambaye anafanya kazi kwenye shirika moja lisilo la kiserikali.baada ya miezi mitano wakakubali wakatambulishane.wakaenda kwanza kwa ndugu wa kijana kisha kwa wazazi wa msichana.baada ya kutoka huko swahiba akapanga mwezi wa tisa apeleke barua ya posa.madada akakubali.ni kama takribani wiki mbili sasa mdada akamfuata jamaa na kumwambia asubiri kwanza kwani sio muda muafaka.cha ajabu amekuwa akipokea simu za swahiba kwa nadra sana bila kuwa na sababu yoyote.jamaa yuko kwenye dilema na hajui kwanini haya yote yanamtokea.nimemuuliza kuhusu kupiga mashine anasema mbona anapiga tuu fresh sasa hajui tatizo litakuwa wapi.plz ushauri wako tafadhali
 
Ungemwambia pia akuoneshe dushelele lake pia......we unafikiri wanawake wajinga nao pia wana haki ya kukataa km dushelele haliheleweki...Ila asikate tamaa na wala asiwe na pupa ndoa ni lifetime commitment so atapata atakae mvumilia..but make sure anakuonesha ''dushelele dushelele dushelele oh
 
Ungemwambia pia akuoneshe dushelele lake pia......we unafikiri wanawake wajinga nao pia wana haki ya kukataa km dushelele haliheleweki...Ila asikate tamaa na wala asiwe na pupa ndoa ni lifetime commitment so atapata atakae mvumilia..but make sure anakuonesha ''dushelele dushelele dushelele oh

sawa mkuu nimeupata ushauri wako lakini hiyo mpaka ya kuonyeshana dushelele is too much.....si unajua tena mapigo hayajalishi size?
 
arudi kijijini akaoe, mbona wenzie tumeoa huko vijijini kwetu!?

ni kweli mkuu hata mimi nilishauri hivyo kwa mara ya kwanza but akadai kuwa atawezaje kumpata mke bora bila ya kujua tabia zake?manake yeye yuko huku kwa miezi 11,ni mwezi mmoja tu kwa mwaka ndio anaenda kijijini.pia mahali alipo ndio anawaona na kufahamu tabia zao
 
Sounds kama kuna some spiritual matters hapa....
 
wana jf salaam,
nimeshindwa kuanalyse situation ya rafiki yangu mmoja hivi ambaye tunafanya kazi,kaniomba ushauri wa kimsaada lakini kwa ushauri niliompa naona kama haujitoshelezi na bado hajapata majibu muafaka wa tatizo lake.swahiba wangu huyu ana nia ya dhati kabisa ya kuoa lakini wachumba wamekuwa wakimkimbia.ndani ya mwaka na nusu sasa amekimbiwa na wachumba watatu na huyu aliyenaye kwa sasa haeleweki.wa kwanza alimfumania lakini hakujua kwanini aliamua kwenda kwa mwanamme mwingine.wakaachana.wa pili aliishi nae kwa muda wa miezi minne lakini baada ya kumeleza kuwa anahitaji akamtambulishe kwa wazazi alikubali,jamaa kaja kazini aliporudi home hakumkuta huyo mdada.alipompigia simu mdada akajibu eti alikuwa na mchumba tayari.watatu ilikuwa siku ya mwakampya wanajiaandaa kutoka lakini ghafla mdada akampigia simu na kumwambia hawataweza kutoka na mapenzi yao yaishie hapo hapo na hana sababu yoyote ya kumpa ila yaishe tu.jamaa kakubali kwa shingo upande.maisha yakaendelea.mwaka huu mwezi wa pili akapata mdada mwingine ambaye anafanya kazi kwenye shirika moja lisilo la kiserikali.baada ya miezi mitano wakakubali wakatambulishane.wakaenda kwanza kwa ndugu wa kijana kisha kwa wazazi wa msichana.baada ya kutoka huko swahiba akapanga mwezi wa tisa apeleke barua ya posa.madada akakubali.ni kama takribani wiki mbili sasa mdada akamfuata jamaa na kumwambia asubiri kwanza kwani sio muda muafaka.cha ajabu amekuwa akipokea simu za swahiba kwa nadra sana bila kuwa na sababu yoyote.jamaa yuko kwenye dilema na hajui kwanini haya yote yanamtokea.nimemuuliza kuhusu kupiga mashine anasema mbona anapiga tuu fresh sasa hajui tatizo litakuwa wapi.plz ushauri wako tafadhali

Huyo jamaa yako ni ''wakijijini type''? Nauliza hivyo kwasababu pengine huyo jamaa yako anachukua wanawake wasio wa ''type'' yake. Hapa nina maana kuwa huenda wanawake wanafanya nae uhusiano ili tu kuweza kumchuna alichonachona lakini wanaona ni mtu ambaye yuko ''too low'' kwenye grade ya kuwa mume wao. Mjini hii ipo sana hasa kwa wanaume wenye kipato kizuri lakini back-ground yao ni washamba washamba. Wanaume wa aina hii unakuta hata kuvaa vizuri hawajui, na mambo mengi wanafanya kishamba kishamba, lakini nao wataka walengeshe masista du wa kileo. Kama jibu ni ndio mwambie ajaribu wanawake wa grade yake hasa wa vijijini.
 
Huyo jamaa yako ni ''wakijijini type''? Nauliza hivyo kwasababu pengine huyo jamaa yako anachukua wanawake wasio wa ''type'' yake. Hapa nina maana kuwa huenda wanawake wanafanya nae uhusiano ili tu kuweza kumchuna alichonachona lakini wanaona ni mtu ambaye yuko ''too low'' kwenye grade ya kuwa mume wao. Mjini hii ipo sana hasa kwa wanaume wenye kipato kizuri lakini back-ground yao ni washamba washamba. Wanaume wa aina hii unakuta hata kuvaa vizuri hawajui, na mambo mengi wanafanya kishamba kishamba, lakini nao wataka walengeshe masista du wa kileo. Kama jibu ni ndio mwambie ajaribu wanawake wa grade yake hasa wa vijijini.


mshikaji ni mtanashati flani hivi,na maanisha ni mtoto wa mjini.labda kama kuna matatizo mengine ambayo siyajui
 
Huenda ana jini mahaba huyo ndiyo maana anakimbiwa na mademu. Ushaur wangu ni huu, Kama ni muislam aende kwa maalim akapate dua, kama ni mkristo aende kwa kiongoz wake wa kiroho na amueleze tatizo lake, nadhan maombi yatasaidia kuondoa tatizo.
 
mshikaji ni mtanashati flani hivi,na maanisha ni mtoto wa mjini.labda kama kuna matatizo mengine ambayo siyajui
Sawa mkuu nimekupata. Lakini mimi naona hamna sababu ya kupaniki kabisa (asijedanganyika ni uchawi nk). Nadhani hii inatokana na aina ya wanawake anaowachagua... (kama hana kasoro eg kutoa harufu mbaya puani nk) ajaribu na kujaribu na kujaribu mwisho atafanikiwa. Halafu mwambie ajaribu kuanzisha uhusiano na wanawake wengi. Sina maana kuwa awe ni play boy hapana, ila afanye urafiki wa kawaida na wanawake wengi kadiri iwezekenavyo... atakuja kushangaa anagombaniwa kama mpira
 
Huenda ana jini mahaba huyo ndiyo maana anakimbiwa na mademu. Ushaur wangu ni huu, Kama ni muislam aende kwa maalim akapate dua, kama ni mkristo aende kwa kiongoz wake wa kiroho na amueleze tatizo lake, nadhan maombi yatasaidia kuondoa tatizo.
asali na kuomba mwenyewe kwa imani, sio kwenda kuombewa tuu
 
ni kweli mkuu hata mimi nilishauri hivyo kwa mara ya kwanza but akadai kuwa atawezaje kumpata mke bora bila ya kujua tabia zake?manake yeye yuko huku kwa miezi 11,ni mwezi mmoja tu kwa mwaka ndio anaenda kijijini.pia mahali alipo ndio anawaona na kufahamu tabia zao

huko kijijini ana ndugu na jamaa ambao anaweza kuwa tumia mkasaidia, akapata mke sio mwanamke! inawezakana jamaa anapata shida kwakuwa anaokutana nao ni mwanamke na sio mke....
 
Mkuu ili linahitaji uangalifu sana, husifikiri kwasababu wewe ulibahatika kupata mke kwa stahili hii basi ita-apply kwa kila mtu.....
huko kijijini ana ndugu na jamaa ambao anaweza kuwa tumia mkasaidia, akapata mke sio mwanamke! inawezakana jamaa anapata shida kwakuwa anaokutana nao ni mwanamke na sio mke....
 
Mkuu ili linahitaji uangalifu sana, husifikiri kwasababu wewe ulibahatika kupata mke kwa stahili hii basi ita-apply kwa kila mtu.....

ni kweli mkuu uangalifu unahitajika tena mkubwa! kwa hali tuendako tunahitaji kurudi miaka ya zamani ya kutumia familia kwa njia moja ama nyingine!
 
Mkuu nina mifano hai ambayo watu wamerudi kwa family kwa ushauri lakini leo hii ndoa zimevunjika au zina hali mbaya kupindukia....
ni kweli mkuu uangalifu unahitajika tena mkubwa! kwa hali tuendako tunahitaji kurudi miaka ya zamani ya kutumia familia kwa njia moja ama nyingine!
 
kuna wanaume wengine wanapenda kuchagua sana utakmkuta mtu mwenyewe mhh.mtu chagua kulingana na wewe utakuta unakakichwa kama papai unataka beyonce wakati unajua pale kumudu beyonce huwezi tafuta size yako mwe
 
Back
Top Bottom