Wachezaji kuhama Yanga kwenda Simba

Mario Kejob

JF-Expert Member
Apr 14, 2020
441
536
Kwa sisi washabiki wa zama hizo tuliowaona Sunday Manara na King Kibaden wakicheza, haikuwa jambo rahisi kwa mchezaji kuhama Yanga kwenda Simba au Simba kwenda Yanga.

Wachezaji walijiunga na vilabu hivi kwa mapenzi yao na vilabu hivyo na hivyo kujitoa kwa moyo wote wakati wakichezea vilabu hivyo.

Mambo yaliyozuka siku hizi kwa mfano kumuona Ajibu Akichezea Simba msimu huu na msimu unaofuata akichezea Yanga yanapunguza ushabiki na hata thamani na upenzi wa mchezaji. Enzi hizo huu ulikuwa ni usaliti mkubwa.

Tumeyaona haya pia kwa Niyonzima na nenda rudi zake na labda hivi karibuni yatajirudia tena kwa Shishimbi na Morrison.

Mimi kama mshabiki wa Simba silifurahii swala hili kabisa na kama Yanga imewaacha wangeenda tu vilabu vingine kama Azam ambayo ingekuwa inawahitaji.

Na wala sioni haja yoyote kama Simba inawahitaji wachezaji hao kwa sasa kwani team inaonekana iko vizuri tu.

Hivyo, nawaomba viongozi wa Simba kama walikuwa na mpango huo waufutilie mbali kabisa kwani hauna tija yoyote kwenye club.
 
Ni kweli usemavyo mkuu lakini wakati ukuta, ukishindana nao utaumia buure. Enzi zimebadilika. Zamani soka letu lilikua la ridhaa na sio professional. Utakuta mchezaji wa Premier League anakazi yake nyingine kaajiriwa na soka ni kama burudani tu

Siku hizi mpira ni ajira na biashara kubwa. Kitendea kazi kwenye tasnia hii ni afya na umri wa mtu. Mchezaji anahakikisha wakati akiwa vizuri kimwili na kiakili na umri unamruhusu basi anapata maslahi yake yatakayo muwezesha kuishi vizuri wakati na baada ya kucheza soka. Na hapo hatajali timu anayohudumu inaitikadi gani au inavaa rangi gani!

Wengi wa wachezaji wa zamani waliocheza kwa mahaba na kujitolea kwenye timu zao leo hii wapo hoi kiuchumi na si club au wanachama na wapenzi wa timu zao wanaowaangalia kwa lolote lile! Vijana wa siku hizi wamejifunza na wameamka
 
unaweza kudhani mmewapa mamlaka ya kuamua watu wenye akili kumbe ni shida. unawezaje kufikiria kumsajiri Morrison ambae ameonyesha kiwango cha juu cha uhuni. unawezaje kufikiria kumleta Shishimbi kwa kiwango gani cha kumzidi Mkude na Fraga. kama wanafikiri hivyo basi ni wajinga sana. na hawatazami mpira kama sisi
 
unaweza kudhani mmewapa mamlaka ya kuamua watu wenye akili kumbe ni shida. unawezaje kufikiria kumsajiri Morrison ambae ameonyesha kiwango cha juu cha uhuni. unawezaje kufikiria kumleta Shishimbi kwa kiwango gani cha kumzidi Mkude na Fraga. kama wanafikiri hivyo basi ni wajinga sana. na hawatazami mpira kama sisi
Kama watamsajili Tshishimbi na kumwacha Shibob nitakubaliana na wale wanaosema Mo hafai ni tapeli
 
Ni kawaida tu kwa mchezaji kuhama timu hizo. Mchezaji yeye yupo kazini, sio shabiki wa timu yoyote.

Mfano Gadiel Michael alivyokuwa Yanga alikuwa anacheza mechi zote. Alivyohamia Simba amekuwa hapati nafasi ya kucheza.
Ni maamuzi ya busara sana kwa msimu huu kaamua kurudi tena Yanga.
 
Ni kawaida tu kwa mchezaji kuhama timu hizo. Mchezaji yeye yupo kazini, sio shabiki wa timu yoyote.

Mfano Gadiel Michael alivyokuwa Yanga alikuwa anacheza mechi zote. Alivyohamia Simba amekuwa hapati nafasi ya kucheza.
Ni maamuzi ya busara sana kwa msimu huu kaamua kurudi tena Yanga.
nu kawaida tu bila kujali mahitaji,au sio?!!
 
Ni kawaida tu kwa mchezaji kuhama timu hizo. Mchezaji yeye yupo kazini, sio shabiki wa timu yoyote.

Mfano Gadiel Michael alivyokuwa Yanga alikuwa anacheza mechi zote. Alivyohamia Simba amekuwa hapati nafasi ya kucheza.
Ni maamuzi ya busara sana kwa msimu huu kaamua kurudi tena Yanga.
nu kawaida tu bila kujali mahitaji,au sio?!!
 
unaweza kudhani mmewapa mamlaka ya kuamua watu wenye akili kumbe ni shida. unawezaje kufikiria kumsajiri Morrison ambae ameonyesha kiwango cha juu cha uhuni. unawezaje kufikiria kumleta Shishimbi kwa kiwango gani cha kumzidi Mkude na Fraga. kama wanafikiri hivyo basi ni wajinga sana. na hawatazami mpira kama sisi
Mkuu hilo kwa timu za Bongo linawezekana kabisa. Angalia mlolongo huu; Morrison amefanya uhuni South Africa, DR Congo na hatimaye hapo kwa Wana Yanga. Ina maana Viongozi wa Yanga hawakujua hili? Sasa Simba nao wanataka kutumbukia mlemle. Halafu ukiangalia viwango vya uchezaji vya akina Morrison na Tshishimbi havitofautiani na viwango vya wachezaji wetu wa ndani akina Miraji (Shaver) na Zawadi Mauya. Tena wachezaji wa nje ni wadenguaji na wasumbufu, akiona mnaenda kucheza mechi Lindi anajifanya anaumwa au ana matatizo ya kifamilia. Ifike mahali tuwaamshe vijana wetu wajitambue na tusitegemee tena wachezaji kutoka nje.
 
unaweza kudhani mmewapa mamlaka ya kuamua watu wenye akili kumbe ni shida. unawezaje kufikiria kumsajiri Morrison ambae ameonyesha kiwango cha juu cha uhuni. unawezaje kufikiria kumleta Shishimbi kwa kiwango gani cha kumzidi Mkude na Fraga. kama wanafikiri hivyo basi ni wajinga sana. na hawatazami mpira kama sisi
Malengo yao ni kuikomoa Yanga sio kusajili wachezaji wazuri, hapa naona ushabiki sio ufanisi.
 
Mkuu hilo kwa timu za Bongo linawezekana kabisa. Angalia mlolongo huu; Morrison amefanya uhuni South Africa, DR Congo na hatimaye hapo kwa Wana Yanga. Ina maana Viongozi wa Yanga hawakujua hili? .
Yanga walijua,kwa Yanga mengi inafanya kama trial kutokana na uwezo mdogo. ila kwa Simba hii ni ngumu kumeza
 
unaweza kudhani mmewapa mamlaka ya kuamua watu wenye akili kumbe ni shida. unawezaje kufikiria kumsajiri Morrison ambae ameonyesha kiwango cha juu cha uhuni. unawezaje kufikiria kumleta Shishimbi kwa kiwango gani cha kumzidi Mkude na Fraga. kama wanafikiri hivyo basi ni wajinga sana. na hawatazami mpira kama sisi
Kaka, wataalam wa Soka Duniani wanakwambia kwamba wakati mwingine unasajili mchezaji au kumzuia mchezaji kuondoka SIYO KWAMBA UNATAKA KUMTUMIA BALI UNAZUIA SILAHA HIYO KUMFIKIA ADUI YAKO (AJIB/NDEMLA). Ni mbinu ambayo ilitumika sana Ulaya hasa EPL wakati Morinyo akiwa kwenye ubora wake na inaendelea kutumika hadi sasa, au wengine wanaenda mbali zaidi wanakupa Mchezaji kwa Mkopo lkn asicheze mechi so and so. Siku nyingine ntakupa somo refu juu ya hii
 
Hao wa zama za akina Kibaden wengi wamefariki wakiwa masikini wakutupwa.

Hawa vijana wanajaribu kurekebisha makosa,popote penye dau wanaenda ila huyo Ajib ndo zero brain!
 
Back
Top Bottom