Dharra
JF-Expert Member
- Jun 23, 2017
- 1,661
- 2,970
Mwaka 2014 Mwezi wa December, niliomba likizo kazini na nilipanga baada ya mapumziko mafupi dar niende kutembea Arusha/moshi kwa mara kwanza katika maisha yangu, nikamtaarifu rafiki yangu fredy dhamira yangu hio na kwa vile yeye alikuwa mwenyeji wa maeneo hao na akanipa ushauri kwamba tarehe 21 nitaelekea home moshi kama hutojali nitakupa lift, nikasema poa. Siku ya safari imefika mkutano ni maeneo ya manzese nakumbuka ilikuwa siku ya Jumapili, saa kumi na mbili safari ikaanza, Ndani ya Noah tulikuwa jumla ya abiria 3, mimi na warembo wawili nadhani walikuwa ni below 20 na walifanana sana Fredy akanitambulisha kuwa hawa ni ndugu zangu na tutakuwa nao safari moja. Baada ya kukuru kakara za road tulifika Moshi majira ya saa kumi jioni. Nikamueleza fredy nia yangu ya kuendelea na safari to Arusha sababu sikuwa na siku nyingi za kuspend huko, akanikubalia na kunieleza kuwa wao bado wako safarini kuelekea wilayani kwao ambapo wanatazamia kuwasili saa mooja jioni. Tukaachana. Baada ya kuhangaika kwa muda kutafuta walao basi zuri (sio mpenzi wa coaster) hatimae niliamua kulala Moshi ili asubuhi niendelee na safari yangu kwa ufasaha zaidi. Nikaelekezwa hoteli moja ya gorofa ambayo haipo mbali na stand kuu. Muhudumu pale akanipa hongera maana chumba kilibaki kimoja tu. call room service, sikutoka hadi siku ya pili saa mbili asubuhi, Kilihonishangaza asubuhi namkuta fredy anakagua Noah pale kwenye parking ya hoteli tayari kwa safari nikashangaa sana!!!! nae baada ya kuniona akashangaa pia. tukawa tunaulizana kulikoni? Akaniambia nisingeweza kwenda mpaka wilayani na mabinti warembo vile bila ya kuonja mkuu. Nimelala nao room moja na kiufupi baada ya vyombo hatukulala usiku kucha, nimewacha huko wanajiandaa tunaondoka. Jamani wa Northern njiani salama huko? Sio mbaya na wewe ukatupia ulioyaona ama kusikia kuhusu ndugu zetu hawa katika safari zao hizi za mwisho wa mwaka