Wabunge wawili wa CCM wabainika kuhusika na ujangili

Informer

JF-Expert Member
Jul 29, 2006
1,599
6,670
WABUNGE wawili wa Chama cha Mapinduzi (CCM), wamebainika kuhusika na vitendo vya ujangili wa kuua tembo, jambo linazorotesha vita dhidi ya ujangili inayofanywa na serikali.

Baada ya kufuatilia kwa karibu matukio ya kesi za ujangili tangu mwaka 2009 hadi mwaka huu, imebainika kuwa baadhi ya wanasiasa wamekuwa wakihusishwa na ujangili, huku vyombo vya dola vikipata shida kukabiliana na vita hiyo kutokana na wanasiasa hao kutumia baadhi ya viongozi ndani ya serikali kufanikisha mbinu za ujangili.

Hata hivyo, taarifa zinaeleza kwamba vyombo vya dola vinaendelea kukusanya ushahidi na kufuatilia nyendo za wanasiasa hao (mawaziri wa awamu iliyopita?) kwa lengo la kuhakikisha kwamba wanachukuliwa hatua. Kwa upande mwingine serikali imeazimia kuvunja kabisa mtandao wa ujangili uliowekwa kwa miaka mingi ukihusisha baadhi ya watendaji wa Idara na taasisi zinazopaswa kupambana na ujangili.

Tukio lililoibua upya uchunguzi dhidi ya wahusika wakuu ni lile la kutunguliwa kwa helikopta iliyokuwa ikisaidia walinzi wa Idara ya wanyamapori katika mbuga ya hifadhi ya Mwiba wilayani Meatu.Tukio hilo ambalo lilisababisha kifo cha rubani wake raia wa Uingereza kwa kupigwa risasi na majangili.

Taarifa zaidi zitashushwa hapa JF muda ukiruhusu

==============

1460631929069.jpg



Gari mojawapo la kampuni inayomilikiwa na Mbunge anayehusishwa na Ujangili]
 
WABUNGE wawili wa Chama cha Mapinduzi (CCM), wamebainika kuhusika na vitendo vya ujangili wa kuua tembo, jambo linazorotesha vita dhidi ya ujangili inayofanywa na serikali.

Baada ya kufuatilia kwa karibu matukio ya kesi za ujangili tangu mwaka 2009 hadi mwaka huu, imebainika kuwa baadhi ya wanasiasa wamekuwa wakihusishwa na ujangili, huku vyombo vya dola vikipata shida kukabiliana na vita hiyo kutokana na wanasiasa hao kutumia baadhi ya viongozi ndani ya serikali kufanikisha mbinu za ujangili.

Hata hivyo, taarifa zinaeleza kwamba vyombo vya dola vinaendelea kukusanya ushahidi na kufuatilia nyendo za wanasiasa hao (mawaziri wa awamu iliyopita?) kwa lengo la kuhakikisha kwamba wanachukuliwa hatua. Kwa upande mwingine serikali imeazimia kuvunja kabisa mtandao wa ujangili uliowekwa kwa miaka mingi ukihusisha baadhi ya watendaji wa Idara na taasisi zinazopaswa kupambana na ujangili.

Tukio lililoibua upya uchunguzi dhidi ya wahusika wakuu ni lile la kutunguliwa kwa helikopta iliyokuwa ikisaidia walinzi wa Idara ya wanyamapori katika mbuga ya hifadhi ya Mwiba wilayani Meatu.Tukio hilo ambalo lilisababisha kifo cha rubani wake raia wa Uingereza kwa kupigwa risasi na majangili.

Taarifa zaidi zitashushwa hapa JF muda ukiruhusu
Yaani CCM haitakaa salama kwa kila jambo
 
Hiki chama hiki haki ya nani hakina tofauti na genge mashetani. Kila kile kinachorudisha nyuma Maendeleo ya nchi wao wapo na chama kilikuwa kinawalinda. Mara KM, mara wabunge Nk Nk halafu bado kuna watu wameelimika na wanauwezo wa kuelewa uovu huu wa CCM lakini bado wanaunga mkono huku wao wamepigika kweli!
 
Back
Top Bottom