Mimi si mpenzi sana wa siasa wala si mwanachama wa chama chochote na nilipiga kura nilipokuwa na miaka 18 miaka 20 iliyopita na nilipiga kwa vile nilitaka kujaribisha ila sijaona cha mabadiliko yoyote kwa kweli ndio maana huwa sihangaiki kwenda kupanga foleni.
Katika kipindi hiki cha kutaka mabadiliko kuna wabunge wanaotaka kuingia kuwasilisha majimbo yao na kunawanaotaka kubakia kuendelea kwenda kusinzia bungeni.Mimi binafsi ninaonelea kuwa ni wakati muafaka wa wabunge kufanyakazi kiukweli wawekewe KPI ( Key perfomance indicators) ziwe zinakuwa reviewed kila mwaka na kama hujatimiza malengo kwa asilimia 75% unapigwa chini anachaguliwa mbunge mwingine mwenye ufanisi.
Nasema hivi kwanini? Sioni sababu ya mtu kuchaguliwa wakati kuna basic things ambazo unaweza kujituma kuvifanya aidha kwa kuhamasisha watu wa jimbo lako au kutafuta misaada mbali mbali kwa wafanya biashara wa eneo lako bila kugonjea serikali. Vitu muhimu kama Zahanati, shule, maji na mambo mengine madogo madogo kwa kweli huwa nasikia uchungu sana kwamba tangu nimezaliwa shida ni zile zile hadi leo hii naelekea uzeeni.
Kwa wabunge vijana na wazee wa chama chochote kile wekeni KPI's kwa wawakilishi wenu muwa tathmini baada kipindi maalum, laasivyo mtajaza wauza sura, mafisadi, wasinziaji na wahongaji lazima ifikie wakati mtu uchaguliwe kwa ulichofanya tena kwa kiasi kikubwa ili tunapokuchagua tena tunajua tunachagua nini hapo ndio maendeleo yatapatikana wakati wa kubebana umekwisha
Amani kwenu, mfungo mwema na uchaguzi mwema
Katika kipindi hiki cha kutaka mabadiliko kuna wabunge wanaotaka kuingia kuwasilisha majimbo yao na kunawanaotaka kubakia kuendelea kwenda kusinzia bungeni.Mimi binafsi ninaonelea kuwa ni wakati muafaka wa wabunge kufanyakazi kiukweli wawekewe KPI ( Key perfomance indicators) ziwe zinakuwa reviewed kila mwaka na kama hujatimiza malengo kwa asilimia 75% unapigwa chini anachaguliwa mbunge mwingine mwenye ufanisi.
Nasema hivi kwanini? Sioni sababu ya mtu kuchaguliwa wakati kuna basic things ambazo unaweza kujituma kuvifanya aidha kwa kuhamasisha watu wa jimbo lako au kutafuta misaada mbali mbali kwa wafanya biashara wa eneo lako bila kugonjea serikali. Vitu muhimu kama Zahanati, shule, maji na mambo mengine madogo madogo kwa kweli huwa nasikia uchungu sana kwamba tangu nimezaliwa shida ni zile zile hadi leo hii naelekea uzeeni.
Kwa wabunge vijana na wazee wa chama chochote kile wekeni KPI's kwa wawakilishi wenu muwa tathmini baada kipindi maalum, laasivyo mtajaza wauza sura, mafisadi, wasinziaji na wahongaji lazima ifikie wakati mtu uchaguliwe kwa ulichofanya tena kwa kiasi kikubwa ili tunapokuchagua tena tunajua tunachagua nini hapo ndio maendeleo yatapatikana wakati wa kubebana umekwisha
Amani kwenu, mfungo mwema na uchaguzi mwema