Wabunge walio wengi wakosa hoja

Wabunge walio wengi wakosa hoja

djcastlelite

Senior Member
Joined
Mar 8, 2014
Posts
159
Reaction score
21
Dodoma. Wabunge walio wengi wamekosa hoja na badala yake wamebaki wakimkosoa warioba na kungangania mfumo wa serekali mbili bila kutoa hoja nzito ni kwa nini wanakataa mfumo wa serekali tatu,mmoja wa wabunge wa kundi la walio wengi wamesema kuwa wanaongangania mfumo wa serekali tatu wanapigania madara, wasomi wengi na watalamu wamesema hizo ni propaganda kuwa serekali tatu zinaongeza garama, watalamu wameenda mbali zaidi na kubaini serekali tatu zitapunguza garama kwa kuwa serekali itakua na mawaziri kumi na tano tu na wabunge sabini peke yake hamsin kutoka tanganika na ishirini kutoka zanzibar
 
Bado wapo kianolojia zaidi,by the time wakiamua kuingia kidijitali watakuwa wameshachelewa.
 
Kiukweli nimemkubali sana james mbatia kwa ustaraabu,hoja nzito na zenye ukweli mtu na takwimu za kweli.ole wenu mnao watukana wasisi wetu akiwemo warioba na jopo lake.
 
Yaani wapowapo tu kama kikundi cha wapewa ofa Bar, wao ni kumtetea mtoa ofa bila kujali anachokisema wala akitendacho.
 
Kwa kweli inasikitisha sana kuona kamati karibu zote kwa upande wa ccm (wanaojiita wajumbe walio wengi) kila ripoti ni cut and paste. Kulikuwa na haja gani ya kuunda kamati zote hizo ambazo zimeongeza gharama kwa kukodi kumbi za hoteli maalufu na kutumia muda mwingi halafu ripoti zote zifanane. Pamoja na kwamba ccm walikuwa na maoni yao, inaonekana wajumbe wa ccm hawakujishugulisha na kuboresha rasimu na akili zao zimeshikiliwa na kikundi fulani.
Naona watanzania inabidi tuwe wakali kwenye masuluala yanayohusu Taifa maana naona hapa watanganyika tunachezewa akili. Hoja za ccm za kuwa tuwe na Muungano wenye Serikali ila ulifanyiwa marekebisho ambayo wamekuwa wakiyahubiri kila siku hazina hazitufai watanganyika. Hoja zao zote zimeegemea kuinufaisha zaidi Zanzibar kwa kuipa uhuru zaidi na cha ajabu wanaharilisha uvunjwaji wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano uliofanywa na Zanzibar.

Hoja za CCM za Muungano ulioboreshwa ziko wapi?????
 
Ata JK angejuwa kama wajumbe wa bunge la katiba watakuja kulinganisha takwimu za kuchaguliwa kwake 26% ya Watanzania na akawa Rais wa Tanzania nzima na takuwimu za Warioba kwamba ni takwimu chache kulingana na idadi ya Watanzania nadhan angeliacha hii point akaja akaeupa hii aibu leo iliyomkuta Bungeni.,
 
Yaani wapowapo tu kama kikundi cha wapewa ofa Bar, wao ni kumtetea mtoa ofa bila kujali anachokisema wala akitendacho.
Hasa yule mjumbe mlemavu wa macho, jamaa amelewa U-CCM kweli kweli!
 
Kupinga uwepo wa Serikali ya Tanganyika kunawagharimu sana....!
Kwanza lazima ujitoe uzalendo wa kuikana nchi yako, dhambi inayowakalia!
Pili lazima ujifanye hamnazo kuupinga ukweli usiopingika ila kwa blaa blaa!
Tatu lazima uwe mnafiki kama mwanazuoni fulani!

Zaidi sana watabeba hukumu ya kihistoria milele.....!
 
Hawawezi kuwa na hoja kwa sababu suala la msimamo wa chama/serikali mbili wanalazimika kulifuata bila utashi wao! Na hiyo kanuni inayotaka m/kiti wa kamati kuwasilisha pia maoni ya wachache ni nzuri sana!

TBCcm wanatamani wasirushe matangazo inapofika hatu ya maoni ya wachache na ufafanuzi wake..lakini hawana namna!
 
All is well
 

Attachments

  • BUNGENI.jpg
    BUNGENI.jpg
    21.1 KB · Views: 105
Hawakupewa nafasi ya kuijadili kwa pamoja ili wapeane hoja za kujitetea ndo maana wakapewa muda wa kuikariri na kuitoa kiuzalendo.
Wanaposema kuwa uwe muungano wa serekali 2 ulioboreshwa; hayo maboresho mbona hakuna hata kamati moja tu kati ya hizo 12 iliyotoa mfano wa maboresho hayo? Zaidi sana ni kuiambia Zanziba kuwa Gas na Petroli hatutaiweka chini ya muungano?? Ili Zanziba wazidi kupewa hallua?? Ama kweli, Tz kuna mambo mapya kiila siku. Hamuoni huku ni kuitukana Zanziba kuwa wao wanalilia sukari tu??
Umeme wameutumia miaka yoote, Mtanganyika ndo anamlipia, Mafuta tunayapitishia bara, yanaenda kwao ka yametoka Pemba tu, Serekali ya Muungano jamani ni ipi hiyo iliyojiunga na Zanziba??
Kila mjumbe akisimama anadiriki kusema kuwa kuwe na Serekali inayoitwa ya Muungano na Serekali ya Zanziba. Hainiingii akilini kuwa hiyo nchi inayoitwa Serekali ya Muungano ni ipi na ya Zanziba ni ipi. Hii ya muungano imetoka wapi bila hiyo Zanziba???
Nimeshaleweshwa na sauti hizi za wenyeviti wa kipekee wasiojua hata wanachokisema. Nasema, Semeni mtakavyo ila kuna siku, Tutaenda UN kuudai uraia wetu mlio tunyang'anya kwa utapeli. CCM Oyeeeee.
 
Wame nyimwa uhuru wa kujieleza na uhuru wa kuamua ndio maana wamenyimwa kupiga kura ya siri yani ni nisawa na mke lazima afuate matakwa ya mume wake! Kama mume hafuati haki sawa!
Ama ccm wamewazihirishia wabunge wao kuwa ukiolewa shari ulale bila chuuuupi !
Kama hawajaole na uhuru wao hauja bakwa basi wapige kura za siri kwenye maamuzi!
Ama kwa lugha raisi ni nchi imenunuliwa na genge la wahuni na kama vijana hatutakuwa makini ni hatari sana kuwa na wabunge walio olewa na waliyo bakwa uhuru wa kuamua mambo ya msingi tutaishia kusikia maendeleo kwa wengine.eeemungu muumba wa mbingu na ardhi waokowe vijana wa lumbumba dhidi ya mafisadi wanao baka uhuru wao na akili zao
 
Ata JK angejuwa kama wajumbe wa bunge la katiba watakuja kulinganisha takwimu za kuchaguliwa kwake 26% ya Watanzania na akawa Rais wa Tanzania nzima na takuwimu za Warioba kwamba ni takwimu chache kulingana na idadi ya Watanzania nadhan angeliacha hii point akaja akaeupa hii aibu leo iliyomkuta Bungeni.,

sio asilimia 26 bali ni asilimia 10. kwa sababu alichaguliwa na watu millioni 5
 
Back
Top Bottom