Wabunge walalamikia adhabu ya kijana aliyemtukana rais kuwa ni ndogo, Waziri wa Sheria azungumza

tajirijasiri

JF-Expert Member
Oct 13, 2012
2,864
3,851


Wabunge wamelalamikia adhabu aliyopewa kijana wa Arusha aliyemtukana rais kuwa ni ndogo kwa kuwa mhalifu alipewa alipe kiasi cha fedha na kulipa kwa mafungu kwa kuwa alitenda kosa kubwa la kumdhalilisha mtu wa juu katika nchi hii

==========

My Take
Wabunge kuhoji Mamlaka ya Mahakama ni dalili mbaya ya Udikteta. Mahakama inapotoa Hukumu halafu anaibuka Mbunge wa CCM anahoji hukumu hiyo, kisha Waziri wa Sheria anaahidi kuileta hukumu Bungeni ni dalili mbaya sana kwa Utawala wa Sheria.

Hayo yemetokea leo Bungeni Dodoma, wakati Mbunge wa CCM Livingstone Lusinde alipohoji uhalali wa hukumu halali ya Mahakama dhidi ya Kijana aliyeshtakiwa kwa kumkashifu JPM. Kama serikali haijaridhika na hukumu basi ifuate sheria kwa kukata rufaa.

June 21, 2016 Mbunge wa Nchemba, Juma Nkamia alisimama bungeni kuomba mwongozo wa bunge kujadili tukio la mtuhumiwa wa kesi ya kumtukana Rais Magufuli kuchangiwa fedha na watu kwa ajili kulipa fidia, kitendo kinachoashiria dharau. Mwongozo wa Nkamia ukaungwa mkono pia na Mbunge wa Mtera Livingstone Lusinde.

Nkamia alisema. "Kuna mtu alimtukana Rais na akahukumiwa kwenda jela au kulipa faini ya milioni 7, alilipa nusu ya faini ile na akaruhusiwa aondoke akatafute fedha nyingine. Nilitaka wanasheri watusaidie, hivi kumtukana Rais wa nchi alafu yule aliyetukana anaruhusiwa akatafute fedha za kulipa" –Juma Nkamia

‘Siku ya kukabidhiwa fedha anaita na waandishi wa habari, na baadhi ya wabunge humu ndani wa chama fulani walionyesha wananchangia fedha yule mtu ili akalipe faini. Kwahiyo ni maana kuwa alitumwa na chama hicho akamtukane Rais.’ –Juma Nkamia

‘Sasa naomba kujua sio dharau kwa Rais? sheria inaruhusu jambo hili kufanyika? na kama mimi leo nikahukumiwa kwa kesi ya kuiba kuku siwezi kuruhusiwa kutafuta fedha, iweje mtu huyu akaruhusiwa kutoka nje kutafuta fedha na bado akaonekana watu wakimkabidhi fedha? hizi ni dharau kwa taifa kwa ujumla‘ –Juma Nkamia

Sasa wataalam naomba mtueleze bunge lina legitimacy ya kujadili mchakato wa utekelezwaji wa hukumu iliyotolewa na muhimili tofauti usioingiliana kikatiba?

Alafu kwanini anataka kujadili hii hukumu wakati huu ambapo watu wameonekana kumchangia kiasi Fulani kilichobakia na wala sio Mara baada ya hukumu kutolewa?
 
Wabunge kuhoji Mamlaka ya Mahakama ni dalili mbaya ya Udikteta. Mahakama inapotoa Hukumu halafu anaibuka Mbunge wa CCM anahoji hukumu hiyo, kisha Waziri wa Sheria anaahidi kuileta hukumu halali ya Mahakama, Bungeni, ni dalili mbaya sana kwa Utawala wa Sheria. Hiyo imetokea leo Bungeni wakati Mbunge wa CCM alipohoji uhalali wa hukumu aliyopewa mtuhumiwa wa kesi ya Kumkashifu Rais. Kama Serikali na Bunge hawajaridhika, basi wakate rufaa na sio kuchukua hukumu na kuileta Bungeni. Mwakyembe usilete mchemko Bungeni. Wewe ni nguli wa Sheria.

Source ITV habari.
 
Wabunge kohoji Mamlaka ya Mahakama ni dalili mbaya ya Udikteta. Mahakama inapotoa Hukumu halafu anaibuka Mbunge wa CCM anahoji hukumu hiyo, kisha Waziri wa Sheria anaahidi kuileta hukumu Bungeni ni dalili mbaya sana kwa Utawala wa Sheria.

Source ITV habari.

Mkuu asante kwa kuliona hilo so fast. Mimi nabakiza maneno ya akiba lakini my initial comment ni kuwa Mh. Waziri ni Dk. Mbunge wa kuchaguliwa, mwalinu wa sheria na waziri ikimmanisha ni mshauri mkuu wa Mh. Rais katika mambo ya sheria. Tone aliyoitumia ilipaswa kuwa tofauti.
 
Siku zote spika au naibu wake wamekuwa wakisema hawana uwezo wa kuhoji maamuzi ya mahakama au kuzungumzia kesi iliyopo mahakamani kwa kuwa huo ni Muhimili unaojitegemea. Lakini leo wabunge wale wale wamehoji maamuzi ya mahakama kuhusu kesi iliyootolewa hukumu na mahakama na naibu spika ameruhusu wajadili. Je sasa ndo kusema bunge linaongozwa toka ikulu au udhaifu wa uongozi wa Bunge unaruhusu bunge kutumiwa na mihimili mingine. Karibu kwa mjadala wenye tija
 
Wabunge kuhoji Mamlaka ya Mahakama ni dalili mbaya ya Udikteta. Mahakama inapotoa Hukumu halafu anaibuka Mbunge wa CCM anahoji hukumu hiyo, kisha Waziri wa Sheria anaahidi kuileta hukumu halali ya Mahakama, Bungeni, ni dalili mbaya sana kwa Utawala wa Sheria. Hiyo imetokea leo Bungeni wakati Mbunge wa CCM alipohoji uhalali wa hukumu aliyopewa mtuhumiwa wa kesi ya Kumkashifu Rais. Kama Serikali na Bunge hawajaridhika, basi wakate rufaa na sio kuchukua hukumu na kuileta Bungeni. Mwakyembe usilete mchemko Bungeni. Wewe ni nguli wa Sheria.
Source ITV habari.
Lakini nyinyi kuhoji ni sawa eti? Wafuasi wa chadema walihoji na kulalamika juu ya hukumu ilikua sawa? Pili umerupuka tu kujiandikia umemsikiliza mwakyembe kwa makini alichosema?
 
Mahakama ni mhimili unaojitegemea na huru kama ilivyo kwa Serikali na Bunge. Mahakama huamua kesi zinazopelekwa huko kwa kuzingatia taratibu,mazingira na matakwa ya kisheria.

Leo Bungeni Dodoma,kama ilivyoripotiwa ITV,kuliombwa mwongozo wa Spika uliohoji uhalali wa hukumu ya faini ya milioni saba iliyotolewa na Mahakama huko Arusha kwa kijana Emily aliyeshtakiwa kwa kumkashifu Rais John Pombe Magufuli. Mwongozo huo ulijibiwa na Waziri wa Katiba na Sheria,Dr. Harrison Mwakyembe badala ya Kiti cha Spika.

Mwongozo huo ulioombwa na Mbunge wa Mtera,Livingstone Lusinde(CCM) ulilenga kujadili na kuonyesha kutokukubaliana na hukumu ya Mahakama. Utaratibu huo si sahihi. Uamuzi wa mahakama hupingwa kimahakama kwa mujibu wa taratibu zilizowekwa. Uamuzi huo,kama hauridhishi,ulipaswa kukatiwa rufaa Mahakama Kuu ya Tanzania.

Kujadili kisiasa uamuzi wa Mahakama Bungeni si suala la kulipongeza. Ingawa Waziri Mwakyembe ameahidi kutoa taarifa rasmi baada ya kuwasiliana na Mkurugenzi wa Mashtaka pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali,taarifa yake yaweza kuharibu zaidi.

Pamoja na wengi wetu kuguswa na kuchukizwa na kudhalilishwa au kusemwa vibaya Rais,sheria inataka uamuzi huo upingwe kimahakama badala ya kujadiliwa kisiasa. Mkurugenzi wa Mashtaka anaifahamu vyema Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai.
 
Bado sijaelewa, je akisha peleka nakala ya hukumu bungeni, ndiyo wataijadili au wataikosoa, je kuna anayefahamu mwaka gani bunge limeshawahi kujadili hukumu fulani?
Mleta mada kapotosha, mwakyembe kasema kwanza akaipitie hukumu yenyewe maana hajui imeandikwajwe, pili ataipeleka kwa mkuregenzi wa mashtaka na mwanasheria mkuu wa serikali ili awasikilize ushauri atakaoupata ndio atauleta bungeni na kua ndo msimamo wa serikali,
 
Hivi hii sheria imetungwa kwa ajili ya rais tu? Mbona Kuna viongozi wengi na wananchi wanatukanwa na hakuna anayekamatwa? Ukiwa mwana ccm hata uwe professor huna tofauti na mtoto wa vidudu. Ndo maana mawazo ya lusinde hayana tofauti na ya mwakyembe anayedai ana PhD ya sheria
 
Mleta mada kapotosha, mwakyembe kasema kwanza akaipitie hukumu yenyewe maana hajui imeandikwajwe, pili ataipeleka kwa mkuregenzi wa mashtaka na mwanasheria mkuu wa serikali ili awasikilize ushauri atakaoupata ndio atauleta bungeni na kua ndo msimamo wa serikali,
Msimamo wa serikali kwenye hukumu ya Mahakama, unaletwa Bungeni kufanya nini badala ya kuupeleka kwa Mwanasheria na Mawakili wa Serikali, ili waone kama wametendewa Haki au la ili wakate rufaa?
Tangu lini Bunge likaletewa Msimamo wa Serikali kwenye Hukumu za Mahakama?
Chama Cha Majipu (CCM) mnalewa madaraka.
 
Vipi hawakuulizia kesi ya Mbowe iliyofunguliwa Mwanza kutupiliwa mbali na jaji??
 
Nimeamini wafuasi wengi wa humu wanaokosoa serikali hua hata hawajui kitu kwa undani, mtu anaanza tu kuropoka na kuiponda serikali ilimradi tu kamsiki mtu kaponda, ina mana wote hamjamsikia mwakyembe alivyosema kwanza akaisome hiyo hukumu na ataipitisha kwa mkurugenz wa mashtaka na AG ndo ailete tena bungeni? Mnasikitisha, Tena mnaolalamika hvyo ndo wale wale mliolalmikia hukumu je na nyie hamkua mnaingilia maamuzi ya mahakama?
 
Back
Top Bottom