abdulahsaf
JF-Expert Member
- Aug 31, 2010
- 858
- 130
[h=1]
[/h]
Na Mwinyi Sadallah
23rd June 2012
Sakata la kero za Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, limechukua sura mpya baada ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi (BLW), kulalamika kuwa wabunge kutoka Zanzibar wamekuwa mzigo kutokana na kushindwa kutetea maslahi ya Zanzibar katika mfumo wa muungano huo.
Tamko hilo wamelitoa walipokuwa wakichagia bajeti ya serikali ya mwaka wa fedha 2012/2013 katika Kikao cha Baraza la Wawakilishi, kinachoendelea Chukwani mjini Zanzibar jana.
Akichagia bajeti hiyo Mwakilishi wa Jimbo la Kitope, Makame Mbarouk Mashimba, (CCM), alisema kwamba Zanzibar kwa muda mrefu imekuwa ikipoteza haki zake ndani ya muungano kutokana na wabunge kutoka Zanzibar kuwa wazito kutetea maslahi ya Zanzibar ndani ya bunge hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti siyo kama nawageuka wenzangu tumewachagua kwenda kutetea maslahi ya Zanzibar ndani ya muungano lakini wameshindwa kufanya kazi kusimamia haki na kutetea maslahi ya Zanzibar, alisema Mshimba.
Alisema kwamba wakati umefika Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi waruhusiwe kuingia katika Kamati ya pamoja ya kujadili kero za muungano ambayo hukutana chini Mwenyekiti wake Makamu wa Rais wa serikali ya Jamhuri ya Muungano ili kuongeza nguvu za utatuzi wa kero za muungano.
Hata hivyo, haliwataka wananchi wa Zanzibar kutumia vizuri fursa ya kutoa maoni juu ya katiba mpya ya muungano wakati ukifika kwa kuhakikisha wanatoa maoni yao bila hofi na kujiepusha na vitendo vya fujo na jazba ili kuhakikisha haki za Zanzibar zinazingatiwa katika mabadiliko hayo.
Upande wake Mwakilishi wa Viti maalum (CCM) Asha Bakari Makame, alisema kwamba wakati umefika nafasi tano za Wabunge kupitia Baraza la Wawakilishi zifutwe kwa vile wabunge wanaonufaika na nafasi hizo wameshindwa kutetea maslahi ya Zanzibar bungeni.
Naye Mwakilishi wa jimbo la Magomeni (CCM) Salmin Awadhi Salmin, (CCM) na Mjumbe wa kamati Kuu ya chama alisema kwamba wabunge kutoka Zanzibar bado hawajafanyakazi ipasavyo katika kutetea maslahi ya Zanzibar, katika muungano.
Naye mwakilishi wa Jimbo la Mkoani (CUF) Abdalla Mohammed Ali alitaka SMZ kutoa maelezo imekuwa ikinufaika vipi na Taasisi na Mashirika ya Umma ya serikali ya muungano ambayo yanatoa huduma Zanzibar.
CHANZO: NIPASHE
Na Mwinyi Sadallah
23rd June 2012
Sakata la kero za Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, limechukua sura mpya baada ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi (BLW), kulalamika kuwa wabunge kutoka Zanzibar wamekuwa mzigo kutokana na kushindwa kutetea maslahi ya Zanzibar katika mfumo wa muungano huo.
Tamko hilo wamelitoa walipokuwa wakichagia bajeti ya serikali ya mwaka wa fedha 2012/2013 katika Kikao cha Baraza la Wawakilishi, kinachoendelea Chukwani mjini Zanzibar jana.
Akichagia bajeti hiyo Mwakilishi wa Jimbo la Kitope, Makame Mbarouk Mashimba, (CCM), alisema kwamba Zanzibar kwa muda mrefu imekuwa ikipoteza haki zake ndani ya muungano kutokana na wabunge kutoka Zanzibar kuwa wazito kutetea maslahi ya Zanzibar ndani ya bunge hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti siyo kama nawageuka wenzangu tumewachagua kwenda kutetea maslahi ya Zanzibar ndani ya muungano lakini wameshindwa kufanya kazi kusimamia haki na kutetea maslahi ya Zanzibar, alisema Mshimba.
Alisema kwamba wakati umefika Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi waruhusiwe kuingia katika Kamati ya pamoja ya kujadili kero za muungano ambayo hukutana chini Mwenyekiti wake Makamu wa Rais wa serikali ya Jamhuri ya Muungano ili kuongeza nguvu za utatuzi wa kero za muungano.
Hata hivyo, haliwataka wananchi wa Zanzibar kutumia vizuri fursa ya kutoa maoni juu ya katiba mpya ya muungano wakati ukifika kwa kuhakikisha wanatoa maoni yao bila hofi na kujiepusha na vitendo vya fujo na jazba ili kuhakikisha haki za Zanzibar zinazingatiwa katika mabadiliko hayo.
Upande wake Mwakilishi wa Viti maalum (CCM) Asha Bakari Makame, alisema kwamba wakati umefika nafasi tano za Wabunge kupitia Baraza la Wawakilishi zifutwe kwa vile wabunge wanaonufaika na nafasi hizo wameshindwa kutetea maslahi ya Zanzibar bungeni.
Naye Mwakilishi wa jimbo la Magomeni (CCM) Salmin Awadhi Salmin, (CCM) na Mjumbe wa kamati Kuu ya chama alisema kwamba wabunge kutoka Zanzibar bado hawajafanyakazi ipasavyo katika kutetea maslahi ya Zanzibar, katika muungano.
Naye mwakilishi wa Jimbo la Mkoani (CUF) Abdalla Mohammed Ali alitaka SMZ kutoa maelezo imekuwa ikinufaika vipi na Taasisi na Mashirika ya Umma ya serikali ya muungano ambayo yanatoa huduma Zanzibar.
CHANZO: NIPASHE