Wabunge wa CCM wanaoipinga bajeti watakiwa kurudisha kadi za chama

MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Jul 5, 2012
13,171
23,996
Magazeti ya leo yana habari inayosema wabunge wa tiketi ya CCM watakaoipinga bajeti ya mwaka huu wa fedha 2016/2017 wametakiwa na uongozi wa juu wa CCM na serikali kurudisha kadi za uanachama wa CCM ili wakaendeleze adhima yao kupitia tiketi za vyama vingine.

Uongozi wa juu wa CCM na serikali umesema mawazo ya wabunge kwenye mchango wa bajeti na michango mingine yatapokelewa na kufanyiwa kazi na serikali kwa maslahi ya taifa lakini wale wabunge watakaopinga kwa sababu ya maslahi yao binafsi hawawezi kuvumiliwa ndani ya CCM.

Uongozi wa juu wa CCM na serikali umebainisha kuwa hauwezi kuruhusu kuwepo bungeni na kundi lililojiandaa kukwamisha bajeti katika wakati huu ambao serikali imedhamiria kwa dhati kukuza uchumi na kufikisha huduma bora kwa wananchi hasa wa kipato cha chini kwa haraka zaidi.
 
Awamu ya tano inawapa wabunge wa tiketi ya CCM uamuzi kama wanataka kusuka au kunyoa!

Zama za kubembelezana ndani ya chama kwa sasa zimepita na kilichobaki ni uamuzi ulio mikononi mwao ambao waingereza husema, the ball is in CCM MP court.

Haya yameanza kuwadia ndani ya CCM wakati zimebaki siku 33 kabla ya Rais Magufuli kuwa Mwenyekiti wa CCM Taifa. Kwa mwendo huu ndiyo maana kuna baadhi ya watu wana wasi wasi na hatima za maisha yao ndani ya CCM.

Kweli hizi ni zama za HapaKaziTu!
 
Hii ndiyo CCM vituko kila kukicha.
WanaCCM kwa ujumla hawaruhusiwi kukosoa au kushauri serikali.
Hivi nani kawaloga nyie watu?

Kweli wamelogeka hasa mimi sioni tanzania ya viwanda hapa. Labda Tanzania ya viwanda vya wachina na wahindi tunapenda shortcut sana.
Tanzania haiwezi kuwa ya viwanda bila mtanzania yeye mwenye kuwa mdau mkuu.
Watakuja na teknolojia zao alafu wakimaliza kutunyonya wataondokka na teknolojia yao.
Huu ndio ubepari wa karne hii hakuna bepari anayekubali kutoa teknolojia yake kirahisi.
 
--->> kila kitu kiwe NDIO MSEE..!!
•kusema NO,ni jinai /
I don't think kama kweli adhima ya viwanda ITAFIKIWA!!/ labda vya serekali, lakini wafanyabiashara,WAKO NA MASHAKA MAKUBWA SANA./ THEY FAIL TO FORECAST.....HOW TOMORROW GONA BE!/
•KIWANDA KINA UTAFITI WA AWALI / NOT LESS THAN 3 YEARS,VINGI HUWA HAVIPATI FAIDA MPAKA BAADA YA MIAKA 3-7.
SASA ENDAPO SYSTEM NI UNFORECASTED WAT GONNA BE..!!!/ TE TE TE....
 
Mi naona ni kuminywa demokrasia ndani ya Chama. Mtoa mada hayo yalikuwa maamuzi ya Chama baada ya kaukasi ya Chama kukutana Ijumaa iliyopita 17.6.2016. Kwa kifupi hata kurekebisha kile alichopanga Mpango ni kosa..hivyo usisifie sio vyema kabisa mi mwanaCCM sijapenda kbisaa. Hii bajeti ni ngumu sana yataka wanna CCM kuijadili so tuwape kichwa upinzani
 
Daaa inasikitisha sana, hakuna haja ya mtu kupata ujuzi wa kuchambua kama anaambiwa cha kufikiri
Hakuna mtu aliyeambiwa cha kufikiri bali wamepewa nafasi ya kuchagua.

Kupewa nafasi ya kuchagua ni zaidi ya kupewa nafasi ya kuchambua fikra zako na kufanya uamuzi kwa faida ya fikra zako.
 
Back
Top Bottom