Wabunge wa CCM wameshindwa kuweka miundombinu wilaya ya Mufindi licha ya utajiri mkubwa uliopo

MUGASHA THE HERO

JF-Expert Member
Mar 22, 2016
327
204
Hi! jf members

Mimi ni mkazi na mzawa wa wilaya ya Mufindi katika mkoa wa Iringa jimbo la Mufindi kusini. Naandika huu uzi kwa masikitiko makubwa sana.

Kwanza tambueni kwamba jimbo la Mufindi Kusini ni miongono mwa majimbo tajiri sana, tumebalikiwa kuwa na utajiri ufuatao ambao ni fursa kubwa sana kwa wanamufindi wote na watamnzania wote:
  1. Kiwanda kikubwa cha karatasi mgololo (Mufindi Paper Mills/ MPM).
  2. Kampuni kubwa 2 za kilimo cha chai ambazo ni Unilever na Mufindi Tea Company.
  3. Shamba kubwa la miti ya mbao na nguzo za umeme (Sao hill).
  4. Kampuni ya upandaji miti (Green resources).
  5. Kiwanda cha utengenezaji wa nguzo za umeme (Merabu).
  6. Hoteli 1 ya kitalii (Fox Farm).
  7. Viwanda vidogo vidogo.
Vyote hivi vipo katika wilaya ya Mufindi jimbo la Mufindi Kusini. hili ni jimbo ambalo miaka yote lipo chini ya mbunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Jambo linalokera watu wengi wa hili jimbo ni barabara ya kutoka Mafinga mpaka Mtwango kuelekea Mgololo na kutoka Mtwango mpaka Nyololo kuelekea Makambako. Hii barabara ni mbovu kupita kiasi kikubwa, gari zinazobeba karatasi, mbao, nguzo za umeme, majani ya chai zinapita katika hii barabara hii.

Kila siku tunadanganywa kwamba watajenga barabara kwa kiwango cha lami lakini hakuna kitu mpaka leo.

Huduma za kijamii ndio mbovu zaidi lakini jambo la kushangaza ni kwamba wahehe wanaoishi haya maeneo ni wabishi sana haswa pale unapowaambia kuhusu suala la mabadiliko ya kiuongozi.

Haya maeneo hutaona bendela ya ACT au CHADEMA.

Ushauri wangu kwa hii serikaLi ni kwamba wangejenga hata barabara kwa kiwango cha lami lakini sio kutoa ahadi hewa kiasi hiki.

WANAMUFINDI BADILIKENI.

(Nimeambatanisha na baadhi ya picha kutoka Mufindi)
 

Attachments

  • CHAI.8.JPG
    CHAI.8.JPG
    230.8 KB · Views: 151
  • download.jpeg
    download.jpeg
    9.1 KB · Views: 84
  • images.jpeg
    images.jpeg
    6.9 KB · Views: 104
  • IMG_2098.jpg
    IMG_2098.jpg
    21.6 KB · Views: 73
  • sao hill.jpg
    sao hill.jpg
    6.6 KB · Views: 107
  • Tea.jpg
    Tea.jpg
    62.3 KB · Views: 91
Kweli kupo vizuri, labda Magufuli atakuja kuweka lami huko maana ndio obsession yake, ila wabunge wa CCM naona wanafanya mambo kimazoea kwa kuwa wanajua watachaguliwa tu
 
Mkuu ni kweli kabisa Mufindi kulitakiwa kuwa mbali sana ... partly, nimekulia huko bwana ni kama vile nyumbani!! Vingamba mbele kwa mbele!!

Ila swala la miundo mbinu kwa jinsi ya muundo wa serikali ya Tanzania Wabunge mtawalaumu bure tu!! Kama tunataka maendeleo yawafikie haraka watanzania basi sera ya majimbo au Decentralization ndiyo inafaa kufuatwa. Hii ya kusubiri mgao wa Magufuli mtasubiri sana ... maana leo akienda kwa Mzee wa Upako anaahidi barabara, kesho akienda kule nako anaahidi ... hivyo hakuna kinachofanyika kwa mpango wa serikali bali utashi ....!!
 
Mkuu ni kweli kabisa Mufindi kulitakiwa kuwa mbali sana ... partly, nimekulia huko bwana ni kama vile nyumbani!! Vingamba mbele kwa mbele!!

Ila swala la miundo mbinu kwa jinsi ya muundo wa serikali ya Tanzania Wabunge mtawalaumu bure tu!! Kama tunataka maendeleo yawafikie haraka watanzania basi sera ya majimbo au Decentralization ndiyo inafaa kufuatwa. Hii ya kusubiri mgao wa Magufuli mtasubiri sana ... maana leo akienda kwa Mzee wa Upako anaahidi barabara, kesho akienda kule nako anaahidi ... hivyo hakuna kinachofanyika kwa mpango wa serikali bali utashi ....!!
umenena vema mnyalukolo, mufindi kunatoa huruma sana
 
Hi! jf members

Mimi ni mkazi na mzawa wa wilaya ya Mufindi katika mkoa wa Iringa jimbo la Mufindi kusini. Naandika huu uzi kwa masikitiko makubwa sana.

Kwanza tambueni kwamba jimbo la Mufindi Kusini ni miongono mwa majimbo tajiri sana, tumebalikiwa kuwa na utajiri ufuatao ambao ni fursa kubwa sana kwa wanamufindi wote na watamnzania wote:
  1. Kiwanda kikubwa cha karatasi mgololo (Mufindi Paper Mills/ MPM).
  2. Kampuni kubwa 2 za kilimo cha chai ambazo ni Unilever na Mufindi Tea Company.
  3. Shamba kubwa la miti ya mbao na nguzo za umeme (Sao hill).
  4. Kampuni ya upandaji miti (Green resources).
  5. Kiwanda cha utengenezaji wa nguzo za umeme (Merabu).
  6. Hoteli 1 ya kitalii (Fox Farm).
  7. Viwanda vidogo vidogo.
Vyote hivi vipo katika wilaya ya Mufindi jimbo la Mufindi Kusini. hili ni jimbo ambalo miaka yote lipo chini ya mbunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Jambo linalokera watu wengi wa hili jimbo ni barabara ya kutoka Mafinga mpaka Mtwango kuelekea Mgololo na kutoka Mtwango mpaka Nyololo kuelekea Makambako. Hii barabara ni mbovu kupita kiasi kikubwa, gari zinazobeba karatasi, mbao, nguzo za umeme, majani ya chai zinapita katika hii barabara hii.

Kila siku tunadanganywa kwamba watajenga barabara kwa kiwango cha lami lakini hakuna kitu mpaka leo.

Huduma za kijamii ndio mbovu zaidi lakini jambo la kushangaza ni kwamba wahehe wanaoishi haya maeneo ni wabishi sana haswa pale unapowaambia kuhusu suala la mabadiliko ya kiuongozi.

Haya maeneo hutaona bendela ya ACT au CHADEMA.

Ushauri wangu kwa hii serikaLi ni kwamba wangejenga hata barabara kwa kiwango cha lami lakini sio kutoa ahadi hewa kiasi hiki.

WANAMUFINDI BADILIKENI.

(Nimeambatanisha na baadhi ya picha kutoka Mufindi)
Hakuna Mhehe anayeitwa Mugasha wewe ni Muha. Viwanda vyote uluvyovutaja ni private, siyo vya umma. Mbunge atafanya nini zaidi ya kutetea sera ya ubinafsishaji iliyokubalika na Bunge? Huna hoja.
 
Back
Top Bottom