Wabunge wa CCM tunaowaheshimu mko wapi?

Wabunge wa CCM tunaowaheshimu mko wapi?

TPDC inatosha ..hao wazee waliokosa vitalu wakafie mbele, nchi kwanza mengine baadae.
 
Hao mafisafi kwenye issue za KULIIBIA Taifa hili wote huongea lugha moja kwa sauti Moja.

Ukoo hou ni wote ni Tumbili kamwe tusitarajie kuona Nyani.
 
Hatimaye mbunge wa ubunge John Mnyika amefichua siri kubwa iliyopo nyuma ya miswada hii kupitia Itv na Star tv kumbe miswada hii inasukumwa na mataifa makubwa likiwemo marekani kutumia udhaifu wa Jk na mawaziri wake kupitisha miswada mibovu kuwa sheria zitakazowalinda kwa miaka mingi kwani anadai miswada hiyo ikipitishwa kuwa sheria haitaruhusiwa kubadilishwa na bunge lijalo wala na bunge lolote litakalotokea huku pengine wao Us wakiwa washasaini mikataba yenye maslahi makubwa kwao kuwawezesha kukwapua gesi na mafuta huku watz tukiendelea kulalama na tukibaki kuwa walalahoi. mods naomba hii reply muiambatanishe hapo juu kama
itawezekana
Kama anayajua hayo kwa nini hoja zake hizo hakusubiri apinge akiwa ndani ya Bunge ili kuwe na kumbukumbu kwenye Hansard,ili hao Wabunge wa bunge lijalo waseme Mnyika aliwahi kusema hivi na kweli imetokea,vinginevyo hana hoja zaidi ya kutafuta umaarufu nje ya Bunge,hoja hupingwa kwa hoja na siyo kukimbilia ITV
 
Misimamo yetu tutawaeleza kipindi campaign za kuwania ubunge na urais,Kwa sasa tunaomba mpotezee tu..
 
Wabunge wa ccm wote ni wanafiki, hawawezi kuongea wanaogopa kukatwa kwenye kura ya maoni.... Kuna watia nia walikua wanajidai majukwaani majuzi nao naona kimya, watanzania wakiichagua tena ccm shauri yao
 
Mungu Baba mwenye nguvu ulisema sauti ya wanyonge ni sauti yako wewe Mungu wa mbinguni na pia ulisema utatumia vile vinyonge vidhaifu na vilivyodharauliwa kuangusha
VYenye nguvu tunakuomba sasa neno lako litimie.haiwezekani sisi watanzania wanyonge na tuliodhaifu tuendelee kuonewa Na kudharauliwa Na waliopo madarakani.Ona sasa wanataka kushinda uchaguzi Kwa goli la mkono.ona sasa wanataka kupitisha miswada mi3 yenye manufaa Kwao.ona sasa wamewahukumu Na kuwatoa nje Danaiel .Meshack Na Abednego ambao ni watetezi wetu.Mungu sisi kama wanadamu hatuwezi Siku bunge likiendelea tunakusihi. Jitokeze kama Mtu wa nne maana wewe ndiye uliowatia nguvu Daniel.Meshack Na Abednego kukataa kuiabudu Na kuisujudia serikali ya mfalme Nebukardineza Na sanamu yake ya kuchonga.Ulisema wakusanyikapo wawili au watatu wewe Mungu upo Kati Kati Yao humu JF tunaopinga udhalimu naonevu wa ndiyoooo! Ama Siyooooo! Ni Zaidi ya wa3 Wewe Mungu si mwanadamu hata useme uongo wala si Mtu hata ujute ukisema utatenda ama Kwa hakika umeshatenda fanya muujiza kuokoa taifa hili la Tanzania.wanyonge tunapaza sauti nakilio Kwako wewe Mungu in the name of Jesus Christ o Nazarette AMEN" Wakati umeika kila mwana JF aombe Kwa Imani yake Na Bwana Atatenda.Kimwili hatutaweza...


Mpendachapati

Aminaa
 
Maamuzi MAGUMU ya ENL kuhusu miswaada 3 ya mafuta na gesi asilia yako wapi? au slogan ya maamuzi magumu ni geresha tu!
 
Wabunge wa CCM ni janga la kitaifa. Wabunge wa CCM wanafikiri wapo bungeni KUPITISHA sheria na sio KUTUNGA sheria.

Kama unategemea wabunge wa CCM watunge sheria is like trying to milk a stone, which you will never get a milk.
 
ndani ya ccm hakuna kiongozi wala mbunge anayeaminika kamwe. sio wabunge wala wagombea urais waliopo ndani ya bunge kamwe. hao kina makamba,mwigulu,lowasa,wasira na wenzao wote lao ni moja. kama watanzania tunataka mabadiliko ni kwa kuinyima kura ccm. nje ya hapo mabadiliko ni ndoto...

Mawaziri pamoja na wabunge wote wa ccm watupwe huko. Hawana huruma wala nia njema ya kuboresha maisha yetu.
 
Back
Top Bottom