Wabunge wa CCM tunaowaheshimu mko wapi?

Wabunge wa CCM tunaowaheshimu mko wapi?

Mr. Mangi

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2014
Posts
1,512
Reaction score
771
Wabunge wa ccm tunaowaheshimu kwa misimamo yenu kwa taifa hili na wananchi wenu bila kujali itikadi za kivyama mko wapi??
Mh. Olesendeka, Kangi lugola, James Lembeli, Ester bulaya mko wapi??
Kwann mnasubiri mambo yenye maslahi kwa taifa yaendeshwe bila kusema lolote hlf madudu yatakapokuja ibuliwa ndo mjifanye mnasimama kupinga, hapana haiwezekani huo ni unafiki kwani mko wapi???
Tunahitaji kauli zenu juu ya hii miswada iliyoletwa kwa hati za dharura bila kujali ubora wala ubovu wake ila wakati uliopo ktk kuzijadili mko wapi?
Hlf kuna hawa watia nia mabubu bungeni ila majukwaani wanaongea kama chiriku tutawaaminije hamuwez kunyanyua midomo yenu kuikosoa serikal waziwazi bungeni lakini majukwaani viherere, Mwigulu Nchemba hayo madawa hospitalin utayapelekaje ilihali rasilimali za taifa zinaundiwa miswada kuwanufaisha wachache na wewe upo kimya na hicho unachoita "mabadiliko ni sasa" hayo mabadiliko umeshindwaje kuyachangia sasa kwa nafasi yako hlf uweze ukiwa ikulu?
Mh. Lowassa huo umaskini utauondoaje ingawa kwa nafasi yako hujasikika hata mara moja ukitetea maswala yenye maslahi kwa taifa wala kukemea uovu unaotokea bungeni ama serikalini sasa ukiwa raisi utakemeaje?
J. Makamba uchumi wa kati utauletaje ilihali huna muda na maswala nyeti ya taifa lako ulinishangaza sana wakati wa sakata la escrow bungeni ulitulia kimya ila swala lilipoisha ndio ukajitokeza eti wezi wote wa escrow waadhibiwe
Na watia nia wengine wote mliopo bungen mnatuacha njia panda kwa kushindwa kusimama kuonesha umahiri wenu ktk maswala yenye maslahi kwa taifa tuwaelewaje? tunajua wakati mwingine ukimya unasaidia kuficha ujinga sasa tuwaeleweje? Mpo bize ama ndo mnaficha ujinga Membe, Pinda, Ngeleja, Magufuli, migiro, Mpina, Kigwangala n.k
Wito: watia nia wote mliopo bungeni ebhu kwa hizi siku chache zilizobakia onesheni misimamo yenu kwa taifa na wananchi pia wabunge wote kwa ujumla + spika mkumbuke tuna mihili 3 inayojitegemea hivyo fanyeni kazi yenu mliyotumwa na wapiga kura wenu na kazi za serikali muiachie ifanye yake
Tukutane oct 25 ila matumaini yangu yanafifia kwani goli la mkono duh!!....
 
Last edited by a moderator:
Hawajali maslahi ya nchi kwani uongozi watanunua kwa pesa zao. Yaani ni ajabu na kweli mtu hajawahi kuongea bungeni hata siku moja lakini eti nje ya bunge anaungwa mkono sana na wananchi awe rais!!! Halafu na wananchi wanajitokeza kumshangilia, akipata urais anafanya apendalo kwani madaraka kapata kwa hela zake.
 
ndani ya ccm hakuna kiongozi wala mbunge anayeaminika kamwe. sio wabunge wala wagombea urais waliopo ndani ya bunge kamwe. hao kina makamba,mwigulu,lowasa,wasira na wenzao wote lao ni moja. kama watanzania tunataka mabadiliko ni kwa kuinyima kura ccm. nje ya hapo mabadiliko ni ndoto...
 
Kumpata mtu wa kutetea maslahi ya taifa ndani ya ccm, ni sawa na kupata damu kwenye jiwe,...
Umeandika vizur broo, cjui wanapita hapa
 
wanasubiri muswada upite,ili bunge lijalo waanze kujitetea oh sikuwepo wakati wakupita..yani hii inatia hasira sana
 
Mkuu kwenye chama cha wahuni hakuna hata Mbunge moja anayestahili kuheshimiwa, wote ni wahuni na mafisadi siku zote wako kimya pale wanapotaka kufanya uharamia wao dhidi ya nchi yetu.
 
Katika kitu siielewi hadi sasa kuna watu bado wanaamini blah blah za GAMBAZ daaah,,,nackitika sana! Huko ccm hakuna mwenye uchungu na NCH wala wanaNCHI hii tuchague wengine
 
Mleta mada usichokijua ni kua hao unaowaita Wabunge wanaoheshimika kwa taarifa yako wako loyal to CCM zaidi kuliko wanananchi wa kawaida.
 
Hatimaye mbunge wa ubunge John Mnyika amefichua siri kubwa iliyopo nyuma ya miswada hii kupitia Itv na Star tv kumbe miswada hii inasukumwa na mataifa makubwa likiwemo marekani kutumia udhaifu wa Jk na mawaziri wake kupitisha miswada mibovu kuwa sheria zitakazowalinda kwa miaka mingi kwani anadai miswada hiyo ikipitishwa kuwa sheria haitaruhusiwa kubadilishwa na bunge lijalo wala na bunge lolote litakalotokea huku pengine wao Us wakiwa washasaini mikataba yenye maslahi makubwa kwao kuwawezesha kukwapua gesi na mafuta huku watz tukiendelea kulalama na tukibaki kuwa walalahoi. mods naomba hii reply muiambatanishe hapo juu kama itawezekana
 
CCM hakuna mwanamke namuheshimu kama Ester Bulaya, be blessed dada, hao wengine hovyo, wanafiki wachache asilimia kubwa mala..ya, wako pale kupiga vigelegele na kukata viuno kushabikia upuuzi tu, ndio maana wengi ndoa zimewashinda. Pumbavu zao.
 
Hawajali maslahi ya nchi kwani uongozi watanunua kwa pesa zao. Yaani ni ajabu na kweli mtu hajawahi kuongea bungeni hata siku moja lakini eti nje ya bunge anaungwa mkono sana na wananchi awe rais!!! Halafu na wananchi wanajitokeza kumshangilia, akipata urais anafanya apendalo kwani madaraka kapata kwa hela zake.
Hapo ndipo utakapoweza kuthibitisha ni kwa namna gani watanzania tulivyo na akili za kushikiwa.

Hivi inawezekanaje mtia nia mmoja wa Urais aweze kuvuta maelfu kwa maelfu ya 'mashabiki' wake kila anapokwenda na kudai yeye ni mtu anayeweza kuchukua maamuzi magumu, sasa mbona huko bungeni hajachukua maamuzi magumu ya kutofautiana na wabunge wenzake wa CCM, ambao wameamua 'kuzimilikisha' kwa wageni rasilimali zetu za gesi na mafuta tulizojaaliwa na Mwenyezi Mungu?

Mashujaa ambao wataendelea kubaki kwenye vitabu vya historia ya nchi yetu ni hao wabunge machachari wa upinzani akina Kafulila, Tundu Lissu, John Mnyika na wengineo wa Ukawa, ambao wenyewe wamejitolea liwalo na liwe, lakini wao wameamua kutetea hadi dakika ya mwisho rasilimali za Taifa hili zisiporwe na wageni.

Hao akina 'team Lowassa' Kangi Lugora, Esther Bulaya, Deo Filikunjombe, Ole Sendeka na wengineo kutoka chama cha.magamba, huwa wanafanya usanii tu ndani ya hilo jengo la Bunge, kwa kuwa ni kama wamejivisha tu ngozi ya kondoo, lakini ndani yao ni chui hatari!
 
Mzee mamvi mwiz .. anaye jinasibu ni mchukia umaskin...yuko wap ....???
 
Watiania wooote mliopita mikoani kuomba kuungwa mkono na wananchi hapa katika hili la gesi na mafuta ni lazima mseme tuwasikie na tuamini yale mliyosema mkiwa na fomu zenu za kuutaka urais 2015.
Msipofungua midomo kupigania hii miswada ya dharura isipitishwe mtarudi kwa wananchi mtuambie nini?
Hiki kichaka cha kuficha magoli ilimradi refa asione mbinu hii imeshagundulika na nyie msije danganya wananchi. Hilo zogo la miswada hii ndiyo njia pekee ya mtanzania halisi kuonyesha uchungu na hisia zao. hakuna njia nyingine ya wabunge wenye uchungu na taifa hili kuonyesha sauti zao. Enyi watiania sauti zenu zi wapi? Mbona hai sikiliza? Anzeni mabadiliko hapo hapo bungeni sasa. Bunge likiisha bila kusikia sauti zenu kuhusu haya mafuta na gesi mtaweka sura zenu wapi???
kama hata mwongozo haupokelewi nini kifanyike ili haki ifanyike?
Enyi watiania mkitaka kueleweka na wananchi mliowatembelea mikoani fursa hiyooooo inapeperuka.
 
Mungu Baba mwenye nguvu ulisema sauti ya wanyonge ni sauti yako wewe Mungu wa mbinguni na pia ulisema utatumia vile vinyonge vidhaifu na vilivyodharauliwa kuangusha
VYenye nguvu tunakuomba sasa neno lako litimie.haiwezekani sisi watanzania wanyonge na tuliodhaifu tuendelee kuonewa Na kudharauliwa Na waliopo madarakani.Ona sasa wanataka kushinda uchaguzi Kwa goli la mkono.ona sasa wanataka kupitisha miswada mi3 yenye manufaa Kwao.ona sasa wamewahukumu Na kuwatoa nje Danaiel .Meshack Na Abednego ambao ni watetezi wetu.Mungu sisi kama wanadamu hatuwezi Siku bunge likiendelea tunakusihi. Jitokeze kama Mtu wa nne maana wewe ndiye uliowatia nguvu Daniel.Meshack Na Abednego kukataa kuiabudu Na kuisujudia serikali ya mfalme Nebukardineza Na sanamu yake ya kuchonga.Ulisema wakusanyikapo wawili au watatu wewe Mungu upo Kati Kati Yao humu JF tunaopinga udhalimu naonevu wa ndiyoooo! Ama Siyooooo! Ni Zaidi ya wa3 Wewe Mungu si mwanadamu hata useme uongo wala si Mtu hata ujute ukisema utatenda ama Kwa hakika umeshatenda fanya muujiza kuokoa taifa hili la Tanzania.wanyonge tunapaza sauti nakilio Kwako wewe Mungu in the name of Jesus Christ o Nazarette AMEN" Wakati umeika kila mwana JF aombe Kwa Imani yake Na Bwana Atatenda.Kimwili hatutaweza...


Mpendachapati
 
Mungu Baba mwenye nguvu ulisema sauti ya wanyonge ni sauti yako wewe Mungu wa mbinguni na pia ulisema utatumia vile vinyonge vidhaifu na vilivyodharauliwa kuangusha
VYenye nguvu tunakuomba sasa neno lako litimie.haiwezekani sisi watanzania wanyonge na tuliodhaifu tuendelee kuonewa Na kudharauliwa Na waliopo madarakani.Ona sasa wanataka kushinda uchaguzi Kwa goli la mkono.ona sasa wanataka kupitisha miswada mi3 yenye manufaa Kwao.ona sasa wamewahukumu Na kuwatoa nje Danaiel .Meshack Na Abednego ambao ni watetezi wetu.Mungu sisi kama wanadamu hatuwezi Siku bunge likiendelea tunakusihi. Jitokeze kama Mtu wa nne maana wewe ndiye uliowatia nguvu Daniel.Meshack Na Abednego kukataa kuiabudu Na kuisujudia serikali ya mfalme Nebukardineza Na sanamu yake ya kuchonga.Ulisema wakusanyikapo wawili au watatu wewe Mungu upo Kati Kati Yao humu JF tunaopinga udhalimu naonevu wa ndiyoooo! Ama Siyooooo! Ni Zaidi ya wa3 Wewe Mungu si mwanadamu hata useme uongo wala si Mtu hata ujute ukisema utatenda ama Kwa hakika umeshatenda fanya muujiza kuokoa taifa hili la Tanzania.wanyonge tunapaza sauti nakilio Kwako wewe Mungu in the name of Jesus Christ o Nazarette AMEN" Wakati umeika kila mwana JF aombe Kwa Imani yake Na Bwana Atatenda.Kimwili hatutaweza...


Mpendachapati

nashiriki pamoja na ww mkuu AMENI!!!!!!
 
CCM hakuna msafi na wakuaminiwa mtoa uzi usiwanyenyekee hao kuwaomba wapuuze wanajua ina masilahi kwao nao we mtangaza nia yupi apo ataongea ukwel unafiki ndio wanao tu
 
Hatimaye mbunge wa ubunge John Mnyika amefichua siri kubwa iliyopo nyuma ya miswada hii kupitia Itv na Star tv kumbe miswada hii inasukumwa na mataifa makubwa likiwemo marekani kutumia udhaifu wa Jk na mawaziri wake kupitisha miswada mibovu kuwa sheria zitakazowalinda kwa miaka mingi kwani anadai miswada hiyo ikipitishwa kuwa sheria haitaruhusiwa kubadilishwa na bunge lijalo wala na bunge lolote litakalotokea huku pengine wao Us wakiwa washasaini mikataba yenye maslahi makubwa kwao kuwawezesha kukwapua gesi na mafuta huku watz tukiendelea kulalama na tukibaki kuwa walalahoi. mods naomba hii reply muiambatanishe hapo juu kama itawezekana

Mleta uzi umeandika vizuri na wote uliowaulizia waliko ni majembe ya ccm yaliyokosea njia. Wote hao wangeweza kuwasaidia wananchi na taifavhili kama wangekuwa kambi ya upinzani na sio ccm na mfumo wao wa kukumbatia mafisadi na kujineemesha na jasho la wananchi na rasilimali za taifa.Toka hawa viongozi kwenda kuliulia azimio la Arusha kule Zanzibar ndipo tulipoanza kuziona rangi zao halisi. Hao wabunge wa ccm awe Sendeka au Lembeli hawana ubavu wa kulikosoa bunge kwa sasa kwani wanaelewa majina yao hayatapita kwenye mchujo wa wagombea ubunge. Wabunge wa ukawa walioadhibiwa bungeni chini ya udikteta wa ccm tunawaambia karibuni mashujaa wetu. Wananchi wamejionea wenyewe kuwa mlikuwa mnawatete wao na taifa kwa ujumla na hakika watawapeni tuzo na kuwaadhibu hawa wakorofi tarehe 25/10/'15 na serikali yao.Kwa watia nia wao hayupo wa kuliokoa taifa hili akiwa ndani ya chama hicho chenye mfumo huo na hawezi kuingia madarakani na kuubadilisha kwani atakuwa ameteuliwa baada ya makubaliano na maapizano makubwa na wanaoachia madaraka. Anatakiwa achaguliwe asiekuwa na ubia nao ndie mwenye uwezo wa kuufumua mfumo huo wa kukumbatia wezi na mafisadi hata kuogopa kuwapeleka mahakamani eti nchi itatikisika/itayumba. Kuwaambia mafisadi lipeni mnachodaiwa kidogo kidogo na hamtapelekwa mahakamani.Pia huyo raisi ndie atakaelirejesha azimio letu la Arusha lenye miiko ya uongozi. Huyo hajafika kwenu na atateuliwa na ukawa. Wananchi mkiendelea kuchagua viongozi kwa kupewa rushwa ndogo ndogona mkiendelea kuyaogopa mageuzi kilio chenu cha miaka yote kitazidi na taifa litakuwa limefilisika maana hata mbwa na paka majumbani mwenu watauzwa. Nasema tena karibuni mashujaa wetu na sasa fanyeni vikao kwa jamii mkiwaeleza madhara ya mikataba ya dharura mliyokuwa mnaikataa na madhara yake kwa taifa.
 
Back
Top Bottom