] Mkuu hapo nilipobold naona alijisahau na kufikiri yupo kwenye vikao vya chama.Kama tayari anajibu la kila tatizo basi bunge livunjwe tusave hela za walipa kodi
Alizungumza baadhi ya mambo ya msingi lakini akaharibu kwa kuingiza mipasho ya chama chake na kurefusha hotuba kwa mambo yasiyo kuwa na mantiki kabisa!
Jambo jingine ambalo naamini sasa ni tatizo sugu ambalo lazima litafutiwe tiba kabla ya kutuletea matatizo makubwa ni aina ya Wabunge Wanawake wa CCM walioko ktk Bunge letu la JMT na Bunge Maalumu la Katiba. Hawa akina mama kutokana background ya uteuzi wao hawana sifa kabisa kuwemo ktk vyombo hivi muhimu ktk Taifa! Jana wakishangilia kama vile wako Taifa wakiangalia Simba na Yanga! Ni aibu!