Wabunge CCM Waiponda hotuba

Wabunge CCM Waiponda hotuba

Geeky

JF-Expert Member
Joined
Mar 2, 2013
Posts
307
Reaction score
181
Mbunge CCM amponda rais
BAADHI ya wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba wameipinga hotuba ya Rais Kikwete kwa madai kuwa imejaa vitisho na kujibu hotuba ya Mwenyekiti wa Tume ya Katiba Jaji Joseph Warioba.

Mmoja wa wajumbe aliyezungumza na Tanzania Daima Muda mfupi baada ya kumalizika kwa hotiba ya Rais Kikwete katika uzinduzi wa Bunge Maalumu la Katiba, Kangi Lugola, alisema kuwa kauli ya Kikwete ni matokeo ya ukiukwaji na uvunjwaji wa kanuni.

Alisema imesikitisha kuona rais akiwa na sura ya vitisho na kwa wajumbe wa bunge maalumu huku akiwa anaibeza rasimu ya Katiba iliyowasilishwa na Jaji Warioba.

Kwa upande wake mjumbe wa Bunge la Katiba, Maria Sarungi alisema kuwa hotuba ya Rais Kikwete imechukua muda mrefu na kujiondoa katika hotuba na badala yake kuwa kama semina.

Alisema pamoja na mapendekezo yake ya kutaka kuwepo kwa muundo wa serikali mbili, haiwazuii wajumbe wa Bunge Maalumu kujadili na kupendekeza maoni yao ambayo wanaona yanafaa.

source:TanzaniaDaima.
 
Uzushi tu mbona walikuwa wanagonga meza mpaka wakasimama hayo ni maneno yenu ya mtaani mnataka kuwalisha wabunge midomoni
 
hii hotuba ni ya kihistoria, hotuba ya jk . hata nyerere hajawahi kutoa hotuba nzuri kama hii. jk ndio rais bora kupita wote africa
 
hotuba ya rais ilisababisha mbowe apige vigelegele kwa furaha
 
Haikuwa busara, na hapakuwa mahali pake kwa Raisi wa nchi kukosoa rasimu na kutoa maoni yake katika kufungua Bunge la Katiba. Athari za hotuba ya Kikwete ni kuamsha zaidi hisia za Utanganyika na kuwapa hamasa zaidi wananchi kutoikubali katiba itakayowasilishwa kwao kama itakuwa tofauti na matakwa yao kama yalivyoelezwa kwenye rasimu. Raisi amejisahahu kuwa Tanzania sio ccm.
 
Mbunge CCM amponda rais
BAADHI ya wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba wameipinga hotuba ya Rais Kikwete kwa madai kuwa imejaa vitisho na kujibu hotuba ya Mwenyekiti wa Tume ya Katiba Jaji Joseph Warioba.

Mmoja wa wajumbe aliyezungumza na Tanzania Daima Muda mfupi baada ya kumalizika kwa hotiba ya Rais Kikwete katika uzinduzi wa Bunge Maalumu la Katiba, Kangi Lugola, alisema kuwa kauli ya Kikwete ni matokeo ya ukiukwaji na uvunjwaji wa kanuni.

Alisema imesikitisha kuona rais akiwa na sura ya vitisho na kwa wajumbe wa bunge maalumu huku akiwa anaibeza rasimu ya Katiba iliyowasilishwa na Jaji Warioba.

Kwa upande wake mjumbe wa Bunge la Katiba, Maria Sarungi alisema kuwa hotuba ya Rais Kikwete imechukua muda mrefu na kujiondoa katika hotuba na badala yake kuwa kama semina.

Alisema pamoja na mapendekezo yake ya kutaka kuwepo kwa muundo wa serikali mbili, haiwazuii wajumbe wa Bunge Maalumu kujadili na kupendekeza maoni yao ambayo wanaona yanafaa.

source:TanzaniaDaima.

Maria sarungi sio mbunge wa ccm.
Mbunge kangi lugola sio wabunge wa ccm. hata cuf chadema tlp nk wapo wanaopenda serikali mbili.
 
hii hotuba ni ya kihistoria, hotuba ya jk . hata nyerere hajawahi kutoa hotuba nzuri kama hii. jk ndio rais bora kupita wote africa

kweli wewe zero brain unalinganisha mlima na kichuguu....mapenzi yakizidi huleta upofu wa akili
 
Tunataka hotuba mbadala kutoka kwa huyo mnaemwita slaa
 
Ni hotubaa au ni mawazo ya mkuu wa nchi ambaye jana alijiteua kuwa mjumbe wa 202 la wajumbe wateule wa BMK katika kujadili rasimu ya katiba? Vyombo vya vinapotosha ukweli kudai JK kafungua rasmi BMK, Maana kama ni kufungua, naamini aliyefanya kazi hiyo ni Jaji Warioba baada ya hotuba yake, ndipo kazi ya mjadala ikaanza rasmi na mchangiaji wa kwanza alikuwa mkuu wa nchi. Kila mtanzania amemsikia jinsi alivyokuwa makini katika kutoa maoni yake japo mwisho alijisahau na hata mzee 6 alipitiwa kumshitua alipotamka maneno haya: MSIMAMO WAKE NI MUUNDO WA SERIKALI MBILI, NA KATIKA MUDA WAKE WA AKIWA RAIS WA NCHI HATORUHUSU MUUNDO WA SERIKALI TATU! Kwa kauli rais alichangia maoni yake lakini alimaliza kazi yote ya BMLK. J'tatu nitashangaa iwapo bunge hilo litaendelea, swali kama wataendelea watajadili na mwenye nchi kaisha tangaza msimamo wake, maana katetea hata suala la vipindi vya ubunge pasiwepo ukomo, na wabunge watakaokuwa wagonjwa wa muda mrefu waendelee kula bata hata kama wameshindwa kuwawakilisha wananchi.
 
hii hotuba ni ya kihistoria, hotuba ya jk . hata nyerere hajawahi kutoa hotuba nzuri kama hii. jk ndio rais bora kupita wote africa

Ndugu yangu hapo tumepishana rais alikuja kuwasilisha msimamo wa chama au mawazo yake. Tutaitisha maandamano nchi nzima kupinga mawazo yoyote yanayopinga serkali 3 namini hata wana s mtahani hawjapenda hutouba ya bwana
Nchi
 
Hivi chanzo ni gazet la Tanzania Daima?, kama ndivyo go for bid, gazeti gani hilo?, uchuro mtupu, tangu lini gazeti la udaku likaongelea siasa? Tanzania Daima kumbuka liliwahi kutoa taarifa kuwa kwenye uchaguzi wa kata 27 Cdm eti imepata Kata 8. !, kumbe ni tatu tu. Hilo nalo ni gazeti? Mbowe alipeleka Mkya Dubai na kumkatisha safari ya kikazi Marekani halikuandika, Slaa aliiba Mil.140 kwa mtindo wa kuzikopa halikusema, Mwigamba alipigwa hadi matofali kwa amri ya Mbowe gazeti halikuandika, Zitto kafukuzwa na kuvuliwa nyazifa halikuandika. Tanzania Daima ni Gazeti la Mashetani.
 
hii hotuba ni ya kihistoria, hotuba ya jk . hata nyerere hajawahi kutoa hotuba nzuri kama hii. jk ndio rais bora kupita wote africa

Ni kweli ni hotuba ya kihistoria kwa kuwa Rais wa nchi alijisahau kutoa hotuba kama Rais anatoa hotuba kama mchangiaji wa mada ya rasimu ya katiba. Hilo ni la kuweka kwenye kumbukumbu kuwa Rais alijisahau kuwa alialikwa kufungua bunge la katiba badala yake akajivika ujumbe wa baraza la katiba na kuchangia rasimu kama mjumbe na siyo Rais wa nchi. Uzuri wa kitu huamuliwa na mtu mwenyewe. Ni kweli hata sumu ni nzuri kwa muuzaji na mtumiaji anapotaka kutimiza lengo fulani. Ila ni mbaya kwa walengwa wa ile sumu.
 
Ni hotubaa au ni mawazo ya mkuu wa nchi ambaye jana alijiteua kuwa mjumbe wa 202 la wajumbe wateule wa BMK katika kujadili rasimu ya katiba? Vyombo vya vinapotosha ukweli kudai JK kafungua rasmi BMK, Maana kama ni kufungua, naamini aliyefanya kazi hiyo ni Jaji Warioba baada ya hotuba yake, ndipo kazi ya mjadala ikaanza rasmi na mchangiaji wa kwanza alikuwa mkuu wa nchi. Kila mtanzania amemsikia jinsi alivyokuwa makini katika kutoa maoni yake japo mwisho alijisahau na hata mzee 6 alipitiwa kumshitua alipotamka maneno haya: MSIMAMO WAKE NI MUUNDO WA SERIKALI MBILI, NA KATIKA MUDA WAKE WA AKIWA RAIS WA NCHI HATORUHUSU MUUNDO WA SERIKALI TATU! Kwa kauli rais alichangia maoni yake lakini alimaliza kazi yote ya BMLK. J'tatu nitashangaa iwapo bunge hilo litaendelea, swali kama wataendelea watajadili na mwenye nchi kaisha tangaza msimamo wake, maana katetea hata suala la vipindi vya ubunge pasiwepo ukomo, na wabunge watakaokuwa wagonjwa wa muda mrefu waendelee kula bata hata kama wameshindwa kuwawakilisha wananchi.
] Mkuu hapo nilipobold naona alijisahau na kufikiri yupo kwenye vikao vya chama.Kama tayari anajibu la kila tatizo basi bunge livunjwe tusave hela za walipa kodi
 
hii hotuba ni ya kihistoria, hotuba ya jk . hata nyerere hajawahi kutoa hotuba nzuri kama hii. jk ndio rais bora kupita wote africa

Nyerere aliondoka madarakani miaka 29 iliyopita,kwa kusoma posts zako unazo andika hapa JF nina hakika kabisa miaka 29 iliyopita ulikua hujazaliwa!
 
Back
Top Bottom