Waandishi wa habari wauziwa cocaine Dar

EMT

Platinum Member
Jan 13, 2010
14,477
15,325
madawa-1.jpg


DAR ES SALAAM: Vita bado nzito! Hivyo ndivyo unavyoweza kusema kufuatia vitendo vya uuzaji na utumiaji wa mihadarati aina ya bangi, cocaine, heroine na mingine kukithiri mitaani, ingawa serikali iko katika jitihada za dhati kuhakikisha mihadarati hiyo inatoweka nchini.

Hivi karibuni, baada ya vita dhidi ya uuzaji na utumiaji wa madawa ya kulevya kuibuliwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ilisemekana kuwa mihadarati hiyo iliadimika kiasi cha baadhi ya mateja kujikuta wanapata madhara na wengine kutimkia kwenye nyumba za kusaidia waathirika (sober house.)

Ili kupima mafanikio ya mapambano hayo, Kitengo cha Kufichua Maovu cha Global Publishers (OFM) kiliamua kuingia mtaani kuchunguza kama madawa hayo ya kulevya yameadimika au bado yapo.

madawa-1-001.jpg


Waandishi wetu walianza kufanya uchunguzi mitaa ya Sinza, Tandale kwa Mtogole, Mwananyamala, Kinondoni, Temeke na Tandika ambapo baadhi ya maeneo ilionekana bado unga unauzwa ila kwa kujuana na kwingine ulikuwa haupatikani kabisa.

madawa-2.jpg


Akizungumza na Risasi Jumamosi, kijana mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Yakuzo wa Tandale aliyeonekana ni teja alisema: “Daah, mwanangu unga umeadimika ile mbaya, sisi ambao ilikuwa ndo’ starehe yetu tunateseka ila sema nini, kuna sehemu unaweza kuupata lakini siyo kirahisi.”

madawa-3.jpg


…wakikagua kama mzigo upo sawa

Baada ya kuzungumza na watu katika maeneo mbalimbali na kubaini bado unga upo mitaani, waandishi walifika mitaa ya Tandika maeneo ya Dabo Kibini, sehemu ya kuoshea magari ambapo walitonywa kuwa, unga unauzwa waziwazi.

madawa-4.jpg


Mmoja wa waandishi alimfuata kijana mmoja na kumuuliza wapi anaweza kupata kilevi hicho ambapo alioneshwa mhusika. Kijana huyo aliyeonekana kuwa makini na biashara yake alipoulizwa kama anaweza kumpatia mwandishi cocaine kete 4 alikubali na kudai bei ya kiasi hicho ni shilingi 10,000.

madawa-5.jpg


Baada ya mwandishi kupewa unga huo, alikwenda kusimama kwa mbali na kushuhudia vijana wengi wakifika eneo hilo na kununua bidhaa hiyo bila wasiwasi.

Ushauri watolewa

Salum Jeti, mkazi wa Magomeni aliyedai ana watoto wake wawili mateja alikuwa na hili la kuishauri serikali: “Hawa waliotangaza vita dhidi ya madawa ya kulevya wasidili na mateja, kama kweli wanataka kutatua tatizo wazuie unga kuingia nchini kisha watafute njia nzuri za kuwasaidia hawa watumiaji. Wakidili na hawa watu wadogowadogo, unga utakuwa unaingizwa, utauzwa kwa siri na vijana wetu wataendelea kuumia.”

madawa-7.jpg


Risasi Jumamosi lilijaribu kumtafuta Kamishna wa Operesheni wa Mamlaka ya Kupambana na Kudhibiti Madawa ya Kulevya nchini, Mihayo Msekhela ili kuzungumzia vita hiyo lakini alipopatikana kwa njia ya simu alieleza kuwa, yupo kwenye kikao hivyo atafutwe Jumanne ijayo.

Chanzo: https://globalpublishers.co.tz/125198-2/
 
Kwa jinsi hao OFM walivyobaini maeneo ya wauza unga nashindwa kuelewa, inakuaje vyombo vyetu vya usalama vimeshindwa njia kama hiyo ya kiwango cha chini sana kiuchunguzi kubaini hawa watu? Iko namna.. hii vita ni pana lakini wanaoipanua ni wenye mamlaka. Hawa watu wanawezekana kudhibitiwa serikali iamue sasa.
 
Kwa jinsi hao OFM walivyobaini maeneo ya wauza unga nashindwa kuelewa, inakuaje vyombo vyetu vya usalama vimeshindwa njia kama hiyo ya kiwango cha chini sana kiuchunguzi kubaini hawa watu? Iko namna.. hii vita ni pana lakini wanaoipanua ni wenye mamlaka. Hawa watu wanawezekana kudhibitiwa serikali iamue sasa.
Serikali haijaamua kudhibiti madawa....
Mkuu wa mkoa alikuwa anatafuta kiki atoke vipi.... Sasa kiki imemgeukia yeye anaanza kulialia na kutangatanga.....
Muda utasema
 
Kwa jinsi hao OFM walivyobaini maeneo ya wauza unga nashindwa kuelewa, inakuaje vyombo vyetu vya usalama vimeshindwa njia kama hiyo ya kiwango cha chini sana kiuchunguzi kubaini hawa watu?

Jukumu la ulinzi na usalama ni jukumu la kila mtanzaniahata wewe.Ukiona mahali ripoti
 
Inatisha sana pale ambapo biashara haramu zinakuwa ni tamaduni za jamii ya watu fulani.
Kuzimaliza itakuhitaji upige Vita dhidi ya serikali, wafanya hiyo biashara na raia wa kawaida ambao kwa namna moja au nyingine Uchumi wao halali unakuwa umeunganishwa na Uchumi haramu.

Sawa na leo mtu aseme anaanzisha Vita dhidi ya biashara haramu kwenye nchi kama Italy au Mexico. (Haiwezekani hata kidogo)
Lazima tu Uchumi utaanguka kwasababu Legal Economy (Uchumi Halali) umeunganishwa na Uchumi haramu (Underground Economy). Nchi kama Mexico biashara haramu ya Madawa ya Kulevya ndiyo imejenga mashule, barabara, viwanda na kuajiri vijana wengi haramu: mpaka walipofika sasa hata serikali haiwezi kupigana na wauza unga bila kujiumiza yenyewe sanjali na Uchumi wa nchi.

Tanzania yetu sasa ndiyo majanga matupu.
Uchumi haramu umekuwa unaendesha nchi kwa miaka miongo zaidi ya mitatu.
Ukwepaji kodi na utakatishaji wa pesa , Ujangili, Rushwa, Biashara ya binadamu, Madawa ya kulevya, Wizi wa madini , Uuzaji wa Silaha za moto n.k

Bahati mbaya sana wanaojihusisha na hizi kazi haramu ndiyo:
1. Wawekezaji wakubwa hapa nchini hivyo basi wao ndiyo watoa ajira wakuu.
2. Wanasiasa wetu. (wengine wameshika hadi nyadhifa kubwa kabisa na wengine ndiyo wapinzani wetu)
3. Wauzaji na wasambazaji wakubwa wa bidhaa muhimu kama Sukari, Mafuta, Nguo, Vipodozi, Nafaka n.k
4. Wamiliki wakubwa wa vyombo vya habari vyenye ushawishi hapa nchini.(Magazeti, Redio na Televisheni)
5. Wachangiaji wakubwa wa shughuli za Vyama vikuu vya siasa hapa nchini.
6. Wachangiaji wazuri wa shughuli za kijamii. (Wanajenga Makanisa, Misikiti, Zahanati, na Shule)

Ukiisha yaangalia haya basi utajua kwamba huwezi kuwashinda hawa mabwana bila kuumiza maisha ya Mtanzania wa kawaida. Hata leo angefufuka Hayati Mwalimu Julius Nyerere angeshindwa kuongoza nchi ambayo imejenga Uchumi ulio imara kupitia biashara haramu. Watanzania wenyewe wangempindua hata mwezi haufiki, kama tu miaka ya 80 wafanya baishara haramu walikuwa ni wachache lakini walifanya watakavyo Usitegeme leo ambapo wana magenge makubwa utaweza kuwashinda kirahisi.


I.M.F wametoa taarifa yao kwamba Uchumi harama (Underground Economy) kwa nchi zinazoendelea ni kama Asilimia 25% hadi 40% ya G.D.P za nchi hizo. Sasa fikiria Tanzania yetu ni moja ya nchi inayosifika kuwa mlango mkuu wa biashara haramu hapa duniani, sehemu kubwa ya Uchumi wa nchi ni baishara haramu. Sidhani kama serikali inaweza kushinda hii vita kirahisi hasa ukiangalia jinsi ilivyogawanyika kioungozi na kiutendaji kuanzia kwenye Ngazi ya Kitaifa hadi Ngazi ya Chama.

Ili nchi kama hii ifanikiwe na mabo yarudi kama kawaida inabidi nchi iongozwe na kiongozi ambaye ni Mafia Oriented ambaye ataendana na huu mfumo wa Kimafia. Mfano Mzuri ni Kenya na Nigeria, ambako Uchumi unakuwa kwa kasi lakini hauko mikononi mwa serikali bali Magenge ya Wahuni ambao ndiyo wenye kushikilia kila kona ya Uchumi wa nchi.


Good bye Afrika.

NB: Ni hat

EMT
 
Kwa jinsi hao OFM walivyobaini maeneo ya wauza unga nashindwa kuelewa, inakuaje vyombo vyetu vya usalama vimeshindwa njia kama hiyo ya kiwango cha chini sana kiuchunguzi kubaini hawa watu? Iko namna.. hii vita ni pana lakini wanaoipanua ni wenye mamlaka. Hawa watu wanawezekana kudhibitiwa serikali iamue sasa.
Hii vita ni longolongo tu. Ndo ishaisha hivooo
 
Cocaine bei yake ipo juu sana sidhani ina watumiaji wengi

Ungesema heroine hapo ningekuelewa

Hizo ni heroine na siyo cocaine ,cocaine utazipata kwenye ma-casino hizi za mitaani ni heroine ,nani atazimudu cocaine hawa mateja wa mtaani wote wanatumia heroine na hawawezi kumudu cocaine ,cocaine ni za ma-don wenye pesa na ukiwa kapuku ukitumia cocaine lazima ufilisike ,cocaine huwezi kupata kama heroine sijui elf 3 au 4 kwa kete ,
 
Mkuu hii biashara ukitafakari sana, madon wa kuu ni viongozi wa nchi, sasa hapo ndiyo unapoona ugumu wake. Kumbuka Noriega, Carlos aliungana na Castrol family. Huku Afrika hali ni hiyo hiyo, viongozi wa miaka ya .com wamejiingiza kabisa katika biashara hii.
 
yaani pamoja na ukamatwaji wa watu unavoendelea eti muuza unga akubali picha ipigwe wakati anauza? hao OFM wanacheza na akili za watu
 
Back
Top Bottom