EMT
Platinum Member
- Jan 13, 2010
- 14,477
- 15,356
Baada ya JF kunizingua, niliamua kwenda zangu Mali kutembea nikakutana na peoples power wa huko wakiwa wanajivinjari Ikulu baada ya kumpa kichapo Rais wao hadi kuzirai. Mamia ya waandamanaji hao walimshambulia Rais Traoure wakipinga mkataba ulioafikiwa na Tume ya kiuchumi ya nchi za magharibi mwa Afrika, ECOWAS, ambapo Traoure ataendelea kutawala kwa hadi mwaka mmoja badala ya siku 40 pekee zilizokubaliwa miezi miwili iliyopita.
Wakuu wa serikali nchini Mali wamesema kuwa Rais huyo wa Mpito amepelekwa eneo salama baada ya kupigwa hadi kuzirai na mamia ya waandamanaji. Wanajeshi waliwaruhusu baadhi ya waandamanji kuingia katika ikulu ya rais ingawa bwana Traore hakuwepo wakati huo.
Shambulio hilo limewashtua wanadiplomasia waliokuwa wakifanya kila juhudi kurejesha amani na utangamano nchini humo. Muda wa kuongoza aliopewa Traore ulitarajiwa kukamilika Jumatatu. Lakini viongozi wa nchi za Magharibi mwa Afrika, waliafikia mkataba na kiongozi wa mapinduzi Kapteni Amadou Sanogo kwamba Bw Traore asalie mamlakani ili aweze kuongoza harakati za uchaguzi na kumaliza harakati za waasi wa Tuareg.
Mkataba huo pia ulijumuisha mpango wa kukubalia Sanogo atajwe kama kiongozi wa zamani alipwe mshahara wa rais na apewe nyumba ya kifahari. Mapinduzi hayo pamoja na harakati za waasi kuteka Kaskazini mwa Mali, yamesababisha maelfu ya watu kutoroka makwao. Mashirika ya misaada wanasema wana wasiwasi mkubwa kuhusu hali ya kibinadamu nchini Mali nchi ambayo pia inakumbwa na baa la njaa.