Egwugu
JF-Expert Member
- Mar 16, 2011
- 17,558
- 8,551
Ngoja niseme alafu mwisho ntamalizia kwa swali dogo,kuna mradi wa usambazaji umeme vijijini chini ya Rea ila hatuoni wafanyakazi wa Tanesco wakikatwa pesa kufanikisha hili,tunaona kuna chanjo ya rubela na surua imeanza jana ila hakuna mtumishi yeyote wa afya anayekatwa kuchangia chanjo hiyo,aidha tumeona upimaji wa ardhi ukiendelea nchi nzima ila hatujaona watumishi wa ardhi wakibanwa ili kuchangia mpango huo,sasa nauliza tu,imetokea sheria hipi na lini ikaonekana ujenzi wa maabara shuleni eti waalimu wachangie mradi tena kwa mabavu kiasi hicho ama ndo enzi za ukoloni na forms of taxations inarudi upya kwa kuanzia kwenu,ama mna mapesa mengi sana waalimu?