Waafrika tuache ushamba!

Waafrika tuache ushamba!

zamani utotoni tulikuwa tunatengeneza magari ya bati yaani toys tunatengeneza wenyewe dah ilikuwa fun kweli au kuendesha taili la gari au mchezo wa goroli na mchezo wa betry za gari kwikwikwi
siku hizi watoto wanataka ps1 sjui na mambo mengine
 
zamani utotoni tulikuwa tunatengeneza magari ya bati yaani toys tunatengeneza wenyewe dah ilikuwa fun kweli au kuendesha taili la gari au mchezo wa goroli na mchezo wa betry za gari kwikwikwi
siku hizi watoto wanataka ps1 sjui na mambo mengine

sisi tulikua tunabuni toys wenyewe kwa kutumia udongo eg. gari,Super man, etc ila now mambo yote england toys + XBox
 
Hope weekend yenu ipo poa,
Jamani, sielewi kwanini waafrika hatujikubali. Na sielewi lini tutaamka na kuanza kujielewa. Nime observe tatizo hili tumerithishwa na tunawarithisha vizazi vyetu e.g pale tunapo nunulia mabinti zetu midoli ya kizungu. Tayari unapanda mbegu fulani kichwani mwao kuwa uzungu ndio deal. Na sidhani hata siku moja kama ataona thamani ya kuwa mwafrika. As a result akikuwa atajichubua, ata taka kufanana na mzungu kwa kila hali.
Nafikiri tujitahidi kujithamini tulivyo

sikubaliani na wewe, watu wananunua midoli kulingana na availability tu, ingekuwapo midoli mingi myeusi watu wangenunua tu. mtoto wangu wa kike hapendi midoli yenye kufanana na watu, anapenda midoli ya cartoon characters, sijaona anajichukia na kupenda kuwa kama teddy!!!!! kinachowaharibu watoto wa kike ni mama zao, ndugu wanaowazunguka na marafiki, kama mama yake anajichubua na yeye ataona kumbe kujichubua ndiyo deal, otherwise watoto wanaelewa utofauti wa rangi kwamba watu tuko tofauti hata miongoni mwa waafrica kuna walio brown sana na wenye lighter skin, kuna albino...watoto hawana neno na rangi ya ngozi wala hawana muda wa kuwaza ubaguzi wa namna yoyote kulinga na race!
 
Utumwa wa akili ndio utumwa mbaya zaidi.Kwenda na wakati kwa mweusi ni kuiga kila afanyalo mzungu!
rafudhi;lugha,mavazi;kufanya mapenzi;elimu;majina;sanaa;imani;ulaji chakula;na namana ya kuishi.
Mzungu anatumia akili ktkt kila nyanj,Mwafrika anatumia sifa au visingizio ktkt kila nyanja
 
nakumbuka hiyo mkuu tena udongo huo ulikua unachimbbwa sehemu maalum pia kutengeneza nyumba za mabox... kasaloo
 
Last edited by a moderator:
nakumbuka hiyo mkuu tena udongo huo ulikua unachimbbwa sehemu maalum pia kutengeneza nyumba za mabox... kasaloo

watoto wa siku hizi hata hawataki kushuhurisha vichwa vyao.. wanataka zawadi za midoli ya newyork tu.. ukimletea kinyago kilichochongwa na mtanganyika atalia sana tena hatolala siku hiyo kwa kukiogopa...wazungu tuwaache jama they are so creative..
 
sasa unampa mtoto likinyago bayyaaa watu wameunganikana mala sura ziko kumi kwenye kichwa kimoja unadhani atapenda, hapa ishu kubwa ni cc wenyewe kuwa creative nakutengeneza bidhaa zinazopendwa zaidi hapo ndipo tulipo pishana na wazungu yani yani wao wanafanya research kabla ya kufanya jambo hivyo hucheza na mind za watu nini wanapenda kwa wakati gani nandomana unakuta hata mavazi tunavaa sana ya nje kwasababu nayenyewe wanaproduse zaidi kwa wingi kipindi vazi limekubalika kama kisketi cha diamond
 
Mbona wazungu hununua vinyago weusi na kwenda navyo kwa watoto wao
 
Wazungu huwezi wapotezea,mbona unapanda magari yao,ndege zao,computer zao . sasa shida iko api.watu hufikilia ni weupe uliowapa chati,hapana ni akili. Waafrica tungekua juu yao kitecgnologia,nao pia wangetuona black is everything
 
.. genuineme kuna michezo fulani ambayo sisi tulipitia watoto wa siku hizi huoni wakifanya zaidi kucheza game
playstation na mambo mengine
utotoni ilikua tunaunda vitu au kuwinda ndege na manati mchezo ya goroli dah.....ah tulikuwa tunaenda kuvuaaa hapo mitaaa ya my fair wakati huo kuliwa na mabwawa tu syo sahvi wamejenga majumba dah ilikuwa fun sana
 
Last edited by a moderator:
Michezo hiyo ya asili binadamu wote hupitia,ata wao walipitia mpaka walipoendelea sana, sasa watoto wanapewa michezo formal zaidi kujenga uwezo wa fikra na ubunifu,kama maisha ya watu wazima wa kale na sasa yanatofauti.Basi ata watoto wa sasa na wa kale watakua na tofauti kwenye michezo yao,ila si mbaya kuitumia pia île ya asili. Usione manati ukafikiri ni bure,ni sayansi,ule mpira kuvutika ni modulus Of elasticity
 
Michezo hiyo ya asili binadamu wote hupitia,ata wao walipitia mpaka walipoendelea sana, sasa watoto wanapewa michezo formal zaidi kujenga uwezo wa fikra na ubunifu,kama maisha ya watu wazima wa kale na sasa yanatofauti.Basi ata watoto wa sasa na wa kale watakua na tofauti kwenye michezo yao,ila si mbaya kuitumia pia île ya asili. Usione manati ukafikiri ni bure,ni sayansi,ule mpira kuvutika ni modulus Of elasticity

tena mimi nlikuwa na shabaa sana ya manati nkitoka uswahilini huku tuna kwenda banda mayai osterbay kuwinda mara tume fukuzwa na midoggy maana watoto wa kishua walikuwa wakituona lazima watusakizie mijibwa kwikwikwi ilikuwa burudani sana
 
Uzungu huu ndio unao zidi kuaribu vijana wa taifa letu. Zamani kitendo cha mwanaume kusuka na kuvaa hereni ilikuwa ni aibu. Lakini cheki vijana wa leo wanavyokuwa. Ukija kwenye vyakula ndio usiseme, tumeacha vyakula vyetu vya asili ambavyo vilikua vinatukinga na maradhi, badala yake tunakunywa misoda, masoseji chipsi mayai na mengineyo. Matokeo yake ndio hayo makansa, presha na sukari kila kona. Wenzetu ni wajanja sana, wanakula hivyo sawa, ila kila baada ya mlo unakuta wanameza dawa za kuwapa virutubisho. Sie wapi?

Ni issue kubwa sana lakini inachangiwa na vitu viwili kwanza umekosekana ubunifu wa ma-chef wetu kuja na mapishi mapya ya asili kuongeza varities and option (ingawa sioni ubaya kula vyakula vya kigeni kama hakuna athari za kiafya). Tatizo wao vyao wanaweka ma chemical mengi na substitute nyingi kwenye kuchanganya sanasana kwenye hayo masosage na wenzetu the cheaper the product the lower the quality, lakini vipo hivyo hivyo vilivyo na viwango na organic bei sasa ndio kasheshe.

Pili ruhusa ya vipindi vya kigeni iliyopitiliza, tumekazana sana na kuachia kuwa influenced na other global cultures hivi tunadhani hizi tamthilia za nchi za magharibi tunazoangalia zaidi ya za kwetu zinatuaffect vipi sisi? Ukienda nchi kama ufaransa radio tu airuhusiwi kupiga zaidi ya % fulani ya miziki yenye lugha za kigeni, ukienda uingereza ukiongea tu na accent za region zingine wanakushangaa.

Ndio maana utakuta ata watu especially public figures ambao ni private schooled ingawa huko walikopitia wanabanwa sana na kutumia formal english bado wanaongea na lafudhi za kwao, sisi ukiwasikia vijana wetu unakuta mtu anaongea with american accent kwa mzungu anaweza kushangaa why dont you just pronounce it right with standard english (lafudhi inayotumiwa na watangazaji wa kimataifa), lakini unakuta mtu anaona aitoshi lazima aiwekee na accent za kigeni unaona ulimbukeni unapoanzia na influence za media.

As days go we dilute our culture, attitudes and identity, inabidi kuwe na ubunifu maana ya hizi alternatives zinatokana na uwepo mchache wa sanaa za kutosha kila sinema ni mapenzi tu au kulogana na mengineo yenye kuaddress ill behaviours in negative perspective to me that is just encouragement quite the opposite of shaping the right thinking (unajiuliza hivi akuna other social issues to be addressed),watu awawezi imba kuhusu mambo mengine zaidi ya mimi kuonewa wivu au kuimba mapenzi, halafu tunashangaa uzinzi uliokithiri. Media ni weapon kubwa sana hila kwa sasa inasaidia western societies to spread their cultures na kuifanya kazi yao rahisi sana kwenye ku-negotiate na sisi in their perspectives.
 
Ni issue kubwa sana lakini inachangiwa na vitu viwili kwanza umekosekana ubunifu wa ma-chef wetu kuja na mapishi mapya ya asili kuongeza varities and option (ingawa sioni ubaya kula vyakula vya kigeni kama hakuna athari za kiafya). Tatizo wao vyao wanaweka ma chemical mengi na substitute nyingi kwenye kuchanganya sanasana kwenye hayo masosage na wenzetu the cheaper the product the lower the quality, lakini vipo hivyo hivyo vilivyo na viwango na organic bei sasa ndio kasheshe.

Pili ruhusa ya vipindi vya kigeni iliyopitiliza, tumekazana sana na kuachia kuwa influenced na other global cultures hivi tunadhani hizi tamthilia za nchi za magharibi tunazoangalia zaidi ya za kwetu zinatuaffect vipi sisi? Ukienda nchi kama ufaransa radio tu airuhusiwi kupiga zaidi ya % fulani ya miziki yenye lugha za kigeni, ukienda uingereza ukiongea tu na accent za region zingine wanakushangaa.

Ndio maana utakuta ata watu especially public figures ambao ni private schooled ingawa huko walikopitia wanabanwa sana na kutumia formal english bado wanaongea na lafudhi za kwao, sisi ukiwasikia vijana wetu unakuta mtu anaongea with american accent kwa mzungu anaweza kushangaa why dont you just pronounce it right with standard english (lafudhi inayotumiwa na watangazaji wa kimataifa), lakini unakuta mtu anaona aitoshi lazima aiwekee na accent za kigeni unaona ulimbukeni unapoanzia na influence za media.

As days go we dilute our culture, attitudes and identity, inabidi kuwe na ubunifu maana ya hizi alternatives zinatokana na uwepo mchache wa sanaa za kutosha kila sinema ni mapenzi tu au kulogana na mengineo yenye kuaddress ill behaviours in negative perspective to me that is just encouragement quite the opposite of shaping the right thinking (unajiuliza hivi akuna other social issues to be addressed),watu awawezi imba kuhusu mambo mengine zaidi ya mimi kuonewa wivu au kuimba mapenzi, halafu tunashangaa uzinzi uliokithiri. Media ni weapon kubwa sana hila kwa sasa inasaidia western societies to spread their cultures na kuifanya kazi yao rahisi sana kwenye ku-negotiate na sisi in their perspectives.
Unayo yaongea ni kweli ndugu yangu
 
Huo hatuiti ushamba kiongozi ni utumwa wa kifikra na si ushamba ambao unatutesa mpk sasa waafrika!
 
Back
Top Bottom