Ngongo
JF-Expert Member
- Sep 20, 2008
- 18,923
- 31,162
Jana usiku muda wa saa 2:45 nikiwa narejea nyumbani maeneo ya Chini ya Mti karibu na lile kanisa la Nabii wa kiNigeria nilikumbana na msururu wa maandamano makubwa ya vijana wa kiArusha wakipelekwa jando [kuondoa suna bila ganzi nadumisha mila ile wengine wameshindwa].
Wakuu najua JF wapo wanajamvi wenye kujua mila na tamaduni za kiMaasai/kiArusha chonde chonde naomba watumwagie mauzoefu ya hili zoezi zima tunajua vijana wanatahiriwa tunajua pia yapo mambo mengi ambayo hatuyajui eg ujasiri,kupewa majina ya marika ie Makaa,Seuri,Landizi na nk watueleze hayo majina yanapatinaje je taratibu za kuzuia maambukizi ya UKIMWI zinazingatiwa.....Je zoezi la kukeketa kina Dada wa kiArusha/Maasai wameacha limeachwa/limesitishwa siku hizi.
Nawapenda sana waArusha/waMaasai wanadumisha mila katika mazingira ya dunia ya utandawazi.
Wakuu najua JF wapo wanajamvi wenye kujua mila na tamaduni za kiMaasai/kiArusha chonde chonde naomba watumwagie mauzoefu ya hili zoezi zima tunajua vijana wanatahiriwa tunajua pia yapo mambo mengi ambayo hatuyajui eg ujasiri,kupewa majina ya marika ie Makaa,Seuri,Landizi na nk watueleze hayo majina yanapatinaje je taratibu za kuzuia maambukizi ya UKIMWI zinazingatiwa.....Je zoezi la kukeketa kina Dada wa kiArusha/Maasai wameacha limeachwa/limesitishwa siku hizi.
Nawapenda sana waArusha/waMaasai wanadumisha mila katika mazingira ya dunia ya utandawazi.