SERIKALI imetoa waraka unaovielekeza vyuo vikuu vyote nchini, kuchelewa kuanza muhula wa masomo kwa mwezi mmoja, ili kupisha uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu.
Kwa mujibu wa waraka huo, badala ya kuanza Oktoba kama ilivyozoeleka, muhula kwa vyuo vikuu vyote katika mwaka huu, utaanza juma la kwanza la Novemba, baada ya kumalizika uchaguzi huo wa madiwani, wabunge na rais.
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Shukuru Kawambwa, alisema vyuo hivyo vitafunguliwa kati ya Novemba 4 na 5.
Hata hivyo alisema hatua hiyo haitokani na uchaguzi na kwamba inatokana na mabadiliko yanayotarajiwa kufanywa na serikali katika utoaji wa mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu nchini.
"Fedha zinazohitajika kwa ajili ya mikopo ya wanafunzi mwaka huu ni nyingi sana, zinafikia Sh250 bilioni ni pesa nyingi, kwa hiyo tunaandaa utaratibu mpya ambao tunatarajia utakuwa umekamilika ifikapo Novemba 3,"alisema Waziri.
@@[0:[0:1:CHANZO TAFADHARI]]