Vyombo vya kiusalama vijitathmini

Vyombo vya kiusalama vijitathmini

malimangapi

JF-Expert Member
Joined
May 12, 2013
Posts
238
Reaction score
48
Taasisi hizi zikiwemo Polisi, na Usalama wa Taifa zimekuwa hazifanyi kazi zao kukidhi mahitaji ya KATIBA ya Nchi wala matakwa ya Uanzishwaji wa vyombo hivi bali kufuata utashi wa Raisi aliye Madarakani.

Maana yake ni kwamba vyombo hivi havitumikii Taifa bali Mtu. Mfano ni wa huyu aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai Ndugu Sabaya, Ujambazi na Uharamia wake ulikuwa unajulikana wakati wote wa utawala wa Hayati John Pombe Magufuli, lakini hakuna hatua zozote zilizochukuliwa kisheria dhidi yake.

Bila shaka kama kungekuwa hakuna mabadiliko ya Kiutawala Leo Sabaya angekuwa bado ni Mkuu wa Wilaya ya Hai
 
Ishu sio vyombo vya usalama ishu ni aliyekuwa raisi ndio alikuwa akilinda haya madudu

Magu ndio alikuwa akiyafuga haya mafirauni kwa maslahi anayoyajua yeye , huyu sabaya mambo aliyokuwa anafanya magu alikuwa anayajua tu
 
issue sio vyombo ni mfumo. vyombo ni watendaji tu, katiba na sheria zetu zinampa mamlaka yote mtu mmoja. huku chini hakuna anaweza kuhoji ni kufuata maagizo tu
 
Ishu sio vyombo vya usalama ishu ni aliyekuwa raisi ndio alikuwa akilinda haya madudu

Magu ndio alikuwa akiyafuga haya mafirauni kwa maslahi anayoyajua yeye , huyu sabaya mambo aliyokuwa anafanya magu alikuwa anayajua tu
Vyombo hivyo vingefanya mpango basi wa kumuondoa huyo mkingia watu vifua maana ilikuwa excess sasa..au ndo walichofanya?

Katiba yetu hii ni mbovu..haiwezekani tuongozwe na akili na ubabe wa mtu mmoja ambaye anajua hakuna mtu yeyote anayeweza kumgusa.
 
MTU ANAJIWEKEA KINGA UNATEGEMEA NINI?

MSISIMAMIZI WA KUTUNGA SHERIA ANAPEWA KINGA.

JAJI MKUU ANAPEWA KINGA NA ALIYEMTEUA.KWANINI ASIAGIZWE KESI HII FINGA NA HUYO MUACHIE

NINI KIFANYIKE
 
ni mpuuzi pekee anayeamini hiki kinachoendelea hakijachorwa.

watu wawanawaza hatua 500 mbele jamani.
 
...
Bila shaka kama kungekuwa hakuna mabadiliko ya Kiutawala Leo Sabaya angekuwa bado ni Mkuu wa Wilaya ya Hai
... pengine angeshakula promotion kwa nafasi ya juu zaidi pengine mtendaji mkuu wa mojawapo wa vyombo hivyo. Kumrundikia mtu mmoja madaraka yote ya nchi ni hatari sana!
 
ni mpuuzi pekee anayeamini hiki kinachoendelea hakijachorwa.

watu wawanawaza hatua 500 mbele jamani.
Kamsalimie jambazi mwenzio kule kisongo

Kwa mwenendo wa Sabaya tangu alipokuwa UV CCM akijifanya usalama wa taifa mpaka alipokamatwa ni majambazi kama yeye ndio watahitaji ushahidi kuthibitisha uovu wake!
 
Kamsalimie jambazi mwenzio kule kisongo

Kwa mwenendo wa Sabaya tangu alipokuwa UV CCM akijifanya usalama wa taifa mpaka alipokamatwa ni majambazi kama yeye ndio watahitaji ushahidi kuthibitisha uovu wake!

wewe endela kuamini sabaya "alijifanya"usalama wa taifa.
 
Back
Top Bottom