Vyama vya Wafanyakazi vimekuwa "paralyzed" na utawala wa awamu hii?

Salary Slip

Platinum Member
Apr 3, 2012
49,324
152,136
Moja ya jukumu la vyama vya wafanyakazi ni kutetea maslahi na luhakikisha haki za wafanyakazi zinalindwa kwa mujibu wa sheria za utumishi wa umma.

Hata hivyo,tangu awamu hii imeingia madarakani,kuna mambo yamefanyika ambayo kwa namna moja au nyingine bila shaka yatakuwa yameathiri watumishi wa umma.

Hivi sasa tunaona kila mtu amekuwa na mamlaka ya kuagiza watumishi wa umma wasimamishwe kazi kupisha uchunguzi jambo ambalo hata mh.Lissu alihoji ndani ya Bunge lakini vyama hivi viko kimya!

Kwa mfano leo hii nimeona kupitia taarifa ya habari ya Star tv ya saa 4 asubuhi,Mkuu wa Mkoa wa Morogoro,bwana Stephen Kabwe akiagiza watumishi kadha wa Halmashauri wasimamishwe kazi katika mkutano wa hadhara uliohusu maswala ya wakulima na wafugaji.

Pia, tumeshuhudia Mkuu wa Mkoa wa Dar-es-salaam,bwana Paul Makonda akiagiza watendaji wa Halmashauri za Jiji la Dar-es-salaam wasaini mikataba maalumu kuhusiana na swala la kudhibiti watumishi hewa.Nia ni nzuri lakini utaratibu ule ulikuwa halali?

Hiyo ni mifano michache tu miongoni mwa mingi tulioshuhudia.Pamoja na nia njema ambayo inaweza kuwepo, swali ni je,taratibu zinafuatwa?Ni kweli Wakuu wa Mikoa wana madaraka hayo?

Kinachonishangaza ni ukimya wa vyama vya wafanyakazi,vyama ambayo watumishi hukatwa mishahara hayo ili kuviendesha.Je,ni kweli vyama hivi havijaona hata jambo moja la kukemea?Vyama hivi vinasubiri watu wafukuzwe kazi ndio vijitokeze hadharani?

Mwaka huu serikali imepunguza PAYE kufikia single digit.Ni jamba jema na la kupongeza.Lakini mwaka huu kuna nyongeza ya mshahara iliyotangazwa rasimi na waziri husika?Vyma vya wafanyakazi vimehoji juu ya jambo hili?

Kuna taarifa zisizo rasimi kuwa kuna mpango wa kupunguza mishahara ya baadhi ya wafanyakazi ili kuleta uwiano.Je,jambo hili ni sahihi?Kama ni kuleta uwiano,kwanini iwe ni kwa kupunguza na si kuongeza mishahara ya watumishi wanaolipwa mishahara midogi?Sheria za utumishi zinaruhusu kupunguza mshahara wa mtu?Vyama hivi vya wafanyakazi vimewahi, hata kuhoji jambo hili?Je,vinasubiri migogoro itokee kati ya mwajiri na mtumishi ndio vianze kujitokeza kwenye vyombo vya habari na matamko ya hapa na pale?

Kuna hili swala la kuunganisha baadhi ya Idara na Taasisi za Umma zinazofanya kazi zinazofafana. Je,vyama hivi vimeshirikishwa?Vinajua nini kinaendelea kuhusu zoezi hili?

Wahusika timizeni wajibu wenu kama kazi imewashinda muwapishe wanaoweza.
 
Wanaanzaje kwanza kwa mfano?

Hapa RC:kada CCM
Pale DC:kada CCM
Huku DED:kada CCM
Kule DAS:kada CCM.

Wote hao lengo lao moja. Kumfurahisha aliyewateua...
 
Katika makosa ambayo wafanyakazi wa Tanzania mliyafanya ni kudharau vyama vya wafanyakazi na kuweka watu wachovu kuviongoza huku kila mwezi mnakatwa mishahara kwa ajili ya hivyo vyama. Viongozi wa vyama vya wafanyakazi ni wajasiriatumbo walioingia kwa ajili ya kupata viposho na sio kuongoza. Sasa ndio mnaisoma namba kwa kudharau labor movement. Hakuna wa kuwatetea, ngoja muishi kama mashetani kama sisi wafanyabiashara
 
Kwa stahili hii ya utendaji wa vyama vya wafanyakazi kuna haja ya kujitoa kwa kushindwa kututetea na kutusemea,mfano watu waliosimamishwa kazi wako tu home hawapewi mashitaka yao.Vyama hivi vitapoteza hadhi yake.
Tunapaswa kuwa na damu mpya ya kuviendesha,pia wajue wanachama hawahitaji kuendelezwa kiuchumi tu.Yaani Chama kuwa na benki,majengo ya kukodisha.Pia wanapaswa kutetewa haki zao.
 
Mkuu kuchagua makada wa chama kuwa wakurugenz huku hawana sifa kwa sheria za kaz hakuna anaye kemea wote wameufyata kwa.... ..dk. uchwar.a.
 
hivi mfano chama kama CWT ..kama ni gazeti hata kufungia mandazi hakifai...
 
Kuhusu payee kupunguzwa hadi single digit ni kweli tu kwa wale wenye mshahara kati ya shs 170,000 hadi shs 360,000.wengine hakuna mabadiliko ya kiwango hivyo wanaendelea kukatwa kati ya asilimia 25 na 30.maumivu ni mazito.sichochei jamani nimeandika tu!
 
Kuhusu vyama vya wafanyakazi hama kit zaidi wanajali matumbo yao.kwa mfano Kuhusu fao la kujitoa kwe mifuko ya jamii wameshindwa hata kuwaambia wafanyakazi ukweli ni up, mimi nilitegemea baada ya kutokea sintofahamu kwenye mitandao ya kijamii wangelitolea ufafanuzi kwa wanachama wao lakini wako kimya,maana yake wanashirikiana na serikali kutaka kutuhujumu.inaniuma sana kila mwezi nakatwa elfu arobaini halafu hawajui wajibu wao kazi yao kulipana posho tu,wanachojua ni maandamano ya may mosi pale uwanja wa Taifa shame on you Mkoba.
 
Hivi kweli kuna mpango wa kupunguza mishahara ya baadhi ya wafanyakazi?!

Kama mpango huo upo bora utekelezwa haraka ili wafanyakazi tutie akili vichwani mwetu kuwachagua akina Mgaya na Mkoba kuwa viongozi wetu.
 
Nakumbuka ATC ilitokea retrenchment shida ilikuwa kwenye malipo.ATC wakatoa offer yao wafanyakazi hawakuridhika tulikubaliana viongozi wetu wa COTWU wasisaini mpaka tujiridhishe sheria mtu ukipunguzwa kazi sheria inasema, Jamaa wakatuzunguka wakapiga hela kwenye management wakaisaini hata wanasheria wao usiwaamini bora mtumie lawyer wa kwako mwenyewe,huwa wanakuzunguka wanapiga hela kwa mwajiri baada ya hapo hawatokei mahakamani.
 
Serikali isiyotaka kukosolewa utafanyaje? Acha wanyamaze tu PPF wamefuta fao la kuijtoa ila vyama vipo kimyaaaa, tuisome namba.
 
Back
Top Bottom