Vyama vya Upinzani, chukueni ushauri huu

herzegovina

JF-Expert Member
Oct 28, 2015
3,129
4,712
Kwa lugha inayoeleweka kabisa ni kuwa nchi hii haikuundwa kuja kuwa nchi ya vyama vingi. Ilibidi tuigize kama tuna vyama vingi ili kuepuka "kibano" tulichokuwa tunakabiliana nacho kipindi hicho kutoka kwa mabeberu. Hata vyama vingi vilipoanzishwa Mali nyingi sana ziliekezwa kwa Chama Tawala.

Leo miaka 28, baada ya mfumo wa vyama vingi bado wapinzani wanaonekana kama maadui wa nchi. Wanaonewa, wananyanyaswa, wanafanyiwa kila hila. Sababu ni moja tu, "mifumo yote" inaamini na ina uhakika kuwa hawawezi kushika dola.

Vyombo vya habari havirushi mikutano, Polisi wanawatisha na kuwakamata, huko NEC ndio usiseme maana hata aibu hawana. Mnajua kwanini wanawafanyia yote haya? Ni kwa kuwa wanajua hamuwezi kuwa mabosi wao.

Katika hali ya usawa wa kidemokrasia, wagombea wowote wale wangekuwa wanaheshimika. Polisi asingemu-harass mgombea ubunge kwa kuwa anajua kuna uwezekano wa mgombea yule kuwa Waziri wa mambo ya ndani. Vyombo vingewaheshimu wagombea Urais kwa kuwa yoyote Kati Yao anaweza kuwa Amiri Jeshi Mkuu n.k

Je, mfanye nini? Kwa kuwa imeshaonekana dhahiri kuwa hamthaminiwi na hamuwezi kushika dola hata iweje bali mnatumika tu kuuonyesha ulimwengu kuwa Tanzania ni nchi ya vyama vingi, basi ni vyema baada ya uchaguzi huu mkafanya MAAMUZI magumu. Either ni wapinzani wote kwa pamoja kwenda kufuta vyama vyao kwa msajili (kwa njia yoyote ile) au wapinzani wote kwa pamoja kujiunga CCM ili vyama vya upinzani vikose hata kiongozi mmoja kuanzia ngazi ya taifa hadi mtaa hivyo vifutike automatically.

Kwa kufanya hivi CCM itabaki peke yake hivyo basi ile "hadaa" kwa ulimwengu kuwa Tanzania ni nchi ya vyama vingi itakuwa imefikia mwisho. Nadhani yanayoendelea yanamulikwa hivyo kama kuna "kibano" kingine watatupa basi na iwe hivyo ili tutakaporudi kwenye suala la vyama vingi basi sasa iwe ni vyama vingi katika uhalisia.

Wapinzani mnatumika bila nyinyi wenyewe kujijua. Ifike mwisho.
 
  • Thanks
Reactions: ZNM
Yaani huu ushauri ni wa hovyo Sana. Unafikiri hata huko upinzani walikochukua dola hawakufanyiwa hayo?? kila kitu huwa kina mwisho wake, na CCM mwaka huu ni mwaka wao wa mwisho kuwa madarakani tutaichinja CCM hivyo hivyo itakavyokuwa sikubaliani na ushauri wa kufuta vyama au kujisalimisha CCM au umetumwa?
 
Kwa tume ipi mjomba? ?? Tusijitekenye na kucheka wenyewe. DKT MAHERA ni kada kindakindaki.

Hivi ya Jecha hayajawashtua tu? ?
Yaani huu ushauri ni wa hovyo Sana ..unafikiri hata huko upinzani walikochukua dola hawakufanyiwa hayo?? kila kitu huwa kina mwisho wake, na ccm mwaka huu ni mwaka wao wa mwisho kuwa madarakani ..tutaichinja ccm hivyo hivyo itakavyokuwa ..sikubaliani na ushauri wa kufuta vyama au kujisalimisha ccm ..au umetumwa??
 
Mkuu hata wakifuta wote,CCM itatengeneza tawi na kuliita upinzani na kisha ngoma ikaendelea!

Tutabanana hapa hapa mpaka kieleweke!Kadri watu wanavyozidi kuelimika na wazee wale wa enzi Nyerere kuisha,ndivyo upinzani unavyozidi kupata nguvu!
 
Kuna hoja kwenye bandiko lako ila imejificha.

Kwa kifupi wapinzani wapiganie TUME HURU YA UCHAGUZI pamoja na KATIBA MPYA.

Hayo mambo mawili yakipatikana, basi yote uliyoyaeleza yatakuwa sawa
 
Mkuu hata wakifuta wote,CCM itatengeneza tawi na kuliita upinzani na kisha ngoma ikaendelea!
Tutabanana hapa hapa mpaka kieleweke!Kadri watu wanavyozidi kuelimika na wazee wale wa enzi Nyerere kuisha, ndivyo upinzani unavyozidi kupata nguvu!
Suala la mpaka kieleweke ndio halipo. Hivi unadhani NEC na majeshi wanapata wapi jeuri ya kuyafanya haya?? Wanajua suala hilo halipo. Jecha alipofuta uchaguzi nini kilitokea? Hakuna

Dawa ni kurudi chama kimoja tu na ikipigwa kura ya maoni tunakataa tunasema tunataka chama kimoja tu labda zikiwekwa "conditionalities" zingine ndipo tutaheshimiana.
 
Ambayo CCM haiwezi kuruhusu. Ni lazima hili suala liwe kwenye maagano na jumuiya za kimataifa baada ya "kibano" kama ilivyokuwa kwa ubinafsishaji na vyama vingi.
Kuna hoja kwenye bandiko lako ila imejificha.

Kwa kifupi wapinzani wapiganie TUME HURU YA UCHAGUZI pamoja na KATIBA MPYA.

Hayo mambo mawili yakipatikana, basi yote uliyoyaeleza yatakuwa sawa
 
Mkuu hata wakifuta wote,CCM itatengeneza tawi na kuliita upinzani na kisha ngoma ikaendelea!
Tutabanana hapa hapa mpaka kieleweke!Kadri watu wanavyozidi kuelimika na wazee wale wa enzi Nyerere kuisha,ndivyo upinzani unavyozidi kupata nguvu!
Hata sasa hivi hayo yote ni matawi ya ccm na iko wazi, mfumo wa vyama vingi ulikataliwa na ccm 80%, kwa kuwa lilikuwa takwa la mabeberu ikabidi kuanzisha matawi, hata Urusi upinzani ni dhaifu kwa kuwa ni matawi.

Kusema kweli kwa Afrika upinzani ni mwanzo wa migogoro isiyoisha, nchi nyingi zimeanguka uchumi wake kwa sababu ya huu ujinga. Wakati Tanzania ikiingia uchumi wa kati nchi kama Algeria imeshuka na kuwa miongoni mwa nchi maskini mwaka huu.Hiyo ni baada ya kuingia kwenye mageuzi ya kuangusha serikali kwa maandamano eti demokrasia.

Upinzani Tanzania utaendelea kuwa tawi la ccm kwa usalama na ustawi wa nchi.
 
Kumbuka upinzani humo humo kuna matawi ya CCM kama TLP, NRA, CCK nk hayo ni matawi ya CCM sasa unategemea watafutwa?
 
Ambayo CCM haiwezi kuruhusu. Ni lazima hili suala liwe kwenye maagano na jumuiya za kimataifa baada ya "kibano" kama ilivyokuwa kwa ubinafsishaji na vyama vingi.
Ubinafsishaji ulikuja na tukaupokea matokeo yake tumeyaona viwanda vilivyokuwepo sasa havipo.Kiwanda cha Urafiki na Mwatex vilikuwa vinatishia soko la bidhaa za ulaya leo Mwanza hakuna kiwanda cha nguo, Musoma hakuna kiwanda cha nguo, urafiki imekufa. Mabeberu yanatuchezesha sindimba bila kujitambua. Kwa ccm YA SASA TARATIBU TUNAANZA KURUDI TULIKOTOKA, KUANZIA JANUARY TUNAANZA KUZALISHA VIATU KWA KAMPUNI YA JESHI 100% STATE OWNED. Ni bora turudi tulikotoka vya mabeberu vinaturudisha nyuma kwa manufaa yao
 
Kiuhalisia CCM ilishatolewa kwenye sanduku la kura miaka mingi iliopita.

Sasa hivi inapumua kwa nguvu ya vyombo vya dola na tume ya uchaguzi.

Imebaki nguvu ndogo ya kuwasukuma nje.
 
Ubinafsishaji ulikuja na tukaupokea matokeo yake tumeyaona viwanda vilivyokuwepo sasa havipo.Kiwanda cha Urafiki na Mwatex vilikuwa vinatishia soko la bidhaa za Ulaya leo Mwanza hakuna kiwanda cha nguo, Musoma hakuna kiwanda cha nguo, urafiki imekufa. Mabeberu yanatuchezesha sindimba bila kujitambua. Kwa ccm YA SASA TARATIBU TUNAANZA KURUDI TULIKOTOKA, KUANZIA JANUARY TUNAANZA KUZALISHA VIATU KWA KAMPUNI YA JESHI 100% STATE OWNED. Ni bora turudi tulikotoka vya mabeberu vinaturudisha nyuma kwa manufaa yao
Ujamaa haujawahi kuwa na mwisho mzuri. Udhaifu katika kusimamia ubinafsishaji usifanye suala zima la ubinafsishaji kuwa ni UNYONYAJI.
 
Kiuhalisia CCM ilishatolewa kwenye sanduku la kura miaka mingi iliopita.

Sasa hivi inapumua kwa nguvu ya vyombo vya dola na tume ya uchaguzi.

Imebaki nguvu ndogo ya kuwasukuma nje.
Kwa mtazamo wangu, Uzi huu umechangiwa na great thinkers kweli kweli ila wewe naona umeweka mzaha!
 
Hata sasa hivi hayo yote ni matawi ya ccm na iko wazi, mfumo wa vyama vingi ulikataliwa na ccm 80%, kwa kuwa lilikuwa takwa la mabeberu ikabidi kuanzisha matawi, hata Urusi upinzani ni dhaifu kwa kuwa ni matawi.

Kusema kweli kwa Afrika upinzani ni mwanzo wa migogoro isiyoisha, nchi nyingi zimeanguka uchumi wake kwa sababu ya huu ujinga. Wakati Tanzania ikiingia uchumi wa kati nchi kama Algeria imeshuka na kuwa miongoni mwa nchi maskini mwaka huu.Hiyo ni baada ya kuingia kwenye mageuzi ya kuangusha serikali kwa maandamano eti demokrasia.

Upinzani Tanzania utaendelea kuwa tawi la ccm kwa usalama na ustawi wa nchi.
Hapana,hapo umepotosha!Upinzani tanzania ungekuwa tawi la CCM haya mambo ya kubambikiziana kesi, kuwekana mahabusu,kutekana,kupigana risasi nk yasingekuwepo kwa wapinzani nchini!

Upinzani nchini unachukuliwa kama uasi na watawala,mpaka tunatishana kutoletewa maendeleo kama watu watachagua wabunge na madiwani wa upinzani!

Hapo unasemaje upinzani ni tawi la CCM?Au mimi ndio sijakuelewa?

Tatizo linaloikumba Africa umelikwepa! Tamaa, viburi na ulevi wa madaraka kwa watawala ndio unasababisha mfumo wa demokrasia kushindwa kufanya kazi!Tatizo sio mfumo wa demokrasia kuwa mbaya ila tatizo lipo kwa watawala!
 
Hapana,hapo umepotosha!Upinzani tanzania ungekuwa tawi la CCM haya mambo ya kubambikiziana kesi,kuwekana mahabusu,kutekana,kupigana risasi nk yasingekuwepo kwa wapinzani nchini!

Upinzani nchini unachukuliwa kama uasi na watawala,mpaka tunatishana kutoletewa maendeleo kama watu watachagua wabunge na madiwani wa upinzani!

Hapo unasemaje upinzani ni tawi la CCM?Au mimi ndio sijakuelewa?

Tatizo linaloikumba Africa umelikwepa!Tamaa, viburi na ulevi wa madaraka kwa watawala ndio unasababisha mfumo wa demokrasia kushindwa kufanya kazi! Tatizo sio mfumo wa demokrasia kuwa mbaya ila tatizo lipo kwa watawala!
Ni kweli pia hata ukiangalia suala la wapinzani kununuliwa au kutishiwa ili wajiunge CCM.

Dawa ni wote wajiunge CCM tu kuwe na chama kimoja uone vifungu kwenye "VIGEZO na MASHARTI" vitakavyotubana.
 
Ni kweli pia hata ukiangalia suala la wapinzani kununuliwa au kutishiwa ili wajiunge CCM.

Dawa ni wote wajiunge CCM tu kuwe na chama kimoja uone vifungu kwenye "VIGEZO na MASHARTI" vitakavyotubana.
Tutafika tu,tusikate tamaa mapema!
 
Ubinafsishaji ulikuja na tukaupokea matokeo yake tumeyaona viwanda vilivyokuwepo sasa havipo.Kiwanda cha Urafiki na Mwatex vilikuwa vinatishia soko la bidhaa za ulaya leo Mwanza hakuna kiwanda cha nguo, Musoma hakuna kiwanda cha nguo, urafiki imekufa. Mabeberu yanatuchezesha sindimba bila kujitambua. Kwa ccm YA SASA TARATIBU TUNAANZA KURUDI TULIKOTOKA, KUANZIA JANUARY TUNAANZA KUZALISHA VIATU KWA KAMPUNI YA JESHI 100% STATE OWNED. Ni bora turudi tulikotoka vya mabeberu vinaturudisha nyuma kwa manufaa yao
Dogo, usipotoshe.. hivo viwanda ulivyotaja wakati vinabinafsishwa vilisha kufa kitambo. Vilikuwepo tu ilimradi kwa ruzuku na gharama kubwa za walipa kodi.
 
Isitoshe tulaumiwe sisi kwa kushindwa kusimamia ubinafsishaji na sio tuulaumu ubinafsishaji.
Dogo, usipotoshe.. hivo viwanda ulivyotaja wakati vinabinafsishwa vilisha kufa kitambo. Vilikuwepo tu ilimradi kwa ruzuku na gharama kubwa za walipa kodi
 
Back
Top Bottom