Vodacom Tanzania ni wezi

Vodacom Tanzania ni wezi

Wewe umeona kwenye bando tu, kwenye miamala ndo usiseme laki mbili unakatwa 5,300 yaani M-Pesa ni tatizo wameongeza sana, mamlaka zifatilie hili jambo wanaumiza wnanchi na makato.

Tumie mabenki mobile money ni gharama kubwa sana watu hamjui tu ukipiga hesabu unatumia hela nyingi sana kwa mwaka kuliko ata kulipia ada ya chuo kikuu kwa mwaka chukua mda kidogo tu alafu uangalie
 
Nimenunua kifurushi cha mwezi mzima kuanzi tarehe 14 February, nilipata GB kama sijakosea 19GB, mpaka tarahe 29 asubuhi bado nilikuwa na salio la GB 16.3.

Kifurushi changu kinaishia tarehe 15 March.
Jana saa kumi na mbili jioni napata sms hii kutoka VODA “Your TSH35000 bundle balance has finished. Enjoy freedom to call or browse in a bundle. Dial *149*01#>Pinduapindua”

Nimewapigia voda mara tatu sasa wananiambia tatizo lako linashughulikiwa tutakujibu baada ya masaa 24.

Hivi VODA Tanzania wanatupa hizi huduma kwa hisani au sisi wateja tunazilipia na ni lazima tupate huduma tuliyolipia kwa wakati?

Nilinunua kifurushi number 4

View attachment 1373354

Salio kama linavyoonekana kwenye app yao wenyewe lakini wamenikatia internet. Kuna hatua yoyote ya kesheria naweza kuchukua? TCRA wanaweza kusaidia chochote hapa?

View attachment 1373358
Hapo wanasema 10GB muda wote na 17GB kuanzia saa sita usiku mpaka 1.59 asubuhi.. Huo sio usanii?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Voda mpenzi wangu badilika acha tabia ya kuwaibia wateja,huoni aibu unazomewa kila kona mwizi mkubwa wewe badilika na ukiri hadharani ulinde heshima yako ya kuwa mtandao bora.
Vodacom ni wezi sana, mwezi uliopita nilikua na uhuru package sh,20,000 kwa bahati mbaya nikawasha data upande wa voda japo sikua na bando la voda jamaa wakaanza kutumia salio langu ambalo halikua linahusiana na bando kabisa nikawapigia cm.wajaniambia siku hizi hata usipojiunga bando kama unasalio kwenye mpesa au uhuru package zinatafunwa zote ghafla nikataka kuunga bando nikakuta nina tshs,0.00 ndo nikatambua huu mtandao ni wezi balaa ila tcra walisha wapa worning sijui kwanini wanaendelea

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimekua mtumiaji wa vodacom kifurushi cha KASI kwa zaidi ya miaka 2 mfululizo (Tsh 50,000) kwa mwezi, hadi mwanzoni mwa mwaka huu nilivyoona wameanza kuniibia bundle, imebidi ninunue router ya TIGO and now I am enjoying enough data at affordable cost ingawa sometime huwa inakatakata but it is worth kuliko Vodacom ya sasa.
 
Voda zamani.

Siku hizi sijui kimewakuta nini!
 
Back
Top Bottom