Watanzania tusitazamie unafuu katika wizi huu kwani huu ni wizi unaofadhiliwa na serikali yenyewe hii hii ya CCM.
Hao mnaowaita TCRA si lolote ni wala rushwa wakubwa, ------------ kitambo na majambazi hayo yaliyoiweka serikali mifukoni na sasa TCRA wanabaki kuwalamba Vodacom na Tigo makalio ili angalau wagange njaa.
Haiingii kabisa akilini nchi nzima kuwapigia kelele hawa wezi wa Vodacom na Tigo lakini kuwe kimya kama hakuna kitu kinachoendelea.
Hata mimi nimewahi kuibiwa zaidi ya mara kumi na makampuni haya. Kwanza ukiacha salio, asubuhi hulikuti, mwenyewe niliamua kuwahama baada ya kuacha salio la 5,000 na asubuhi kukuta eti salio linasoma Sh. 670/=!
Niliwapigia hawakuniitikia na badala yake kompyuta yao ilinielekeza nikubali kukatwa Sh. 100 ili niunganishwe "haraka" nikiafiki nibonyeze namba 1, baada ya kufanya hivyo niliambiwa " hatuwezi kukuhudumia kwa sasa jaribu baadae" na hela walishakata! Baadae wananambia huna salio la huduma hii! kucheki salio kuna Sh. 40!
Watanzania tuamke; hizi mia mia wanazotuibia ni fedha nyingi sana. Fikiria Voda au Tigo wana kila mmoja wateja milioni Saba, na kati ya wateja hao kila siku milioni nne wanaibiwa Sh. 300/=, makusanyo ya wizi huo yatakuwa zaidi ya Sh. Bilioni moja na laki mbili kwa siku moja na pengine dakika moja! Fedha kiasi hicho inatosha hata kumhonga Rais achilia mbali hawa makuwadi wa TCRA.
Tatizo ni kwamba bado watu wanaendelea kuwapigia kura majambazi hawa katika sare za kijani! Tuna akili kweli sisi?