Vodacom kweli ni wezi sana comfirmed

Vodacom kweli ni wezi sana comfirmed

gedo

JF-Expert Member
Joined
Nov 16, 2012
Posts
314
Reaction score
53
Nimeweka vocha ya elfu2 kucheki Salio mda huo huo nikakuta 1,664 kweli hili kampuni jizi....jihadharini nalo.
 
Zaidi ya wezi, ukitaka kuwajua tumia huduma ya NMB mobile wanakata hadi unalia, mim hadi sasa nishagombana na mtu kumbe ametuma hela toka alhamis mimi sijui kwasababu kwangu haijafika, tunawapigia wanasema eti mtandao mbovu ndio mana hela haionekani kwenye ACC huo si wizi siku tatu zote hela ionekane kwenye acc?
 
hii kampuni basi muda si mrefu nitahamia baba lao kila nikikopa 900 nanunua kifurushi cha 500 kabla hakijaisha ukiangalia salio unakuta umebakiwa na 370 sasa tumechoka na utapeli huu imenitokea kama mara 7 sasa ukiwapigia wanakwambia ulijiunga na huduma flan ambayo hata hujawai kuisikia huu ni wizi kama kama majambazi yanayovunja nyumba za watu inatakiwa upigwe vita kali tutaibiwa mpaka lini
 
Kwanamna hii wakituibia watz mil2 370 tsh wanashingapi?lazima nitawahama ...
 
Nimeweka vocha ya elfu2 kucheki Salio mda huo huo nikakuta 1,664 kweli hili kampuni jizi....jihadharini nalo.

mkuu usimpe mtu namba zako hovyo, utalizwa, kuna watu wanajifanya custome care wakipata namba zako utalia
 
Nipo makini sana...usijar mwanajf..
 
Hivi tcra hawapo au ---------- ili kufumbia macho wizi huu. wk iliyopita nilitumia mpesa kwa namba mbili tofauti za airtel. hadi sasa pesa haikufika ilikokuwa inaenda na wala haijarejeshwa kwenye acct yangu hata baada ya siku saba kuisha. Huu ni wizi na haukubaliki
 
Voda awafai,nliingiza pesa kwny ac ya mpesa,kibandan anasema kaingiza kwangu haikufika mpaka leo hii,ni mwez sasa,nishawahama siku nyingi,baba lao ndo habar ya mjini
 
PoLe mkuu miMi nililizwa kama ww nikaWajulisha ila kama ni wezi sugu
 
Mimi sisemi ni wezi bali hawatendi haki.Mwezi nov 2013 niliweka tshs.12000 nikasafiri nikaacha simu nyumbani niliporudi nikakuta salio tsh.3650.Nilipokwenda kuuliza ikawa dadana hadi leo. Hata promotion (michezo) yao zawadi zao hutolewa kiajabu kufuata mikoa. kwani kunatuliocheza tangu ianze miaka zaidi ya kumi lakini tunachangia wengine wapate. Hapa inaonyesha wazi kwao Haki na wajibu hamna.
 
...sio wezi per see, nilichogundua wengi wetu tunatumia simu za smart (smart phone) bila ya kujua jinsi ya kui "utilise" hasa kwenye suala zima la "net" mtandao.....iko hivi..smart phone zenye 3G ikiwa activated, kama haujajiunga na bundle then ukaweka credit, "LAZMA UKATWE" maana simu ina automatic updates, so ukicheki salio unakuta linaisha kila baada ya muda, nlishawahi kulalamika sana miaka ya nyuma, lakini baadaye nikaja jua tatizo, so ukitaka usikatwe, wewe jiunge na bundle, au deactivate 3G, utumie 2G, ikikushinda kabisa deactivate data...
...so the problem is within ours, (mashkolo mageni)
 
voda wezi wamekubuhu yaani hii namba ingekuwa haipo kwa watu wa muhimu ningeacha voda majizi sana
 
Hivi tcra hawapo au ---------- ili kufumbia macho wizi huu. wk iliyopita nilitumia mpesa kwa namba mbili tofauti za airtel. hadi sasa pesa haikufika ilikokuwa inaenda na wala haijarejeshwa kwenye acct yangu hata baada ya siku saba kuisha. Huu ni wizi na haukubaliki

Watanzania tusitazamie unafuu katika wizi huu kwani huu ni wizi unaofadhiliwa na serikali yenyewe hii hii ya CCM.
Hao mnaowaita TCRA si lolote ni wala rushwa wakubwa, ------------ kitambo na majambazi hayo yaliyoiweka serikali mifukoni na sasa TCRA wanabaki kuwalamba Vodacom na Tigo makalio ili angalau wagange njaa.
Haiingii kabisa akilini nchi nzima kuwapigia kelele hawa wezi wa Vodacom na Tigo lakini kuwe kimya kama hakuna kitu kinachoendelea.
Hata mimi nimewahi kuibiwa zaidi ya mara kumi na makampuni haya. Kwanza ukiacha salio, asubuhi hulikuti, mwenyewe niliamua kuwahama baada ya kuacha salio la 5,000 na asubuhi kukuta eti salio linasoma Sh. 670/=!
Niliwapigia hawakuniitikia na badala yake kompyuta yao ilinielekeza nikubali kukatwa Sh. 100 ili niunganishwe "haraka" nikiafiki nibonyeze namba 1, baada ya kufanya hivyo niliambiwa " hatuwezi kukuhudumia kwa sasa jaribu baadae" na hela walishakata! Baadae wananambia huna salio la huduma hii! kucheki salio kuna Sh. 40!
Watanzania tuamke; hizi mia mia wanazotuibia ni fedha nyingi sana. Fikiria Voda au Tigo wana kila mmoja wateja milioni Saba, na kati ya wateja hao kila siku milioni nne wanaibiwa Sh. 300/=, makusanyo ya wizi huo yatakuwa zaidi ya Sh. Bilioni moja na laki mbili kwa siku moja na pengine dakika moja! Fedha kiasi hicho inatosha hata kumhonga Rais achilia mbali hawa makuwadi wa TCRA.
Tatizo ni kwamba bado watu wanaendelea kuwapigia kura majambazi hawa katika sare za kijani! Tuna akili kweli sisi?
 
Mwisho wa siku nyote mtahamia zantel tu, makaburu na wazungu siku zote wezi. Ukiwauliza watakwambia lugha zao za kubabaisha tu, hakuna cha kushangaa hapo. Nendeni zantel kule serikali ya zanzibar ina share so wako makini na uhuni wa aina yoyote kwa wananachi wake.
 
...sio wezi per see, nilichogundua wengi wetu tunatumia simu za smart (smart phone) bila ya kujua jinsi ya kui "utilise" hasa kwenye suala zima la "net" mtandao.....iko hivi..smart phone zenye 3G ikiwa activated, kama haujajiunga na bundle then ukaweka credit, "LAZMA UKATWE" maana simu ina automatic updates, so ukicheki salio unakuta linaisha kila baada ya muda, nlishawahi kulalamika sana miaka ya nyuma, lakini baadaye nikaja jua tatizo, so ukitaka usikatwe, wewe jiunge na bundle, au deactivate 3G, utumie 2G, ikikushinda kabisa deactivate data...
...so the problem is within ours, (mashkolo mageni)

hili na mi nimeligundua bt still vd nt yao mizingio compare to others
 
Back
Top Bottom