Habari wandugu, kuna kitu kinasikitisha hivi Dar es salaam tena wilaya ya kinondoni hadi leo hakuna umeme ukiuliza utaambiwa wanaleta. Kuna ndugu yangu anaishi bunju kwenye maeneo ya bunju kulikokuwa na mradi hadi leo hakuna umeme na sasa hivi wameanza kusambaza nguzo lakini kama wewe hujulikani basi utaendelea kukaa giza mpaka tanesco wafurahi ndio utaona umeme hatujui ni lini. Embu tujiulize kweli kuna haki kweli wakati huduma yenyewe utakuja kuilipia na kuiingizia nchi yetu mapato?