TUKUTUKU
JF-Expert Member
- Sep 14, 2010
- 11,763
- 4,046
Nimepatwa na mshangao na utendaji wa tume ya uchaguzi,nilikwenda kuhakiki jina langu kwenye kituo ambacho nilijiandikisha,lakini kwa bahati mbaya sikuliona jina langu katika orodha ya wapiga kura halali.Baada ya kuona hivyo nilijalibu kupiga simu namba +255222199780 ambayo ilitolewa na tume ya uchaguzi ili kujibu maswali ya wapiga kura wenye matatizo,nilipoipiga namba hii waliniambia niwatajie namba ya kadi yangu ya mpiga kura .Baada ya hapo wakaniambia inavyoonekana simo kwenye daftari la kudumu la wapiga kura.Pia wakanishauri nitume namba yangu ya kitambulisho cha mpiga kura kwenda 15455 na nilijibiwa Ombi lako halikufanikiwa,tafadhali hakikisha namba yako ya utambulisho wa kupiga kura kasha tuma tena baadaye.Baada ya hapo, wakanishauri niende posta house Gorofa ya saba ambapo ofisi ya tume uchaguzi ilipo,nikaenda kufika huko wakaniambia niende bohari,kabla sijaondoka wakabadilisha tena na kunishauri niende kwa katibu mtendaji wa kata.Sikuchoka,nikaenda kufika huko,yeye akaniambia sasa kama haupo kwenye daftari la kudumu la wapiga kura unataka nifanye nini?mimi sina uweze wa kuongeza au kupunguza jina nakushauri uwende kwa mkurugenzi wa halmashauri,ambaye ndiye msimamizi mkuu wa uchaguzi katika eneo hili
Sasa mimi nimeshakata tamaa kabisa kwa kuwa inavyoonekana tume ya uchaguzi hawakufanya maandalizi yoyote ya namna ya kushughulikia matatizo ya wapiga kura na hawajui wanachokifanaya,kama wanajua basi wana dhamira mbaya.Walitakiwa wawe na mpangilio maalumu wa kushughulikia matatizo ya wapiga kura.Huu ni ubabaishaji wa hali ya juu.Naomba ushauri wenu ili niweze kupiga kura na kuchagua kiongozi bora.
Sasa mimi nimeshakata tamaa kabisa kwa kuwa inavyoonekana tume ya uchaguzi hawakufanya maandalizi yoyote ya namna ya kushughulikia matatizo ya wapiga kura na hawajui wanachokifanaya,kama wanajua basi wana dhamira mbaya.Walitakiwa wawe na mpangilio maalumu wa kushughulikia matatizo ya wapiga kura.Huu ni ubabaishaji wa hali ya juu.Naomba ushauri wenu ili niweze kupiga kura na kuchagua kiongozi bora.