Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 360,386
- 829,665
Siku kikieleweka mtaa mzima mtajua, mtarushwa roho mwanzo mwisho, akiamka saa nne ataenda sokoni akirudi kanunua samaki, nyama steki na maini nk atajipikisha vyote hivyo nje ya chumba chake tena na kanga moko na taarabu za vijembe juu, wenye waume zao watakoma! Siku hakijaeleweka wanakuwa kama wagonjwa na watagombana na kila mtu, hawataamka mapema na jirani akijipigia taarabu yake atahisi kawekewa yeye! Ni watu ambao mood zao zinaendana na nini kapata siku hiyo.