Una bahati huendeshi ma Yutong. Yutong ya ukweli ukijichanganya ukabebeshwa mamiguu namna hiyo utachemsha...now I see why you prefer hungry emaciated galz
Umenikumbusha nilivyokuwa darasa la tatu tulipangwa wanne kwa dawati moja bahati mbaya dawati zote zikaenea nikabaki mimi pekee yangu, mwalimu akaniambia nitafute dawati lolote nikae.
Kila mtu alinikataa nikakaa chini, jumapili nikaenda shuleni nikaenda darasa la saba kule ni kuchukua dawati nikaenda kulitenga nyuma kabisa darasani kwetu.
Jumatatu kila mtu anashangaa nimetoa wapi dawati, wakati wao wanababana mimi nimejiachia mwenyewe kwenye dawati.