Kitu nilichojifunza kwenye maisha yangu,binadamu tumeumbiwa kuzoea kitu/mtu/jambo. Jaribu kukumbuka wakati unanunua gari yako ya kwanza/unajenga nyumba etc.
Yaan Ile shauku inakuwa kubwa sana wakati huo, sasaaa kaa kidogo uone hali ikoje.
Hata upande huu uliopost,tunazoea na kuona vyakawaida,ndio maana mtu mwenye mke pisi kali,anachepuka na mwanamke wa kawaida kabisa.
Kisa kama hiki kimewahi kunikuta, nilidhamiria kumfunidisha jamaa adabu nikiwa mlevi, wakatusuluhisha, baadaye nikaja kuambiwa ni mtu hatari sana tena usalama wa taifa.