Hadithi za Allan Qurtamain...kazi muhimu katika mlolongo mrefu wa fasihi ya kikoloni iliyolengwa katika kumwonyesha mtu mweusi kama chombo tu cha kumtumikia mzungu. Umslopagasi - mzee shujaa wa Kizulu mwenye uwezo wa ajabu kimapambano; na shoka lake lisilo na huruma (Inkoskazi) hana faida nyingine yo yote mbali na kupigania himaya ya kizungu mpaka kupoteza uhai wake. Ndiyo maana kitabu hiki kilipigwa marufuku sehemu mbalimbali duniani ambako kulikuwa na msisimko wa watu weusi (na wengineo) kujikomboa kifikra.