Jamaa kaamka asubuhi, kavaa track suit na kumuamsha mkewe BETTY
JOHN: Amka twende jogging mke wangu?
BETTY: Alaaa kwa hiyo una maana mi tipwatipwa?
JOHN: Hapana si hivyo jogging ni nzuri kwa afya.
BETTY: Kwa hiyo una maana mi mgonjwa?
JOHN: Basi yaishe endelea kulala
BETTY: Kwa hiyo unaniona mi mvivu sana sio?
JOHN: Hujanielewa mpenzi wangu sikuwa na maana hiyo baby
BETTY: Kwa hiyo mie mjinga mpaka nashindwa kukuelewa?
JOHN: Jamani mi sijasema hilo
BETTY: Kwa hiyo mie muongo?
JOHN: Chonde tusiendeleze haya asubuhi namna hii
BETTY: Kwa hiyo mie ndio naendeleza ugomvi?
JOHN: Sikia we lala mie naenda jogging.
BETTY: Ndio zako hizo mambo yote unafanya peke yako hunishirikishi"
JOHN: Unajua nimeanza kusikia kizunguzungu
BETTY: Unaona nikiongea kidogo unakimbilia kuumwa, mbinafsi sana wewe...
JOHN: Basi ngoja tu nilale siendi jogging
BETTY: Kwahiyo ulikua unanijaribu?
Wanawake Mungu anawaona