Vituko mitandaoni. Tupia chako

Wakija kukupopoa nitakutetea🀣πŸ’ͺ
 
Mkuu bado unakutana naye Gym, natamani nije nipate huduma mahali hapo kama ni mji huu ninaoishi ndipo mlipo.
Kama nje ya Tz basi.

Hiyo ilikuwa miaka 20 iliyopita.

Niliacha kwenda gym baada ya mazoezi ya kitandani kunilemea....πŸƒβ€β™€οΈπŸƒβ€β™€οΈπŸƒβ€β™€οΈπŸ˜πŸ˜πŸ˜
 
Hiyo ilikuwa miaka 20 iliyopita.

Niliacha kwenda gym baada ya mazoezi ya kitandani kunilemea....πŸƒβ€β™€οΈπŸƒβ€β™€οΈπŸƒβ€β™€οΈπŸ˜πŸ˜πŸ˜
HeeπŸ™„.

Umezidisha dozi ya kumburudisha mheshimiwaπŸ€£πŸƒβ€β™‚οΈπŸƒβ€β™‚οΈπŸƒβ€β™‚οΈπŸƒβ€β™‚οΈ
 
HeeπŸ™„.

Umezidisha dozi ya kumburudisha mheshimiwaπŸ€£πŸƒβ€β™‚οΈπŸƒβ€β™‚οΈπŸƒβ€β™‚οΈπŸƒβ€β™‚οΈ

Yaani acha tuu, mzani ulielemea upande mmoja. Ikabidi niwe mtiifu kutoa huduma yakinifu nyumbani plus ni mazoezi yenye raha na utamu...

Gym ukipiga pushup unaumia, squat vivyo hivyo, kuruka kama ndo balaa makalio na matiti kila moja vinarukia upande wake, basi tafrani tupu bin kizaazaa...😁😁😁

Maana kilichonipeleka gym ilikuwa kuongeza pumzi, nilipokutana na zoezi la kuruka kamba ambalo lilikuwa linasambaratisha uelekeo tofauti wa makalio na matiti yangu nika saini out.

Sema pumzi ilikuwa ishaongezeka ongezeka πŸ€ͺπŸ€ͺπŸ€ͺπŸ€ͺ

Mweeh hebu niweke kalamu chini maana kwanza simalizi kuongea halafu nsijeweka mambo hadharani buree watoto wakapofuka masikio...πŸ˜„πŸ˜„πŸ˜„.

Alamsiki.
 

View: https://youtube.com/shorts/8elQi1zkZUI?si=7ZnXr7mDhLaiqe8l
Aliyemuwekea Valuu bibi harusi kwenye maji ya kunywa Mungu anamuona....πŸ€ͺ

Ila, hii ndo namna mke anatakiwa kukaa mbele ya mume wake, unacheza style zote bila kuchoka (muhimu mwanamke uwe na pumzi) hadi mwanaume aombe poo au aseme ajuaa ndo unaacha kucheza... na hapo kashakuachia pasiwedi zote...😁😁😁.

Mwanamke ukijituma kucheza, mwanaume atakutunza tuu...😊

Nimemaanisha kucheza sio kucheza uliyoelewa wewe....πŸ€ͺ.
 
Hili tukio lingetokea kwenye miji ya pwani wabaguzi wa dini na ukabila wangesema mengi.
Kasie bwana!🀣
 
Kasie bwana!🀣


Aaabeeeh....😁😁😁😁

Ila hiyo video imetoa/imenipa taswira namna mke aliyeamua kuolewa na mwanaume haswa aliyekamilika idara zote.

Hii kichwa yangu sijui huwa inatoaga wapi tafsiri, sijui bangee nnazokorogea kwenye chai...!!!??πŸ€”πŸ€”

Anyways acha niendelee kidogo... huyo bibi harusi ametoa namna mke aliyekubali kuolewa aenende kwa mume wake kwa mustakabali mzima wa akili ya mume wako kuwa nawewe..... (maana asili ya mwanaume ni kuwa na wengi, wanaopinga na wapinge kivyao).

Bibi harusi ameonekana tangu mwanzo wa video anacheza non stop kwa furaha, tuweke kituo; mke unatakiwa ukiwa mbele ya mumeo muda wote uwe na furaha na mumeo akuone wewe ndo chanzo cha furaha yake, amani yake, burudiko lake na hapa ndo maana haswa ya mwanamke kuitwa kiburudisho cha mwanaume.... hakuna anayeburudoshwa na mwenye gubu..... kazi kwenu kunyoq au kusuka.... tuendelee....

Mwanaume ana mambo mengi kikubwa wewe ndo amekuoa ni mkewe, akili yake ya chini ikimtuma kwenda nje, usimkague, usimfate fate kufumania aka kutaka kujua yuko wapi yuko na nani anafanya nini...

La muhimu tuu akiheshimu, asiende huko na huko halafu hafuti ushahidi hadi unajua. Mwanaume mshenzi ni yule anafanyq ubaladhuli wake huko makusudi akuudhi huyo ukiweza hata usiolewe nae ni mshenzi wa tabia na ukiwa ndani tayari ujumlishe na kutoa maamuzi ni yako...

Hapo bwanahqrusi alipoenda pembeni wamshikie simu yake, bibi harusi aliona na akasindikiza kwa macho kuhamaki kulikoni, alipotambua namuamini mume wangu akaendelea na dansi lake kwa furaha, mume alirejea na akaendelea kucheza nae.

Hakumuuliza ulikuwa wapi kwa nani ulikuwa unafanyq nini, kalale hukohuko.....!
Bali alimsikiliza akapungiza beats na wakacheza wote hadi mume akablow mwenyewe na kutunzwa juu.


Well msitilie maanani sana alfulela ulela za Kasinde, tuendelee na vituko mitandaoni mambo ya ukungwi tuwaachie makungwi.

Ila kucheza style ya huu wimbo imenishinda kabisa aisee, yaani kila nikijaribu mabega na magoti vinaishia kutetemeka badala ya kucheza kuendana na beats.... sijui ndo uzee...

Alamsiki.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…