Vitabu vya Nyangine vichomwe moto popote vilipo

Umenikumbusha mbali ..

Hivo ndo vitabu bana

yaani nimetaja vichache anaekumbuka vitabu vya kweli aseme hapa kuna vile vya history vya nyerenda,

na vingine vingi bado vipo katika maktba niliona majuzi, nililogundua madogo wavivu sana. Na tatizo ni watoto wenyewe

wasimsingizie mtu. Nyangwine kaja tu kama nini sijui.

chemistry kuna Norman Lambert nani anakumbuka
 
ni kweli vitabu vingi vya nyambali nyangwne vinasaidia lakini tujiulize hiyo ndio elimu bora tunayoitaka, maana km kufaulu kunatokana na kusoma vitabu hafifu basi tukubali elimu yetu ni hafifu .najua kuna watu watataka ushahidi wa hili ninalolisema basi nenda kachukuwe vitabu vya nyangwine uone mambo yalivyorahisishwa na wala hayamjengei mwanafunzi kujisomea vitabu na kuwelewa nini maana ya kinachozungumzwa .wanachofanya wanafunzi wa sasa ni kukariri nini kinasemwa na ndio maana matokeo ya wanafunzi yanazidi kuwa mabovu .hii inatokana na wanafunzi kupoteza muda kukariri majibu kutoka katika vitabu vilivyobase katika mtindo wa maswalina sio kuwelewa somo .kama hamuamini mwakani matokeo yatakuwa mbovu zaidi ya haya.tatizo serikali imejisahau na kuwalaumu walimu hata hili pia ni tatizo katika elimu yetu.
 
Umenikumbusha mbali ..

Hivo ndo vitabu bana

Enzi hizo vijana walikua serious na elimu, wanafunzi walikua wanasoma kweli na hawana vishawishi kama siku hizi ambapo unakuta wako busy na mambo ya kipuuzi na mitihani ikikaribia wanaanza kusoma kwa zimamoto kupitia vijarida vya Nyangwine.
 
Enzi hizo vijana walikua serious na elimu, wanafunzi walikua wanasoma kweli na hawana vishawishi kama siku hizi ambapo unakuta wako busy na mambo ya kipuuzi na mitihani ikikaribia wanaanza kusoma kwa zimamoto kupitia vijarida vya Nyangwine.

Enzi gan hizo mkuu unazozingumzia na wakati mlikuwa mabingwa wa kuiba mitihani, Hiv sasa kuna changamoto nyingi sana sio kama zamani.

Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni
 
kitabu nilichotumia mm ch history f6 wewe hukiwezi, jamaa kasema kweli nyangwine amewaandalia, jiandae vijarida tu

vyuo vikuu mnababaika mby.
 
Vichomwe kabsa,tena hata majivu 2cyaone kamwe!toka ln udadisi na ufanisi ktk kujfunza ukaletwa na vtabu vya maswal na majbu km hv vya nyangwine?!jamaa anaspoil wanafnz,ndo maana cku hz wanafnzi wamekua waviv kutafuta maarfa,coz washazoea short answers!
 
vitabu vya Nyangwine ni kama summaries tu, mwanafunzi mzuri (hata na mwalimu pia) hatotazamiwa kutegemea machapisho hayo kama complete source. mdau anataka vichomwe moto, hakutatatua tatizo la namna wanafunzi wanavyosoma na kuelewa, the whole system is in disarray, mitaala haifuatwi na hakuna vitabu vya kutosha (especially mashuleni). mdau punguza jazba, kwa kuwa umeona kuna tatizo, then ni vyema ukifuatilia ngazi husika na kuwahusisha wadau wote ili kama itawezekana ku petition zuio la utumiaji wa vitabu vya Nyangwine na wengine pia.

lakini pia, labda ieleweke ni vitabu vipi vinavyo ongelewa, alivyo compose huyo jamaa auvyote ambavyo publication company yenye jina lake imechapisha.
 
Nadhan unaesema vichome moto haujasoma shule ya kata.mfano nkiwa sekondari,shule haikuwa na vitab vya notice zaid ya vya nyambari kwa upande wa masomo ya sanaa.na huyu jamaa anakawaida ya kufanya sumary kutoka kwenye vitabu kama major event n.k!anasaidia tena sana,nani anataka awe interlecture alafu afel mtihani?!choma wewe maana havina umuhimu kwako..inawezekana kwenu kuna library ya vitab vya kila aina ndo maana unaweza kujudge ubora.je umejiuliza wangapi hata kitab cha nyambari hana.huyu jamaa anasuply vitab kwa wingi sana na kwa bei ya kawaida...ebu acha fitina.tokea form 1 had 4 tunamtumia nyambari,mbona tumefaulu!!
 
Mtoa mada inawezekana unahaki kabisa ya kuandika hivyo kwa mtazamo na ujuzi ulionao juu ya vitabu hivyo ila bandiko lako halieleweki na inaonekana ni bifu lilipo kati yako na Nyangwine na si vinginevyo. Nakushauri uweke bandiko lenye sababu siyo conclution bila sababu.
Mimi binafsi nimevitumia sana vitabu hivyo, nilichogundua mle jamaa anatoa hints kumfanya mtu anaposoma vitabu vingine aweze kuelewa haraka.
Kwa kizazi chetu cha watu wavivu wa kusoma naweza sema havikidhi matakwa yote ya mwanafunzi na jamaa amepata soko kubwa kwa kuwa watoto wa siku hizi wanapenda mteremko na hawataki kuumiza kichwa.
Mwisho niseme tu kwamba si vizuri kurusha matusi humu jf pindi hoja yako inapokuwa imecrashiwa na watu jaribu kuangalia mapungufu yako then songa mbele.

Yaap....Vitabu vya nyangwine vinatoa hints ambazo kimsingi ndizo zinampa mwanafunzi picha halisi ya anachopaswa kukifahamu.
 
Kwa wale wote wanaojiita walisoma zamani.
KUSOMA KWENU ZAMANI KUNAJIBU HOJA YA MTOA MADA?
jengeni hoja si porojo.
TAMBUENI KUWA VITABU VYA Nelkon,Lambart,Abort na Vingine vingi nimevitumia pia na nilipotoa mfano wa kemia nilikuwa naweka supporting point,kama unataka matokeo yangu yote wala hayasaidii kujenga hoja japo nilifaulu masomo yote 9.
PIA hivyo vitabu vya nje nimevitumia Advance PURE UNDERSTANDING MATHEMATICS,PURE ONE&TWO,NELKON,CHAND,nk.MSIFIKIRIE SIVIFAHAMU HIVYO VITABU ILA HAO MNAOJIITA WA ZAMANI HAMVIJUI VIZURI VITABU VYA NYANGWINE,nimetoa mfano wa kitabu cha maths cha wakamoga mbona hakuna aliyekuja kudhibitisha hakifai,NI UJINGA kuendelea kupinga kitu huku ukishindwa kuonyesha ubovu wake,UNATAKA TUAMINI BILA USHAHIDI,MATHS vya serikali fm1 to fm4 are the worst books HAKUNA ALIYEPINGA AMA KUONESHA VINAFAA just check 1topic logarithm.
Where is the easthetic of your old books in logical argument?
I can't substentiate your ability to argue from a tabularasa way of argument.
SPLENDID Nyangwine.

heko, kiu, ijumaa wikienda na mazombi au nakosea mkuu Bin Masunga viongozi weeengi wameamua kutetea udaku. awali facebook ilikuwa kama Hi5 lakini siku hizi kuna wanaingia facebook kusoma, kupoteza wakati lkn mark akijilia dolali. wewe mtz With you lilttle brain unaacha kuingia kusoma na kutoa arguement za maana unaleta magazeti ya udaku humu? mtabaki hivyohivyo.
 
Yaap....Vitabu vya nyangwine vinatoa hints ambazo kimsingi ndizo zinampa mwanafunzi picha halisi ya anachopaswa kukifahamu.

Twende taaratibu, akishapata mwanga atasoma lini? Wengi wakiwa vyuo vikuu ndio wanajitambua whch is too late.

Mtoto lazima apate mwl mzuri ataejua kucheza na akili yake kutokea chekechea, mtoto akiwa bush school anaanza na kuona na kuzoea mazingira mapya kitaalamu wanaita mountessory age, walimu watakubaliana nami. Ni wakati huohuo mtoto ataanza kutambua mambo mbalimbali. Katika jamii zetu hasaa kusini mwa jangwa za sahara ni maskini sana, shule zimeanza kuwasaidia kutembeza watoto sehemu mbalimbali watoto waone nature/asilia ilivyo, baadae watarudi darasani waanze kuonyeshwa picha na objects mbalimbali na kuanza kuzitambua kwa majina. HII TUTAIITA EXPOSURE kwa plain english. Hii exposure ni muhimu kuliko kitu chochote. Mtoto ataishi nayo popote pale itamsaidia kubalance mambo mbalimbali katika maisha ya mtaani/shuleni/nyumbani.

Sijasoma chekechekea lakini ninakutana na aliesoma chekechekea iliyo na walimu wazuri waliofundwa atanigundua(sina ufahamu kadha wa kadha) na mimi nitamgundua(kumbe mimi sijui 1,2,3..) hapo ni wakati labda tuseme nipo f3 au f4 kwa namna anavyoweza kutambua mambo..mimi nitajifukia library yenye vitabu vya maana simaanishi hivi mnavyosema, nazungumzia vile walivyoandika wasomi wanaotoa paper/majarida/tafiti/publication mbalimbali, watunzi wenye talent kubwa, vitabu vya wakina obama nk ni mfano tu. Baadae nikirejea nimepata a,b,c...lkn bado siwezi kumfikia yule aliyesoma kwa vitendo akiwa bushschool, huwezi ukajifunza kwa ubishi hata siku moja ktk utu uzima wkt huo umeshaanza kuwajua mabinti na wkt mwingine wanakuchanganya na kukulia muda wako. ule muda wa miaka 3,4,5(KG age) ni muhim sana, wengi wenu mlikutana na walimu waliofeli feli f4.

Sishangai wanaotetea nyangwine, simjui nyangwine visually, naona vitabu vyake wkt mwingne nikiwanunulia vitabu anko zangu na aunties, wengi wa watoto mlipewa sumu mapema kindergatten, kUNA UHUSIANO MKUBWA SANA baina ya umri wako na mafunzo unayopata.

Siajabu kuona watu wakiwa na mawazo tofautifauti, ni kwa sababu walilelewa tofauti, walisoma shule tofauti, walifundishwa na walimu tofauti, mwalimu anafilosofia anayompa mtoto na kuathiri maisha yake yote...na ndio maana mwalimu anatakiwa awe ginias, hawa watoto walilishwa vyakula tofauti, na macho yao yalianza kuiona dunia katika perspective flaniflani. Watatofautiana sana ktk mambo yao/matendo/mawazo nk

Kwa mfn mwalimu nyerere tuchukulie anafundisha unategemea huyo mtoto wanafunzi wake atapata athari gani, mwanafunzi kama obama alifundishwa na walimu wa aina gani, mwisho wa siku kila mwanafunzi atatoka kivyake na zile four R(writing,reading,counting) 4th R ni namna mtoto(mwanafunzi) anavyoweza kusimama na kupambanua mambo, hii naweza kuiita Rhythm. sasa bishaneniiii lkn hata wewe unaebisha mapungufu ya baadhi ya vitabu nadhani pia hutagundua madhara kwa kuwa ufahamu haupo
 
Mtoa hoja una chuki binafsi na nyambari,kwanza umeanza na elimu hujamaliza hoja unaanza benki sasa tuelewe nini, kama msomi na uliyeona tatizo ni vema kama ungetoa suluhisho. Kumbuka nchi yetu ilikuwa ikitegemea vitabu kutoka tanzania intitute of education (tie) siku hizi tie hatujui imefia wapi na hawatoi vitabu tena. Unaweza ukawa sahihi lakini kumbuka kama vitabu vya taasisi husika vingekuwepo sokoni tungeacha kuvitumia tena si kwa kuvichoma moto kama ulivyosema.nyambali ameokoa taifa letu kwa kiasi kikubwa sana ktk suala la elimu lkn leo hii anaonekana eti anashusha elimu yetu tusome vitabu vya nani sisi tuliopo shuleni kwa sasa? ni bora kunywa uji kuliko kulala njaa'''
 
Nyambari Nyangwine ameharibu wanafunzi na mfumo mzima wa elimu ya sekondari. Naunga mkono vitabu vyake vichomwe ikiwezekana na yeye pia kwa kuchangia kuzalisha vihiyo na murugo wengi hadi grading system imeshushwa.
 
Jambo usilolijua ni sawa na usiku wa giza. Nyambari Nyangwine ni chanzo cha kufubaa kwa elimu Tanzania. Naona watu wanasukumwa na hisia zaidi badala ya hoja. Binafsi sina ugomvi na Nyangwine ila kazi zake za kutaaluma ndizo zilizo hovyo sana. Tungekuwa katika nchi za watu makini vitabu hivyo serikali ingevikusanya vyote na kuvichoma moto kwa kuwa sio tu havimfanyi mtu apate ujuzi bali vinapotosha ukweli kwa kuandika mambo ya uwongo
 
umeona hata waandishi wake aliotaja huyo aliepata two, wameshakwisha ona hata huo ufafanuzi wake hapo,

anajua competency na content, hawajui tulikuwatunazalisha ng'ombe shule agriculture, mbeya tech, mosh tech balaa

waache wabishe ni kweli ni kama umeingia choo chao[/QUOT jumlisha na haya

wakati wetu wa abot, nelcon nk ndio vitabu vidogo hivyo kulikuwa na vitabu vwa akina erwin vya uchumi na

kwenye uchambuzi wa vitabu ni balaa

utamkuta anajua kubishana tu kufungua facebook
jumlisha na haya

Kizazi hiki Kimeshaahirisha, hakiwezi kikakuelewa:

wakati wetu watunzi wadogowadogo walikuwa namkumbuka mmoja wa usdm alifariki yule mzee

Siku hizi hata ukiongea nao unasumbuka bure mansa

Kwa wale wote wanaojiita walisoma zamani.
KUSOMA KWENU ZAMANI KUNAJIBU HOJA YA MTOA MADA?
jengeni hoja si porojo.
TAMBUENI KUWA VITABU VYA Nelkon,Lambart,Abort na Vingine vingi nimevitumia pia na nilipotoa mfano wa kemia nilikuwa naweka supporting point,kama unataka matokeo yangu yote wala hayasaidii kujenga hoja japo nilifaulu masomo yote 9.
PIA hivyo vitabu vya nje nimevitumia Advance PURE UNDERSTANDING MATHEMATICS,PURE ONE&TWO,NELKON,CHAND,nk.MSIFIKIRIE SIVIFAHAMU HIVYO VITABU ILA HAO MNAOJIITA WA ZAMANI HAMVIJUI VIZURI VITABU VYA NYANGWINE,nimetoa mfano wa kitabu cha maths cha wakamoga mbona hakuna aliyekuja kudhibitisha hakifai,NI UJINGA kuendelea kupinga kitu huku ukishindwa kuonyesha ubovu wake,UNATAKA TUAMINI BILA USHAHIDI,MATHS vya serikali fm1 to fm4 are the worst books HAKUNA ALIYEPINGA AMA KUONESHA VINAFAA just check 1topic logarithm.
Where is the easthetic of your old books in logical argument?
I can't substentiate your ability to argue from a tabularasa way of argument.
SPLENDID Nyangwine.
 
Kizazi hiki Kimeshaahirisha, hakiwezi kikakuelewa:

wakati wetu watunzi wadogowadogo walikuwa namkumbuka mmoja wa usdm alifariki yule mzee

Siku hizi hata ukiongea nao unasumbuka bure mansa
Mkuu, ukisema kuwa kitu fulani hakifai unajenga hoja kwa kuchambua vigezo fulani. Wahakiki wa maandishi wanaweza kufanya kazi hiyo kwa kuonyesha strengths, weaknesses na relevance ya kitabu kwa somo husika, wanaokusudiwa kukisoma, wakati na level inayokusudiwa.
Mimi nimevipitia sana vitabu vya Nyangwine ambopo vingi yeye ana play role ya sponsor. tatizo la vitabu hivi vingi vimeandikwa kama notes na ka vya crash programme. kulikuwa na pengo la vitabu kwa muda mrefu nchini na hivi alipojitokeza Nyangwine akaja na mtindo kama wa crash programme. Basi wakajitokeza watu ambao kimsingi si wataalamu wa uandishi na kandika vitabu hivo tunavyoviona.
tatizo kubwa la hivi vitabu ni kuwa uandishi haujengwi katika logical order. kwamba hoja itolewe ifafanuliwe kwa mifano na evidence kisha ihitimishwe kulingana na hoja iliyotolewa. badala yake vitabu vingi vinatumia mtindo kama outline, highlight, list n.k. na hivi humlazimisha msomaji akariri. mtu ambaye uwezo wake wa kukariri ni mdogo ni vigumu sana kuelewa. wanaosoma vitabu hivi na kufaulu wana uwezo wa kukariri ka aya za Biblia au Qoran.
Wale walioandika wasikasirike bali wakubali kuwa uandishi ni taaluma wa watu husomea na kupaata shahada kuhusu namna bora ya kuandika.
pendekezo langu ni kuwa Serikali na taasisi za elimu hasa elimu ya juu na hasa taasisi ya elimu waweke utaaratibu wa kuendesha mafunzo kwa waandishi wa vitabu vya shule. pia vitaabu vilivyopo vihakikiwe na kuonyeshwa mapungufu ili viandikwe upya. Kimsingi Kuvichoma moto si suluhissho bali ni ni vema kutafuta namna ya kuboresha uandishi.
 
Back
Top Bottom